Skip to main content

Posts

Showing posts from June 30, 2024

'MADEO' AIBAKISHA WAWI STAR MSIMU WA LIGI UJAO

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TIMU ya Wawi star, imejihakikishia kubakia ligi daraja la kwanza kanda ya Pemba msimu ujao, baada ya jana kuichakaza Azimio SC kwa mabao 3-2, kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Ngere ngere Jeshini, majira saa 10:30 jioni. Kwa timu ya Wawi star, mchezo huo kwao ulikuwa na maana pana, ili wajihakikishie kubakia kwenye daraja hilo, hasa kwa vile mchezo unaofuata wataumana na Junguni anayesaka alama za lazima za kuongoza ligi hiyo. Katika mchezo wa jana, ambao uliohudhuriwa na watazamaji wengi, ulianza kwa kasi, huku kila timu ikiangalia ulipo udhaifu wa mwenzake, ili aondoke na alama tatu muhimu. Katika kuhalalisho hilo, Wawi star ilianza kuwafurahisha washabiki wake, mnamo dakika ya 15, pale mshambuliaji wao hatari Suleiman Seif ‘Madeo’ alipotikisa nyavu kwa bao la kwanza. Lakini Azimio SC, kwa vile walishaazimia ushindi, walisawazisha bao hilo, mnamo dakika ya 34, kwa shuti la mbali lililopigwa na mlinzi wao Salum Kazumar, na kujaa wavuni. Ingawa ‘Ma

TAMAA YA MAHARI, MKAJA WA WAZEE WAKATISHA NDOTO ZA WATOTO WA KIKE MFIKIWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAHARAKATI wa haki za watoto shehia ya Mfikiwa wilaya ya Chake chake, wamesema tamaa ya mahari na haki ya wazee (kilemba cha wazee), ni miongoni mwa sababu, zinazochangia watoto kukatishwa masomo kwa kuozwa waume mapema. Walisema, baadhi ya wazazi wamekuwa wakikimbilia haki ya wazee na mahari, wakati mtoto wake anapotokezea muume, na hivyo kumkatisha masomo kwa tamaa hiyo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, walisema hiyo ni miongoni mwa sababu moja kubwa, ambayo sasa husababisha watoto, kukatishwa masomo. Mratibu wa wanawake na watoto shehiani humo Kheriyangu Mohamed Ali, alisema pamoja na elimu wanayoitoa, lakini bado wapo wazazi wamekuwa wazito kubadilika. Alieleza kuwa, na hasa pale inapotokezea kuna mtoto ni mtoro masomoni, ndipo hapo wazazi huchukua nafasi hiyo, kuwakatisha masomo. ‘’Hapa shehiani, wapo wazazi na walezi wamekuwa wakivutiwa mno na yale mahari na fedha za wazazi (kilemba cha wazee), hivyo huwa rahisi kuw

RIPOTI: WAANDISHI WA HABARI ZA MAZINGIRA NA HALI YA HEWA WAKABILIWA NA UKOSEFU RASILIMALI NA VITISHO

    Ripoti ya hivi karibuni ya Internews, iliyofanywa kupitia mpango wake wa Uandishi wa Habari za mazingira kupitia shirika lake la Earth Journalism, imetoa tathmini ya kina kuhusu hali ya uandishi wa habari za hali ya hewa na  mazingira duniani . Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi chache zilizojumuishwa katika utafiti huu wa kimataifa, ikitoa maarifa muhimu kuhusu mitazamo na uzoefu wa waandishi wa habari katika eneo hilo. Matokeo yanaonyesha kuwa kwa Tanzania nan chi nyingine uandishi wa habari za mabadiliko ya hali ya hewa na masuala ya mazingira umeongezeka kwa kiasi kikubwa. Kuongezeka kwa habari hizi kunahusishwa hasa na matatizo ya mazingira yanayozidi kuongezeka na, kwa kiwango kidogo, kuongezeka kwa hamu ya jamii kufhamu kuhusu masuala haya muhimu ya mazingira. Ripoti hiyo inaonyesha kwamba Asilimia 82 ya waandishi wa habari duniani kote walikubali kuwa habari za hali ya hewa na mazingira kwasasa zina umuhimu zaidi ikilinganishwa na miaka kumi oiliyopita.. Hata hivyo,

KWA NINI SHERIA MPYA YA HABARI NI MUHIMU ZANZIBAR

  NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR Ni takriban miaka 20 sasa, shauku ya waandishi wa habari pamoja na watetezi wengine wa haki za binaadamu Zanzibar kuona nchi yao inapata sheria rafiki za habari imekuwa ikitimizwa kwa maneno. Viongozi wa ngazi mbalimbali serikalini wamekuwa wakitoa ahadi lakini utekelezaji wake unasuasua. Tangu alipoingia madarakani, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amekuwa akionesha kutambua umuhimu wa sekta ya habari kusimamiwa kwa kutumia sheria zilizo rafiki, kwa vile si mkosefu wa kujua ukweli kuwa sheria zilizopo ni kongwe zisizoendana na mazingira mapya yanayochagizwa na kasi ya ukuaji wa sayansi na teknolojia. Akiwa amekalia kiti cha Ikulu baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, Dk. Mwinyi hakuchukua muda kusikika akitoa matamshi yenye mtizamo wa kupendelea waandishi wawe na uhuru zaidi wa kufanya kazi zao, kwa kuamini kuwa itarahisisha manufaa ya utendaji wao kuwafikia wananchi kwa ukamilifu. Mara baada ya Baraza la