Skip to main content

Posts

Showing posts from May 19, 2024

MASHEHA PEMBA WASHIKWA SIKIO UUZAJI, UNUNUAJI ARDHI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MASHEHA kisiwani Pemba, wameonya kutojishusisha na uuzaji wa ardhi, kwani sheria zinazosimamia ardhi, hazitambui nafasi yao, katika zoezi la awali la uuzaji ama ununuaji.   Ushauri huo umetolewa leo Mei 25, 2024 , na Hakimu wa mahkama ya ardhi ya mkoa wa kusini Pemba, Abdalla Yahya Shamuuni, wakati akijibu maswali ya wananchi wa shehia ya Kukuu Kangani, wilaya ya Mkoani, kwenye mkutano wa wazi, uliondaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar, kupitia mradi wa upatikanaji haki, unaofadhiliwa na UN-WOMEN kupitia Umoja wa Ulaya ‘EU’.   Alisema, sheria ya Ardhi, zinaanza kutambua kazi ya sheha wa eneo husika, lililouzwa ardhi, wakati wa uhaulishaji, ambapo hapo yatahitajika maoni yake, pamoja na ya Mkuu wa wilaya.   Alieleza kuwa, ni kosa kwa sheha, kujihusisha na mauziano ya ardhi, ingawa hutakiwa kuwepo kama shahidi, ili kuwa na taarifa sahihi zinazoendelea katika eneo lake.   ‘’Sheha hahusiki moja kwa moja wakati wa mauziano

WATOTO WA KIKE BADO NGOMA NZITO KUSHIRIKI MCHEZO WA SOKA

    HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@    Ushiriki mdogo kwenye michezo kwa watoto wa kike, Kisiwani Pemba ni sababu moja inayopelekea wanawake kuwa nyuma katika sekta hiyo.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti kisiwani humo, wananchi hao walisema bado wanawake ushiriki wao ni mdogo, katika michezo ya aina mbali mbali, hivyo jitihada zinahitajika kuhakikisha nao wanashiriki kama walivyo vijana wa kiume.     Said Ali Said wa Mkoani, alisema watoto wa kike huishia maskulini kushiriki michezo na wanapomaliza hawajiendelezi na wala hakuna mtu wala taasisi ya kuviendeleza vipaji hivyo.   "Wapo watoto wa kike wanakuwa wazuri tu katika michezo mbalimbali, kama mpira wa miguu, kikapu, mpira wa Pete na mengine, lakini cha kusikitisha ni kuwa baada ya kumaliza skuli hawajiendelezi tena,"alisema.   Massoud Ali Mohamed wa Chake Chake, alisema kutokana na changamoto ya mavazi, kunasababisha kudumaza kwa michezo kwa watoto wa kike.   Alifahamis

MAHKAMA KUU TANZANIA KUJENGA KITUO JUMUISHI CHA HAKI PEMBA

NA HASSINA KHAMIS, PEMBA@@@  JAJI Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhani Abdalla, ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kusimamia  na kudumisha Muungano kwa maendeleo ya wananchi  wote. Alisema hayo kwenye hafla ya utiaji saini ya mkataba wa ujenzi wa kituo jumuishi cha haki Pemba katika ukumbi wa ZRA Gombani Chake Chake. Mkataba huo wenye ishara ya kuimarika kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ulisainiwa kati ya Mtendaji mkuu wa Mahakama ya Tanzania Profesa, Elisante Ole Gabriel na Mkandarasi wa kampuni ya Deep Construction Mr, Ravinder Singh Jabbal . Alisema ujenzi utajengwa kwa fedha za mkopo   kutoka benki ya Dunia kupitia Mahakama ya Tanzania, ambapo utawawezesha wananchi wa Pemba, kurahisisha kupata haki zao bila ya usumbufu wowote. Aidha nae Mtendaji mkuu wa Mahakama Tanzania Prof:  Elisante Ole Gabriel, alisema kituo hicho jumuishi kitajegwa kwa fedha za mikopo, yenye gharama nafuu iliyoombwa na Mahakama ya Tanzania kwa

WADAU WA HABARI ZANZIBAR WAIKUMBUSHA TENA SMZ JAMBO LAO

  NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR@@@@ WADAU wa vyombo vya habari wameiomba serikali ya Mapinduzi Zanzibar kukamilisha mchakato wa marekebisho ya sheria za habari zilizotolewa maoni na wadau ili  kutoa mazingira rafiki kwa waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao bila vikwazo.   Imeelezwa kwa muda mrefu licha ya wadau mbalimbali kutoa na kuwasilisha mapendekezo yao kuhusu mapungufu yaliyopo kwenye baadhi ya sheria hizo, lakini utekelezaji wake bado umekuwa wa kusuasua jambo linalopelekea mazingira magumu ya utendaji kazi wa vyombo vya habari nchini.   Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ), Dkt. Mzuri Issa alieleza mchakato wa mabadiliko ya sheria za habari umekuwepo kwa miaka mingi lakini bado sheria hizo ambazo nyingi ni za muda mrefu zimekwama kurekebishwa.   "Sisi wengine tangu tuko waandishi chipukizi tunazungumzia kupata hizi sheria mpya za habari, tangu 2008 kwa kweli ni muda mrefu, tunahitaji kusimamia jambo hili kwa umoja wetu na hatimae

