Skip to main content

Posts

Showing posts from August 14, 2022

MWALIMU SKULI YA MADUNGU KUPANDISHWA MAHAKAMANI PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::: JESHI la Polisi mkoa wa kusini Pemba, litampandisha mahakamani wakati wowote, Mwalimu skuli ya Msingi ya Madungu wilaya ya Chake chake Pemba, Ali Makame Khatib, akidaiwa kumchezea sehemu zake za siri na kisha kumbaka, mwanafunzi wake wa darasa la tano skuli hapo. Taarifa za Jeshi hilo, zilizotolewa na Kamanda wa Jeshi hilo mkoani humo, Abdalla Hussein Mussa alisema, kwa sasa wanaendelea kumuhoji mwalimu huyo, kuhusiana na tuhuma zinazomkabili, na kisha taratibu zikikamalika atafikishwa mahakamani. Alieleza kuwa, awali walipokea taarifa za malalamiko kutoka kwa mama mzazi wa mtoto huyo, akidai mtoto wake, amechezewa na kisha kuingiliwa na mwalimu wake. Kamanda huyo alieleza kuwa, baadae taratibu za kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo, zilifuata na kuanza kuhojiwa juu ya tuhuma hizo. Awali mama mzazi alidai kuwa, aligundua tatizo hilo kwa mtoto wake, baada ya kusikiliza moja ya kituo cha redio kikielezea aina za udhalilishaji. Mama huyo alieleza kuwa, mtoto wake alim

WIZARA YATILIANA SAINI NA 'GWP' KUONDOA SHIDA YA MAJI ZANZIBAR

  NA SALMA LUSANGI, WMNM-ZANZIBAR::: WIZARA ya Maji, Nishati na Madini Zanzibar, imetiliana saini ya makubaliano (MoU)  na taasisi ya 'Global Water Partnership (GWP)'  kuhusu utekelezaji wa mpango mkuu wa maji safi na salama Zanzibar. Hafla hiyo ya kutiliana saini imefanyika mjini, Zanzibar baina ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo Joseph Kilangi na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya GWP Dk. Victor Kongo na  kushuhudiwa na viongozi wakuu na watendaji wa taasisi mbili hizo.     Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Katibu Mkuu huyo alisema kupitia makubaliano hayo Mpango Mkuu wa Maji Zanzibar wa mwaka 2022/2027 utaweza kutekelezeka kwa haraka na kuleta ufanisi ambao Wizara yake inahitaji katika utekelezaji wa huduma ya maji  Zanzibar. Alisema  changamoto zilizopo katika masuala ya maji yanahitaji utafiti wa kina ikiwemo miundombinu ya maji, maeneo sahihi ya kuchimba visima na mambo mengine ya kitalaamu ili Wizara yake iweze  kutatua tatizo la maji  kwa wananchi. “Taasisi ya Global Wate

CITIZENS BRIGERD WAPEWA NENO PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WAHAMASISHAJI jamii kisiwani Pemba, wamekumbushwa kuacha ushabiki wa kisiasa na kumdharau mtu yeyote, wakati wanapofanya ushawishi na utetezi kwa jamii wa kudai haki zao zikwemo za kisiasa na demokrasia. Ushauri huo umetolewa na Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said ofisi kwake Chakechake, wakati akiwasilisha mada kwa wahamasishaji hao. Alisema mshawishi mzuri na mtetezi ni yule anaejitenga na ushabiki wa kisiasa wa moja kwa moja na kuhakikisha anawashirikisha watu wote. Alieleza kuwa jamii itawaamini ikiwa wataweza kuzuia hisia zao kisiasa wakati wanapofanya utetezi juu ya jambo fulani. "Pamoja na sifa kadhaa lakini kujionyesha wazi wazi kwa mshawishi na mtetezi wa kudai haki za wanawake au jamii huweza kumkosesha kusikilizwa na kundi jengine, "alisema. Hata hivyo alisema wakati wanapofanya zoezi hilo lazima wajifunze kuzielewa sheria na kanuni zinazowaongoza. Mapema akiwasilisha ma

WAZIRI AZINDUA UVUNAJI ZAO LA KARAFUU PEMBA, AWAPA NENO WATOROSHAJI, WIZI

          SAID ABDULL-RAMAN, PEMBA   WAKULIMA wa zao la Karafuu Kisiwani Pemba, wametakiwa kuvuna zao hilo, lililopevuka na kuacha kuvuna karafuu changa, kwani kufanya hivyo, ni kupoteza ubora wa zao hilo.   Hayo yalielezwa na Waziri wa Biashara Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Omar Said Shaaban, wakati akizindua zoezi la uvunaji wa zao hilo katika mashamba ya mikarafuu Kichunjuu Mtambili wilaya ya Mkoani Pemba.   Alisema, kuwa endapo wakulima wa zao hilo wataweza kuvuna karafuu zinazostahiki, wataweza kupata faida kubwa kwao na kwa Serikali, kwa kule kuliongezea thamano zao hilo.   Waziri Shaaban alifahamisha kuwa, kwa mwaka huu Serikali imedhamiria kurudisha hadhi ya zao la karafuu ya Zanzibar, kuwa na ubora wake, ambapo tayari Shirika la biashara la taifa ZSTC limeshakaa na wadau wake.   "Mashine ambazo tumeziweka katika vituo vyetu vya kununulia karafuu ziko salama, na zimethibishwa na kuthibitika kwamba zina ubor

KAMATI USTAWI 'BW' YARIDHISHWA UCHAPAKAZI KAMATI ZA KUPINGA UKATILI PEMBA

                                                                                  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMATI ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, imesema kazi inayofanywa na kamati za kupambana na ukatili na udhalilishaji kisiwani Pemba, ni nzuri na zinafaa kuungwa mkono na wananchi, ikiwa wanataka kuondoa matendo hayo. Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mohamed Ahmada Salim, wakati akighairisha kikao maaluma cha kupokea na kujadili ripoti za miezi mitatu za kamati hizo, kilichofanyika ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo Wawi Chake chake. Alisema suala la kufuatilia au kuibu matendo ya ukatili na udhalilishaji kwa jamii, ni jambo zito na huandamwa na changamoto kadhaa, ingawa kwa kamati hizo, zinaonesha mafanikio makubwa. Mwenyekiti huyo alieleza kuwa, matendo hayo hufanyika kwa siri kubwa, hivyo huwa kunahitaji ujuzi na uweledi wa hali ya juu kuyaibua na kisha kuyafuatilia. ‘’Kwa niaba ya kamati hii, lazima wajumbe nyinyi wa