Skip to main content

Posts

Showing posts from August 13, 2023

ZAFELA YAJA NA JAMBO JEMA KWA WATOTO WA KIKE

  NA FATMA HAMAD, PEMBA MKURUGENZI wa Jumuiya ya Wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA,   Jamila Mahamoud Juma, amezitaka asasi za kiraia, kushirikiana kwa pamoja na kuwajengea uwezo watoto wa kike, waliyokatisha masomo, ili   waweze kurudi na kupata haki yao ya msingi. Mkurugenzi huyo, aliyasema hayo katika mkutano wa kuutambulisha mradi wa Malala, utakaoendeshwa na ZAFELA, Zanzibar kwa muda wa mwaka mmoja, kikao kilichowajumuisha asasi mbali mbali za kirai kisiwani Pemba. Alisema katika utafiti wao walioufanya, waligundu kuwa, kuna wimbi kubwa la watoto wa kike wamekuwa wakikatisha masomo yao, kutokana na sababu mbali mbali, ikiwemo kuolewa, kupata mimba za utotoni pamoja na kufanyishwa kazi za nyumbani. Alisema, wamekuwa wakipokea kesi nyingi za watoto wa kike, kudai haki zao, aidha waliolewa au waliojihusisha na mahusiano, ambao ukiwangalia umri wao unapaswa    wawe wako masomoni. ‘’Tumeamua kuleta mradi huu wa ‘Malala’   kwa ajili ya kumuezesha na kumsaidia mtoto wa kike,

HEDHI SALAMA KWA WANAFUNZI BADO KITENDAWILI, WAPO WANAOAZIMANA VITAMBAA

        NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ HEDHI ni damu maalum, anayotoka mwanamke pekee, mwenye umri maalum na kwa siku maalum. Tena mwenye umri wa kubeba ujauzito, ambapo mabadiliko hayo, hata uwe fukara, fakiri, maskini na tajiri hujitokeza. Naam….damu hii haitoki eneo jingine la mwanamke, bali ni kwenye sehemu yake ya uke tu, tena ni yenye rangi, harufu na uzito kama damu ya kawaida. Tulishazoea kila atokae damu, huwa ni kwa ugonjwa, ajali, kuumia, ingawa kwa ii, ndio uzima na umadhubuti wa mwanamke kiafya. KWA NINI DAMU HII ITOKEA? Kwamba, kiyai kilichokomaa na kutoka nje ya kifuko kisipopata mbegu ya mwanamme ‘ sperm’ baada ya siku moja, kinaharibika haraka haraka. Hapo ngozi nyembamba ya tumbo au mji wa uzazi, iliyotanuka kwa damu, ili kupokea na kulisha mimba, inachanika chanika na kutoa damu. Kumbe mbegu ikikifikia kijiyai, mimba inapatikana na kujishikiza kwenye kuta ‘ wall’  za tumbo la uzazi, ili iendelee kukua. Ingawa, kama mimba ikishika rasmi, hapo huwa vi