DK. FADHIL ATAKA WANANCHI KUUNGA MKONO NJIA ZA KUONDOA SARATANI YA MLANGO KIZAZI

 NA  ASHA  ABDALLA ,PEMBA@@@@ Afisa Mdhamini Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekazaji Pemb Dk., Fadhila Hassan Abdalla amewataka wananchi wa kisiwani Pemba, kushirikiana na uongozi wa mradi wa Head of Jasmine kutoka China,  katika kuondoa tatizo kubwa la saratani ya mlango wa kizazi ambalo linaongezeka kwa kila mwaka . Ameyasema hayo leo katika Hospitali ya Chakechake wakati alipokua akifungua kambi ya Madaktari wa kichina itakayo kuwepo kwa muda wa wiki mbili kisiwani hapa, kwa ajili ya kufanya matibabu ya magonjwa hayo katika hospitali na hata vijijini  Alisema kuwa wanachi hususani akina mama wawe na utayari wa kuhamasishana katika kutoa ushirikiano mkubwa, ili kupatiwa tiba iliyo sahihi na kuondokana na maradhi ambayo yanaongezeka siku hadi siku. Akitowa takwimu ya ongezeko la saratani ya mlango wa kizazi Tanzania, alisema kuwa kumefikia  ongezoko la watu 10,242 ambao nisawa na asilimia 34.4,  waliopata maradhi hayo  nchini hapa. Nae Daktari kutoka China  Xiaomin Qi alisema kuwa, m

MAAFISA USTAWI: ‘ONGEZENI MAARIFA KUKABILI MAJANGA NDANI YA JAMII’

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAAFISA ustawi wa jamii kisiwani Pemba, wamekumbushwa, kuongeza maarifa zaidi, ili kukabiliana na majanga yaliomo katika jamii, kwani wao ndio wahusika wakuu, katika kuilea jamii.   Walielezwa kuwa, jamii imekuwa ikiwapelekea vilio vyao mbalimbali, hivyo wasipokuwa makini kuongeza maarifa ya utatuzi wa majanga, utoaji wa ushauri nasihi na malezi ya kisayanysi, wanaweza kupoteza uaminfu wao, kwa jamaii.   Hayo yameelezwa leo Mei 19, 2024 na Mkurugenzi wa Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, wakati akiyafungua mafunzo ya siku tano (5), kwa maafisa walioko serikalini na wale wa mtaani, kwenye mafunzo yanayoendelea, skuli ya maandalizi Madungu Chake chake.   Alisema, kila siku ndani ya jamii, kumekuwa kukiibuka majanga mapya, hivyo kama hawakuwa makini kuongeza maarifa, ya jinsi gani ya kuisadia jamii, wanaweza kukosa kazi kuachwa nyuma baadae.   ‘’Kila siku huzuka majanga mapya, kwa mfano watoto kubakwa, kulawitiwa,

HIFADHI YA MAZINGIRA KAMBINI, YASEMA WAANDISHI NGUZO YA MAFANIKIO

  NA HAJI NASSSOR, PEMBA@@@@   UONGOZI wa Jumuiya ya uhifadhi wa mazingira ya kijiji cha Kambini Kichokochwe, wilaya ya Wete Pemba, umesema kuwa, ukitaka kufanikiwa katika utekelezaji wa jambo lolote, ni vyema kuwashirikisha waandishi wa habari.   Ulisema, kutokana na kuwa na suati pana na ya haraka, wanaweza kufanikisha kampeni yoyote, ambayo jumuia, jamii au serikali kuu imeamua kuwafikia wananchi wake.   Kauli hiyo imetolewa leo Mei, 19 na Katibu wa Hifadhi hiyo, Bakari Suleiman Juma, wakati akizungumza na wanachama wa jumuiya ya waandishi wa habari Pemba ‘PPC’ na wananchi wingine, kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari dunia, ambapo waandishi hao, waliiadhimisha kwa upandaji wa mikoko.   Alisema, waandishi wa habari, wamekuwa na mchango mkubwa, katika kufakikisha kila kitu, mfano zoezi la uhamasishaji upandaji miti hiyo, hivyo kwa tukio hilo, limewapa hamasa.   Alieleza kuwa, aanamini jamii ya Tanzania, itapata mwanga wa kuhakikisha wanapan