NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KILA ifikapo Juni 5 ya kila mwaka, Zanzibar huungana na nchi nyingine, kuadhimisha siku ya mazingira duniani. Siku hii kwa mujibu wa mitandao ya kijamii, ilianzishwa mwaka wa1972, ambapo ni miaka 54, sasa imeshapita. Iliasisiwa wakati wa mkutano wa Stockholm wa Umoja wa Mataifa, tena kuhusu mazingira ya binadamu nchini Sweden. Inafafanuliwa kuwa, pia mkutano huo, ulipitisha azimio la kuunda United Nations Environment Programme (UNEP), ili kuongeza juhudi za kimataifa za kupamba na uhifadhi wa mazingira. Aidha mtandao wa dcc.go.tz unaripoti kuwa, sherehe rasmi ya kwanza, ilifanyika mwaka wa 1973 chini ya kaulimbiu “Dunia Moja Pekee ”. Tena tarehe hii, imekuwa jukwaa la kimataifa la kuhamasisha jamii, kuchukua hatua za kulinda , kuhifadhi mazingira na kuendeleza uendelevu wa rasilimali za asili. UNEP, inahimiza jamii kuchukua hatua kali dhidi ya wale wachafuzi, wah...