Skip to main content

Posts

Showing posts from September 10, 2023

IDARA YA KATIBA KUWASAKA WASIOJISAJILI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MKURUGENZI wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, amesema msako mkali unakuja kuwabaini watu na taasisi, zinazofanyakazi za kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria, pasi na kujisajili kama sheria inavyotaka. Alisema, Sheria ya namba 13 ya mwaka 2018 ya Msaada wa Kisheria   Zanzibar, inamtaka mtu yeyote au taasisi inayotaka kujishughulisha na kazi hiyo, kwanza kujisajili, ili kuwa halali kufanya kazi hiyo. Alieleza kuwa, Idara imebaini wapo watu na hata taasisi zinaendelea kutoa ushauri, msaada na elimu ya kisheria, bila ya kujisajili, jambo ambalo ni kosa kwa mujibu wa sheria hiyo. Mkurugenzi Hanifa, aliyasema hayo Septamba 16, 2023 ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makoyo Wawi Chake chake Pemba, wakati akijibu hoja za baadhi wa wahusika wa msaada wa kisheria, kwenye mkutano wa nusu mwaka, ambao umeandaliwa na Idara hiyo, kwa kushirikiana na UNDP. Alieleza kuwa, msako utanzia katika wilaya za Wete, Micheweni, Chake cha

UNESCO: ''MKIWA WABUNIFU MAAFISA HABARI WANANCHI WATAJUA KINACHOENDELEA SERIKALINI''

  NA SHAIB KIFAYA, PEMBA@@@@                      MAAFISA habari Kisiwani Pemba, wametakiwa kuwa wabunifu zaidi kutokana na   kukuwa kwa teknologia ya habari, ili kuifikishia jamii taarifa sahihi, kwa maendeleo ya taifa . Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Hassan Khatib Hassan, alipokuwa akifungua mafunzo ya siku mbili, kwa maafisa habari, uhusino wa Wizara na tasisi za serikali na waandishi wa habari, uliofanyika Gombani Chake chake. Alisema licha ya kuwa na ukosefu mdogo wa utendaji na vitendea kazi, bado kuna umuhimu wa kupambana na kuisaidia jamii, juu ya kupata taarifa bora na za uhakika. Alifahamisha, kwa sasa taarifa nyingi zisizokuwa sahihi zitawa katika mitando ya kijamii, hivyo ni vyema kwa maafisa hao na vyombo vya vijana wengi wasiokuwa na taaluma   kuwa wepesi na haraka kuilezea jamii juu ya usahihi na taarifa husika. Kwa upande wake Naibu Katibu Mtendaji Idara ya Program, Tume ya Taifa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ‘UNESC