Skip to main content

Posts

Showing posts from June 4, 2023

MAKOMBENI WAOMBA KUONGEZEWA DOZI ATHARI UTIRIRISHAJI MAJI TAKA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Makombeni wilaya ya Mkoani Pemba, wamesema bado wanahitaji elimu zaidi ya athari za utiririshaji maji machafu katika makaazi yao, ili kujiepusha na magonjwa ya kuharisha na kutapika. Wakizungumza na waandishi wa habari waliofika shehiani hapo, walisema bado wapo baadhi yao wamekuwa wakitiririshaji maji hayo, bila ya kujalia afya za wenzao. Walieleza kuw, inawezekana wanaofanya jambo hilo ni kutokujua athari za maji hayo kwa jamii na hasa watoto ambao tahadhari yao ni ndogo. Mmoja kati ya wananchi hao Ali Khamis Juma alisema, moja ya chanzo cha utirirshaji wa maji hayo, ni magonjwa kama ya tumbo la kuharakisha na kutapika. ‘’Ni kweli suala la uchafuzi wa mazingira hasa la utiririshaji maji machafu lipo kwenye shehia yetu, na inawezekana wengi wao hawajui madhara,’’alieleza. Nae Semeni Juma Kheir, alisema hayo yanajitokeza kutokana na kutokuwepo kwa adhabu kali kwa wananchi wanaodharau uchimbaji wa shimo la kuhifadhi maji ya m

‘KINJE KUKU’ UTAMADUNI WA MICHEWENI UNAOWAHUSU WATOTO WA KIKE PEKEE

  NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ UTAMADUNI wa uvaaji kanga ya shingoni, ama kwa lugha Micheweni ‘kinje kuku’ umepotea kwa kasi. Kizazi cha sasa cha Micheweni, na hasa watoto wa kike ambao ndio walengwa wa utamaduni, wameanza kuupa kisigo. Wakionekana, kuachana na vazi hilo, na sasa wakivaa nguo nyingine ambazo wanaona zinawastiri hasa sehemu ya kifuani.   Hiyo ni kutokana na karne ya sasa na utandawazi jinsi ulivyokua, ndipo watoto wa kike wa Micheweni takribani kwa asilimia kubwa kuacha utamaduni huo. Vazi hili lilikua linavaliwa sana na watoto, wengi wao wanaishi vijijini, lengo hasa la kinje kuku, ni kuwastiri watoto hao wa kike sehemu ya kifuani, hasa wakianza kutanuka kifua. Vipo vijiji vyengine vingi katika Mkoa huo   ambavyo watoto wa kike walikua wanavaa vazi hilo kama utamaduni wao, lakini mwandishi wa makala hii aliamua kwenda kwenye kijiji cha Kwale Wilaya ya Micheweni kuzungumza na wazee.   Wilaya ya Micheweni ni Mkoa unaoongoza kwa masuala mbali mbali ya utam

WASIOJULIKANA WAIBA MAZAO YA BAHARINI MTAMBWE PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WATU wasiojulikana, wamevamia na kuiba Kaa na Vitango bahari, waliyokuwa yakifugwa na wanaushirika wa ‘yashasemwa’ uliopo shehia ya Mtambwe kusini, wilaya ya Wete Pemba. Watu hao kwa nyakati tofauti, wanadaiwa kuiba Kaa 80 kati ya 120 waliyoyaingiza na Vitango bahari kuibiwa yote 1,000 kwa nyakati za usiku.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, viongozi wa ushirik huo, walisema wizi huo umefanyika miezi mitano, baada ya kuweka vifaranga hivyo, kwa ajili ya ufugaji. Msaidizi wa Mwenyekiti wa ushirika huo Jabir Saleh Jabir, wamepatwa na mshangao mkubwa, baada ya kupokea taarifa za kuibiwa, kwenye shamba lao. Alisema, walitumia gharama kubwa kuanzisha maeneo hayo husika, kwa ajili ya ufugaji wa vitango bahari na Kaa, ingawa watu wasiowafahamu, waliwarejesha nyuma kwa kuwaibia. ‘’Na sisi ni ushirika ambao tuna nia ya kuvuna matunda ya uchumi wa buluu, na tulishajikusanya na kuunganisha nguvu zetu, lakini wengine waliamua kuturejesha nyuma,’’a

MWENGE WA UHURU WATUA PEMBA, WAANZA WILAYA YA WETE UFUNGUZI WA MIRADI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MWENGE wa uhuru umewasili kisiwani Pemba, ukitokea Mkoa wa kaskazini Unguja, tayari kwa ajili ya kukimbizwa katika wilaya nne za Pemba, samba mba na ufunguzi wa miradi kadhaa, ikiwemo ya maendeleo kisiwani humo. Mwenge huo umepokelewa jana, katika uwanja wa ndege wa Karume Pemba, ambapo wananchi wa mikoa miwili ya Pemba, wakiongozwa na Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk Khatib, wamejumuika. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa kaskazini Unguja Ayoub Mohamed Mahamoud, alisema mwenge huo ukiwa mkoa mwake, ulizindua miradi minane ya maendeleo na program nne, yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 14.4. Alisema wakimbiza mwenge, walitoa ujumbe kwa wananchi, ukiwemo suala la uhifadhi na utunzaji wa mazingira, lishe na kupinga rushwa na kisha kuchunguza afya kwa wananchi. Mkuu huyo wa Mkoa, alisema katika kipindi hichi, walipanda miti 120,000, ingawa katika shamra shamra za mwenge wamepanda miti 2,500. ‘’Mkuu wa mkoa wa kas