Skip to main content

Posts

Showing posts from April 21, 2024

CHAPO: ‘ANZENI MAPEMA KUWAONESHA NJIA ZA KUWA VIONGOZI WATOTO WA KIKE’

    NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@   WAZAZI wanawake wa kijiji cha Jamvini shehia ya Ndagoni, wilaya ya Chake chake Pemba, wametakiwa kutenga muda wa kukaa na watoto wao, ili kuwaonesha njia za wao kuwa viongozi mapema, ikiwa ni pamoja na kuwalea bila ya ubaguzi.   Ushauri huo umetolewa na Masaidizi wa sheria Jimbo la Ziwani, shehia ya Wesha Khadija Said Khalfan, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, kwenye mfululizo wa mikutano ya kutoa elimu, inayoratibiwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’.   Alisema, njia moja wapo ambayo inafaa kuafutwa kwa wazazi hao, ni kuacha ubaguzi wa malezi kama vile kubagua kazi ndani ya familia zao.   Alieleza kuwa, kazi kama za kwenda dukani, kushughulikia mifugo, kubeba kuni zinatakiwa zisitolewa kwa ubaguzi, bali watoto wa kike wafanyishwe, ili kukataa dhana ya ubaguzi.   Msaidizi huyo wa sheria alieleza kuwa, njia nyingine ambayo inaweza kuwatayarisha watoto wa kike kuwa viongozi wa baadae, ni

WANAFUNZI WASHAJIHISHWA KUSOMA MASOMO YA HESABATI KUZALISHA WATAALAMU

  Na Nihifadhi Issa, Zanzibar@@@@ Mkurugenzi mkuu wa chuo cha Indian Institute of Technology Madras (IIT) Prof.Preeti Aghlayam amesema wataendelea kuiunga mkono serikali    kuhakikisha somo la hesabati linapewa kipau mbele maskuli. Akizungumza baada ya kumaliza kwa mtihani wa majaribio uliofanyika katika chuo hicho huko bweleo mkoa wa mjini magharibi alisema kufanya hivyo kutapelekea kuwa na wataalamu wa wazuri ambao watajikita katika teknolojia mbali mbali. Alieleza kuwa lengo ni kufanya majaribio ya mitihani hasa katika somo la hesabati kuona   wanafunzi hao wanakuwa na uwelewa mpana hasa katika masomo ya sayansi ikiwemo hesabati pia ni     kuunga mkono maadhimisho   miaka 60 ya muungano wa tanganyika na zanzibar. Mrajis wa IIT madrasa mshauri Abdallah Khamis amesema kuwepo kwa siku hiyo ya kuwatahini mabingwa wa hesabati kutasaidia wanafunzi kujenga kujiamini na kujitahidi kufanya vizuri katika somo hilo ambalo limekuwa naa kinyan'ganyiro kikubwa cha ajira. Akizungumza

SHERIA MPYA YA ZAECA IWE MKOMBOZI WANAWAKE KUINGIA KWENYE UONGOZI

     Na Nihifadhi Issa Zanzibar@@@@ Katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania imeweka wazi   haki za wanawake za kushiriki katika uongozi, ibara ya 21 inasisitiza kuwa kila raia wa jamhuri ya muungano ana haki sawa za kushiriki katika uongozi wa nchi aidha moja kwa moja au kwa   njia ya uwakilishi.   Kwa   katiba ya zanzibar sehemu   inaeleza kwamba kila mtu apewe nafasi sawa katika kupata nafasi za uongozi kwenye serikali, aidha kwa njia ya moja kwa moja   ama kupitia wawakilishi wao waliochaguliwa kwa njia ya huru na haki. Aidha   mpango wa utekelezaji wa beijing katika maelezo ya dhamira namba 7 imeeleza uezeshaji wa mwanamke na ushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa kuangalia uwiano wa jinsia ili kuhakikisha wanawake na wanaume wanapata nafasi sawa ya kushiriki katika ngazi zote za maamuzi Licha ya hayo yote ambayo yanayompa nafasi mwanamke kushiriki kikamilifu nafasi ya uongozi lakini kuna changamoto mbalimbali zinazomkwamisha kufikia ndoto hizozakuwa kiongozi ikiwemo sual

