Skip to main content

Posts

Showing posts from August 11, 2024

TIMU YA SOKA YA MKOANI QUEENS BADO IPO IPO SANA, MATUNDA KIDUCHU CHANGAMOTO LUKUKI

  NA HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ ‘HAMASA kubwa ilifanyika tokea pale ilipoanzishwa timu ya Mkoani Queens mwaka 2014 na hadi sasa kuweza kusimama’. ‘Pamoja na dharau, kejeli ambazo tumepewa lakini bado tunaendelea mbele kuhakikisha timu yetu inakata mawimbi na kusonga mbele’. Ni kauli ya baadhi ya wachezaji wa timu ya mpira wa miguu wanawake Mkoani qunes, walipokuwa wakizungumza na makala haya kuhusiana na uhai wa timu yao. Timu hiyo iliyoanzishwa mwaka huo wa 2014, ikiwa na wachezaji 26, imepitia madhila makubwa kwa jamii husika ila bado inaonekana kuwepo. Wanasema pamoja na wanajamii kuwachukulia wanawake wanaocheza soka, wanafanya uhuni wao hawakujali hilo, maana nia walikuwa wanaijua wenyewe. Wachezaji hao wanatumia fursa ya vipaji vyao kuhakikisha wanaingiza kipato na kuhudumia familia zao, kujiajiri na kufanya mambo mengine ya kimaendeleo   kutokana na kipato wanachopata kupitia vipaji vyao. Mmoja wa muanzilishi wa timu hiyo ambae sasa ni kocha wa timu hiyo ya Mkoani Qu

ZAINAB SHOMARI: ‘CCM ITAENDELEA KUHUBIRI AMANI, UTULIVU’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAKAMU Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake wa CCM Tanzania ‘UWT’ Zainab Khamis Shomar, amesema CCM, itaendelea kuhubiri amani na utulivu, maana ndio mwalimu wa vyama vingine vya siasa nchini.   Alisema, CCM baada ya kuwahudumia wananchi wote wa Tanzania bila ya ubagauzi, msingi wake mwingine ni kuhubiri umoja, mshikamano, amani na utulivu kwa nia ya kuwaunganisha watu wote.   Makamu huyo Mwenyekiti ameyasema hayo jana, uwanja wa Umoja ni Nguvu wilaya ya Mkoani Pemba, kwenye mkutano wa hadhara uliowajumuisha wana ‘UWT’ wa wilaya za Mkoani na Chake chake, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuimarisha chama kisiwani humo.   Aliwataka viongozi wa UWT, kuanzia ngazi ya shina hadi taifa kuendelea kuhubiri jambo hilo, kwani ndio msingi mkuu wa kwa chama hicho na vyama vingi vingine.   Alieleza kuwa, hata chama kinachopanga kufanya machafuko, kamwe hakiwezi kufanikisha lengo lao, kama nchi hii haina amani na utulivu.   ‘’Sisi UWT na jumuia nyingin

UNYANYAPAA TISHIO JIPYA VIPAJI VYA WATOTO WA KIKE WENYE UALBINO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘MICHEZO kwa wote ‘ or sport for all’’ . Michezo kwa maendeleo endelevu, michezo ni ajira, afya, udugu na kujenga uhusiano wa kudumu. Wapo walioinadi kuwa, michezo ni sehemu ya maisha ya mwanadamu yeyote yule, bila ya kujali rangi, kabila wala jinsia. Kwa mfano sheria 17 za mpira wa miguu, hazijambagua mtu yeyote, chamsingi awe anajimudu kufikia miundombinu husika. Miongoni mwa vifungu vya sheria hiyo, ili kandanda ifanyike moja ni uwepo wa uwanja, pili ni mpira, idadi ya wachezaji, vifaa vya michezo, mwamuzi pamoja na sheria ya 17 ya pigo la kona. Wapo wanawake warefu, wafupi, wanene, wembamba na hata kwa wanaaume, wapo katika maeneo kama hayo, wakishiriki michezo mbali mbali. Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kwenye sura yake ya tatu na hasa kifungu cha 11, kimebainisha usawa wa binaadamu. Hata kile cha 12, kikaendelea kuweka usawa mbele ya sheria, cha 13 haki ya kila mmoja kuwa hai, 14 haki ya uhuru wa mtu binafsi pamoja na kila cha 18 cha