Skip to main content

Posts

Showing posts from June 25, 2023

WAJASIRIAMALI WATAKA MITAJI KUPIGA HATUA

  NA KAIJE SALIM, ZANZIBAR@@@@ Wajasiriamali wameomba kupatiwa mitaji ili waweze kujikwamua kutoka katika hali moja ya kimaisha na kuelekea kwenye hali nyengine ya kipato cha juu. Ombi hilo limetolewa na wajasiriamali walioshiriki katika mafunzo yaliyo tolewa na SMIDA huko Maruhubi chuo cha utalii. Miongoni mwa washiriki hao ni Aisha Said Omar  wameeleza wamekuwa wakishindwa kujikwamua kimaisha kutokana na mitaji midogo waliyonayo. Chales Silima kutoka kutoka Mamlaka ya mitaji  na dhamana amesema wamekuja Zanzibar kutoa elimu ili wafanya biashara na wajasiri amali wapate kujiendeleza zaidi Amesema mafunzo hayo yatawawezesha hasa vijana kuanzisha majukwa yakujiendeleza kibiashara na kujiwezesha  kufikia katika kuongeza kipato. Kwa upande wake mkurugenz mkuu  Wakala wa maendeleo ya Viwanda vidogo na vyakati SMIDA Soud Said Ali amesema wataendelea kushirikiana wajasiri amali kwa kuwapatia mafunzo iliwapate kufanya kazizao za uzalishaji kwa usahi na kufikia malengo waliyo yakusudia.

WADAU WA KUPINGA UDHALILISHAJI WALIA UTOROSHWAJI WATUHUMIWA PEMBA

  NA HANIFA SALIM, PEMBA@@@@ WADAU wa Kamati ya kupinga udhalilishaji Kisiwani Pemba wamesema, kukimbizwa kwa watuhumiwa hususani kesi za wanafamilia, ni moja ya changamoto zilizopo zinazorejesha nyuma juhudi zao za kupunguza matendo hayo. Waliyasema hayo katika kikao kazi cha kuwasiliasha ripoti kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Juni mwaka huu kwa kamati za kupinga udhalilishaji Kisiwani humo, kilichofanyika ukumbi wa ofisi ya Chama cha waandishi wa habari wanawake (TAMWA) Mkanjuni Chake chake. Afisa ustawi wa Wilaya ya Wete Salma Saleh Hamad, akiwasilisha ripoti ya udhalilishaji wa wanawake na watoto kwa kipindi cha miezi sita, alisema kuchelewa kwa kipimo cha DNA na rushwa muhali bado pia ni changamoto kubwa kwa jamii.  Alisema, malalamiko 64 ya matunzo na mvutano wa malezi yaliripotiwa katika kitengo cha ustawi wa jamii, ikiwemo 39 ya matunzi ya watoto na 25 ni mvutano wa malezi, ambapo malalamiko hayo yalipatiwa ufumbuzi na mawili yanaendelea kusikiliza katika ofisi zao za Wilaya