Skip to main content

Posts

Showing posts from June 22, 2025

SWAHILI COAST PROJECT: EMPOWERING WOMEN AND YOUTH AS CHAMPIONS OF PEACE IN PEMBA

  BY KHELEF NASSOR@ZANZIBAR Peace is more than the absence of conflict; it is a state of harmony where communities live with respect, understanding, and cooperation. True peace creates an environment where individuals can thrive, families grow strong, and societies progress. However, peace is fragile and must be actively nurtured by all members of society. Women and youth play a critical role in building and sustaining peace. They are not only the majority of many communities but also agents of change, innovation, and resilience. When empowered with knowledge and leadership skills, they become vital contributors to conflict prevention, social cohesion, and community development. Their involvement ensures that peace is inclusive, representative, and sustainable. Recognizing this,   Norwegian Church Aid - NCA recently organized a comprehensive three-day training program focused on leadership and peacebuilding for women and youth in Pemba Island. The training was part ...

MASHEHA CHUMBAGENI, WAMBAA WAAHIDI KUIPIGA TAFU JUMUIYA TAHAFIDHIL-QUR-AN WAMBAA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   MASHEHA wa shehia za Wambaa na Chumbageni, wilaya ya Mkoani Pemba, wameiahahidi jumuiya ya tahafidhil quran, kwamba, watashirikiana nayo, ili kuhakikisha mashindani ya sita ya mwakani yanafanyika kwa ufanisi.   Wakizungumza kwenye kikao maalum cha kamati kuu cha jumuiya hiyo, kilichofanyika Chumbageni, walisema wako tayari kuona mashindani ya mwakani yanafanikiwa.   Walisema, suala la kuwakusanya watoto katika jambo jema kama hilo, hawaa budi kuliunga mkono, kwani ndio eneo la kutafuta kheir kutoka kwa Muumba,   Shehia wa Chumbageni Mgeni Othman Shaame, alisema atazishauri taasis kadhaa na waumini wingine, ili kutoa michango yao ya hali na mali.   Alisema, kutokana na mashindani ya tano kufanikiwa, vyema binafsi ameingia tena hamu, kuona ashirikiane na Jumuiya hiyo, kwa ajili ya mwakani.   ‘’Kwa hakika, mashindani ya tano yalifanikiwa vyema, na kwa kwa mara ya kwanza, mgeni rasmi alikuwa Mkuu w...

MWENGE WAUKUBALI USHIRIKA WA UPANDAJI MIGOMBA KUKUU KANGANI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ KIONGOZI wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ismail Ali Ussi amesema, ameridhishwa kwa asilimia 100, na utekelezwaji wa mradi wa upandaji wa migomba uliotekelezwa na kikundi cha ‘tusitupane Cooparative’ kilichopo shehia ya Kukuu wilaya ya Mkoani Pemba. Alisema, mradi huo ni miongoni mwa jitihada za serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, za kuunga mkono wananchi wake, katika kuhakikisha wanatumia fursa za kiuchumi zinazowazunguka katika maeneo yao. Aliyasema hayo jana, wakati alipotembelea shamba la migomba la kikundi hicho, shehiani humo, ikiwa ni shamra shamra za mwenge huo, kwa mwaka huu. Alieleza kua, mradi huo ni utekelezaji wa ahadi alizoziweka Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi baada ya kuingia madarakani, za kuwawezesha wananchi kuzitumia fursa za kiuchumi zilizopo nchini. Alifafanua kua, kilimo hicho kinaonyesha dhahiri kwamba, vijana wa kikundi hicho wamefanya jitihada nzuri, katika kutimiza azma na maono ya Dk. Mwinyi. "Vijana w...

MWENGE WABISHA HODI CHAKE CHAKE, UKITOKEA MKOANI

    NA MWANDISHI WETU, PEMBA MKUU wa wilaya ya Mkoani Dk. Hamad Omar Bakari, ameuhakikishia, uongozi wa mbio za mwenge kitaifa wa mwaka 2025, kwamba watayafanyia kazi maagizo, maelekezo na ushauri waliutoa, hasa suala la kutunza amani na utulivu, kuelekea uchaguzi mkuu .   Mkuu huyo wa wilaya aliysema hayo jana, eneo la skuli ya Ngwachani wilayani humo, kwenye hafla ya kumkabidhi mwenge huo, mwenzake wa wilaya ya Chake chake Mgeni Khatib Yahya.   Alisema ujumbe wa mwenge kiujumla, umekuja kuwazindua wananchi wa wilaya yake, juu ya umuhimu wa kutunza amani, kwa maslahi mapana ya taifa na watu wake.   Alieleza kuwa, wakati mwenge huo unakimbizwa wilayani mwake na kukutana na wananchi, ulisisitiza utunzaji wa amani, na hasa kuelekea mwezi Oktoba mwaka huu, kwenye uchaguzi mkuu wa vyama vingi.   Dk. Hamad alifahamisha kuwa, jingine ambalo mwenge huo wa uhuru chini ya kiongozi wake Ismail Ali Ussi, ulisisitiza, ni kupiga vita dawa za kulevya ...

