Skip to main content

Posts

Showing posts from July 2, 2023

TAMWA -ZANZIBAR "SHERIA, SERA ZINAZOLENGA KUPUNGUZA UDHALILISHAJI KWA WATOTO ZITUPIWE JICH0"

  Na Najjat Omar – Unguja.   Wadau wa masuala ya kijamii na kijinsia wamekutana kwa pamoja kuzungumzia sera na sheria zinahusu masuala ya unyanyasaji wa kijinsia na mapungufu yake.   Mkutano huo ambao umeendaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Zanzibar –TAMWA uliokutanisha wadau kutoka katika Taasisi mbalimbali za kijamii na kiserikali kujadili juu ya ufuatiliaji,utekelezaji na kutoa maoni juu sera na sheria zinahusu masuala ya udhalilishaji wa kijinsia kwa jamii hususan watoto.   Takwimu kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali inaonesha matukio hayo yameongezeka kutoka matukio 1,222 mwaka 2021 hadi matukio 1,360 mwaka 2022, ongezeko ambalo ni la matukio 138.   Takwimu hizo zinaonesha kwamba kwenye matukio 1,361 yaliyotokea mwaka 2022, matukio 1,173 yalijumuisha watoto, 185 yalihusu wanawake na matatu yalihusu wanaume. Kwenye matukio 1,173 ya watoto, 889 walikuwa ni wasichana, huku 284 walikuwa ni wavulana.   Akifungua mkutano huo Afisa miradi kutoka TAMWA –Pemba Fathiya M

TAMWA CHAWAKUTANISHA WADAU WA TEKNOLOGIA NAMNA YA KUPUNGUZA UDHALILISHAJI

    Na Najjat Omar – Unguja.     Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Zanzibar –TAMWA, wamewakutanisha wadau mbalimbali katika kujadili masuala ya ukuaji wa teknolojia kwenye dhana ya kupunguza vitendo vya udhalilishaji.   Majadiliano hayo yalifanyika katika ukumbi wa Raha Leo ulipo kisiwani Unguja kwa kuwakutanisha wadau wa masuala ya kijamii kama viongozi wa kisiasa,walimu,wanafunzi, viongozi wa dini,Jeshi la Polisi,Mahakimu pamoja wadau kutoka Mahakamani.   Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wanawake TAMWA –Zanzibar Asha Abdi amesema licha ya ukuaji wa teknolojia kurahisisha masuala ya ujifunzaji kwa watoto ila kwa   upande mwengine unachochea udhalilishaji wa watoto kuiga hata kufanya na kujifunza mambo mabaya.   “Ukuwaji wa teknolojia umekuwa mkubwa ambapo nao una changamoto zake ,watoto wanajifunza mambo huko kwenye mitandao na kujaribu kwa kufanya sasa hii teknolojia pia inachochea sana masuala ya udhalilishaji kwa watoto kama jamii tunatakiwa tujit

'WAHARIRI MASHINE NYOOFU UKUZAJI, UIMARISHAJI LUGHA YA KISWAHILI'

  NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIAR   JUHUDI za wahariri kutoka vyombo mbali mbali vya habari nchini zimesaidia kwa kiasi kikubwa kukuza na kuleta mabadiliko katika matumizi  ya Kiswahili fasaha na sanifu nchini. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameyasema hayo katika Mkutano wa wahariri wakuu wa vyombo vya habari  kuelekea maadhimisho ya siku ya Kiswahili Duniani uliofanyika Ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.  Amesema wahariri wakuu wana jukumu la kupitisha na kuweka sawa maandishi yote ndani ya Vitabu, Magazeti na majarida hatua ambayo imesaidia kwa kiasi kikubwa kukuza lugha ya kiswahili . Aidha  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewataka wahariri kulinda Maadili ya kazi zao katika kuyaibua mambo mbali mbali yasiyoendana na mila, tamaduni na silka zetu bila ya kumuonea Mtu au Taasisi fulani. Sambamba na hayo Mhe. Hemed  ameeleza kuwa kuna fursa nyingi zinazopatikana katika lugha ya Kiswahili na kuwataka wenye ujuzi w