Skip to main content

Posts

Showing posts from July 24, 2022

WADAU WA HABARI PEMBA WAVIONESHEA KIDOLE VIFUNGU KANDAMIZI KWA WAANDISHI

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA WADAU wa habari kisiwani Pemba wamesema, kuwepo kwa baadhi ya vifungu vya sheria visivyo rafiki kwa wanahabari vinasababisha kunyima uhuru wa vyombo vya habari nchini. Wakizungumza wakati wa mkutano wa kukusanya maoni ya wadau juu ya maboresho ya vifungu  vinavyominya uhuru wa habari, uliofanyika TAMWA Pemba, wadau hao walisema, kuna haja ya kuwekwa sheria ambazo zitawasaidia waandishi wa habari kufanya kazi zao bila vikwazo. Walisema kuwa, habari ni muhimu sana na ndio chanzo cha maendeleo katika nchi, hivyo ni vyema vifungu vya sheria vilivyo na mapungufu vifanyiwe maboresho na visivyofaa viondoshwe kwa maslahi ya wanahabari na jamii kwa ujumla. "Kwa kweli baadhi ya vifungu vyetu vya sheria havipo huru kwa wanahabari kwa sababu upande mmoja wamepewa uhuru lakini upande wa pili unapokonywa, kwa hiyo sio rafiki vinahitaji kurekebishwa", walisema wadau hao. Said Rashid Hassan kutoka kituo cha Huduma za Sheria Pemba alipendekeza kuwepo kifungu kitakachom

FCS YAAHIDI KUENDELEA KUFANYAKAZI NA ZLSC

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::  email: hajipembatoday@gmail.com TAASISI ya Foundation for Civil Society ‘FCS’ ya Tanzania bara, imesema itaendelea kufanyakazi kwa karibu na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’, ili kuhakikisha jamii inajengewa uwezo, wa kutatua migogoro kwa njia mbadala za amani na haki. Hayo yalieleza na Afiss programu kutoka tasisi hiyo Eveline Mchau, wakati akiwasalimia wananchi wa Kibubunzi shehia ya Shumba Mihogoni, wilaya ya Micheweni, kwenye mkutano wa wazi wa kutoa elimu ya utatuzi wa migogoro, kwanjia mbadala. Alisema ‘ZLSC’ imekuwa ikifanya vyema kwenye kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria kwa wananchi bila ya malipo, jambo ambalo wao limewavutia. Alieleza kuwa, kinachofanywa na ‘ZLSC’ cha kuwaelekeza wananachi namna bora ya utatuzi wa migogoro, hasa kwa kesi za madai, ni jambo jema, na tasisi yao inapendezewa mno. ‘’Wananchi, wakati umefika kutozitumia sana mahakama hasa kwa migogoro ya madai, na badala yake tuitumie elimu tunayopewa na wenz

WANAWAKE WAJASIRIAMALI KWENYE MASOKO, MADIKO WAKOGA MATUNDA YA UCHUMI WA BULUU PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA ‘KABLA ya kuongezeka kwa wavuvi na wachuuzi hapa soko  la samaki Mkoani, nilikuwa mauzo yangu ya uji na maandazi ni shilingi 35,000 kwa siku, lakini sasa yamezidi mara mbili,’’anasema Aisha Hemed Khalifa. Anasema, kwanza hakujua nini sababu ya kuongezeka kwa wavuvi na wachuuzi kwenye soko hilo, na alijikuta akiishiwa na biashara yake kabla ya saa 5:00 asubuhi muda aliouzoea tokea zamani. Kwa kwaida, alishazoea anapoanza biashara yake hiyo, humaliza kati ya saa 5:00 hadi 5:30, ingawa kuanzia mwezi Januari mwaka huu hali imebadilika. Biashara yake hiyo aliyoianza miaka mitano sasa, anasema ilikuwa ya kusua sua, kutokana na kuwa na idadi ndogo ya wavuvi na wachuuzi (wateja) kwenye soko hilo. Awali aliacha biashara ya duka la vyakula, na kujiingiza kwenye uuzaji wa uji na maandazi, sokoni hapo Mkoani, ili kuongeza pato lake. Akiwa kwenye soko hilo anasema biashara ilikuwa ya kudoro dora kiasi, ingawa pato lake lilikuwa tofauti, ikilinganishwa na biashara

SAADA KHAMIS: MWALIMU WA MADRASSA MWENYE ULEMAVU ANAYEFUNDISHA KWENYE MAZINGIRA MAGUMU

NA FATMA HAMAD, PEMBA ‘’KIPINDI cha mvua   wanafunzi hulazimika niwafungie   wasije madrasani mpaka   zitakapo malizika,’’ hayo ni maneno ya Sada   Khamis   Hamad   mwenye ulemavu wa viungo   ni   mwalimu wa madrssa. Kwake anasema ulemavu alionao   haukua mzigo kuwa   asitimize ndota zake za kuwa mwalimu wa madrassa. Hii ni baada ya kuukosa uwalimu wa skuli kutokana na changamoto za hapa na pale, ingawa hakukata tamaa. ‘’Nilikuwa natamani siku moja niwe darasani nafundisha    ila sikubahatika, kusoma skuli hata darasa moja, kwani ilikuwa iko maeneo ya mbali na siwezi kutembea,’’anakumbuka.   Ukosefu wa kiti mwendo kwa wakati huo, na hasa kutokana na ukata wa fedha waliokuwa nao wazazi wake, ulimkosesha elimu ya skuli. Yote hayo ni masikitiko ya Mwalimu wa Madrasa ya Qur-aan   Sada Khamis Hamad mwenye ulemavu wa viungo anaeishi katika kijiji cha Shumba Vyamboni Wilaya ya Micheweni Pemba. Maalim Sada Khamis Hamad ambae ni mtoto wa sita   katika familia yao, anasema suala la

ZLSC: 'TATUWENI MIGOGORO KWA NJIA MBADALA ZA AMANI NA HAKI '

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KITUO cha Huduma za Sheria Zanzibar, ZLSC kimewashauri wananchi wa shehia ya Wingwi Njuguni wilaya ya Micheweni Pemba, kikitumia kituo hicho wanapokuwa na migogoro mbali mbali, ili kupata sulhu kwa njia ya amani na haki. Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa Kituo hicho Pemba, Safia Saleh Sultan, wakati akizungumza na wananchi hao, kwenye mkutano wa wazi wa kutoa elimu ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala za amani na haki, uliotanguliwa na igizo. Alisema, ZLSC imekuwa ikibuni njia kila siku, kuhakikisha wananchi wanajengewe uwezo wa kujua sheria na kanuni,   na kisha weweze kutatua migogoro kwa njia ya amani, hasa kwa kesi za madai. Alieleza kuwa, migogoro ya kesi za madai kama vile ya ardhi, ndoa, matunzo ya watoto, madeni baina yao ni vyema wakavitumia vikao vya familia, kuyamaliza. ‘’Kesi kama hizi mnapokimbilia mahakamani, kuna athari kadhaa moja wapo ni kupoteza muda, fedha na kuchelewa kupatikana sulhu, ambayo itakuwa endelevu,’’alifafanua. Aki