HIVI NDIVYO TAMWA -ZANZIBAR ILIVYOFANIKIWA KUWAJENGA WAANDISHI VIJANA, MASUALA YA WANAWAKE NA UONGOZI

  Na Nihifadhi Abdulla, UNGUJA. Jitihada mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa siku hadi siku kuhakikisha usawa wa kijinsia unachukua nafasi yake kwa kupitia mikataba ya kimataifa, kikanda, sera, sheria, matamko na mbinu nyengine tofauti Mpango wa utekelezaji wa beijing katika maelezo ya dhamira namba 7 imeeleza  uezeshaji wa mwanamke na ushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa kuangalia uwiano wa jinsia ili kuhakikisha wanawake na wanaume wanapata nafasi sawa ya kushiriki katika ngazi zote za maamuzi Aidha Mkataba wa kikanda wa nchi za kusini mwa afrika kifungu cha 12 kinasisitiza ushiriki sawa wa wanawake kufikia asilimia 50/50 kwenye nyanja za maamuzi, pia kifungu namba 13 kinaeleza kuwekwa mikakati madhubuti ya kuwawezesha wanawake kushiriki katika mchakato mzima wa uchaguzi na upigaji kura na kuondosha mila na desturi potofu zinazopingana na maendeleo ya mwanamke katika siasa na uongozi Chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA Zanzibar ni taasisi inayotetea mambo mengi ya haki ikiw

DIWANI WA KIUYU ADHAMIRIA KUMALIZA KERO NDANI YA WADI YAKE

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA    DIWANI wa Wadi ya Kiuyu Pemba kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Nasra Salum Mohamed amesema, atahakikisha anatatua changamoto zote zinazowakabili wananchi ili kuleta maendeleo katika wadi yake.    A lisema kuwa, ametatua changamoto mbali mbali na anaendelea kushirikiana na wananchi kuziibua changamoto nyengine ili zipatiwe ufumbuzi kwa ajili ya maslahi yao na Taifa kwa ujumla.    Akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika wadi yake alisema, baadhi ya changamoto alizotatua ni pamoja na kuhamasisha kujengwa vyumba vinne vya madarasa katika skuli ya Minungwini na vyumba vinne katika skuli ya maandalizi Kangagani.   Mambo mengine aliyoyatatua Diwani huyo ni kuchimba shimo la vyoo (chamber) katika skuli ya Minungwini, kuezeka vyumba viwili vya skuli ya Mjinikiuyu, kujenga matundu manne ya vyoo katika skuli ya tutu Penjewani na ujenzi wa kituo cha Afya Minungwini.   Diwani huyo alisema pia alitatua changamoto ya umeme katika kijiji cha

FCS: YAVUTIWA NA PACSO UTEKELEZAJI MRADI 'URAIA WETU'

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TAASISI ya The Foundation for Civil Society ya Tanzania bara 'FCS' imesema inaendelea kuridhishwa na utendaji kazi wa Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’, katika utekelezaji wa mradi ‘uraia wetu’ hasa kwa kule kuwanganisha wadau husika. Hayo yameelezwa na mwakilishi wa taasisi hiyo Neil Ngala, wakati akitoa salamu zake, kwenye mkutano wa siku moja, wa kuibua changamoto za kisheria na sera, zinazokwaza wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, uliofanyika Gombani Chake chake. Alisema PACSO, imekuwa ikiendelea vyema na utekelezaji wa mradi huo, jambo ambalo limeanza kutoa taswira ya mafanikio yaliyotarajiwa, ikiwa ni pamoja na kuibua changamoto za kisheria na sera. Alieleza kuwa, mradi huo ambo unatekelezwa na taasisi za PACSO, CYD na JUWAUZA kama hatua ya kitaifa, PACSO imekuwa ikifanya vyema kwa kule kuwakutanisha wadau hisika. ‘’Sisi FCS, tumekuwa tukijivunia mno kila tunapofanyakazi na ‘PACSO’ maana kile ambacho wanakifanya, mat

SHAMRA SHAMRA ZA MIAKA 60 YA MUUNGANO, DK . MWINYI AFUNGUA BARABARA MAENEO HURU MICHEWENI

    NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameziagiza taasisi, serikali ya Mkoa na Wilaya kuhakikisha wawekezaji wanaajiri vijana wa maeneo ambayo watawekeza, ili azma ya Serikali kukiinua kisiwa cha Pemba kiuchumi iweze kufikiwa.   Alisema kuwa, sio jambo zuri kuona mwekezaji anaajiri vijana wa mbali na kuwaacha vijana wa eneo husika, hivyo ni vyema lisimamiwe vizuri hilo, ili kuhakikisha wananchi wananufaika na uwekezaji, hali ambayo itasaidia kukuza kipato cha wananchi na kuimarika kiuchumi.   Akizungumza kwenye uzinduzi wa barabara katika maeneo huru ya uwekezaji Micheweni Aprili 23, 20204, ikiwa ni katika shamra shamra za maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania Dk. Mwinyi alisema, Serikali ya awamu ya nane ya Mapinduzi Zanzibar imedhamiria kukiinua kisiwa cha Pemba kiuchumi, hivyo ipo haja kwa wananchi kunufaika na uwekezaji utakaokuwepo.   Dk. Mwinyi alieleza kuwa, kuna mambo mbali mbali yanayo