WANANCHI PANDANI, MKAGUZI WAO WAJIIMARISHA KUTOKOMEZA UHALIFU

     NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA WANANCHI wa shehia ya Pandani wilaya ya Wete mkoa wa kaskazini Pemba, wamesema wataendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi, ili kudumisha amani na utulivu kwa kupambana na matendo maovu katika shehia yao.   Walieleza hayo katika kikao cha pamoja na mkaguzi wa shehia hiyo cha kujadili na kupanga mikakati ya kuzuiya uhalifu katika shehia hiyo, kilichofanyika shehiani.   Saada Hamid Ali mkazi wa shehia hiyo na Said Juma walieleza kwa niaba ya wanakijiji wenzake walipongeza jitihada za Mkaguzi huyo kwa kuona wanafikia lengo la kuondosha uhalifu.   Walieleza kuwa, kijiji kinapokuwa salama, huwapa nafasi vijana na wananchi wingine, kufanya shughuli zao mbali mbali za maendeleo kwa ufanisi   Akifafanua kikao hicho, Mkaguzi wa shehia hiyo kutoka Jeshi la Polisi mkoa wa kaskani Pemba Khalfan Ali Ussi, alieleza kuwa wanazo mbinu kadhaa za kukabiliana na uhalifu.   Hata hivyo, aliwasisitiza wananch...

KIDUTANI CHUMBAGENI PEMBA WAPITISHA KANUNI ZA KUWALINDA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa kijiji cha Kidutani shehia ya Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wamepitisha kwa pamoja, kanuni zitakazowaongoza wao na watoto wao, katika kufikia malezi na makuzi mema ya vijana wao. Akizisoma kanuni hizo mbele ya mkutano mkuu wa wanakijiji hao, Katibu wa kamati ya maadili, taaluma na ushari Machano Ali Makame, alisema moja ya kanuni hizo kati ya 19, walikubaliana kuwa, mwisho wa kutembea iwe ni saa 4:00 usiku. Alisema kanuni hiyo, itawahusu watu wote, na ikitokezea kuna kundi la watu au mtu mmoja ana dharura mfano ugonjwa, wavuvi, wafanyakazi wataieleza kamati hiyo. ‘’Inawezekana ukamkamata mtu saa 5:00 usiku, lakini kama ukitoa maelezo yenye ushahidi mbele ya kamati, unaweza kusameheka, maana lengo sio kukomoana,’’alisema. Katib huyo alisema kanuni nyingine ambayo wanakikiji hao wamekubaliana ni, kupiga marfuku mikato ya nywele inayopongina na uislamu pamoja na nguo za mbano. Alifafanua kuwa, kanuni nyingine ambayo wan...

RC KUSINI PEMBA: WAANDISHI WA HABARI YAELEZENI MAFANIKIO YALIOPO

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ WADAU wa habari kisiwani Pemba, wametakiwa kutumia taaluma zao  katika kuelimisha jamii kuhusu maendeleo  yalioyopatikana ndani ya awamu ya nane ya Seikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini  ya uongozi wa Dk. Hussein Ali Mwinyi. Hayo yalielezwa jana Juni 21, 2025 na  Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Rashid Hadid Rashid kwenye kongamano   la wadau wa habari, lililofanyika katika ukumbi wa "ZRA" Gombani Chake chake Pemba.  Alisema ipo haja ya wanahabari  kutumia taaluma zao vizuri, ili  kuimarisha upatikanaji wa taarifa sahihi kwa wananchi, hasa zinazohusu maendeleo, kutokana na umuhimu wa taarifa hizo. Alieleza kua serikali ya awamu ya nane chini ya Raisi Dk. Mwinyi imepiga hatua kubwa za maendeleo katika kuwasogezea huduma bora wananchi wake, ya maeneo mbali mbali ya mjini na vijijini. "Serikali ya awamu ya nane, imepiga hatua kubwa katika maendeleo nchini kwa kuwasogezea  huduma mbali mbali, hivyo ni vizuri wa...