Skip to main content

Posts

Showing posts from 2026

LEO NI SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI, HAYA UNAYAJUA?

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KILA ifikapo Juni 5 ya kila mwaka, Zanzibar huungana na nchi nyingine, kuadhimisha siku ya mazingira duniani.   Siku hii kwa mujibu wa mitandao ya kijamii, ilianzishwa mwaka wa1972, ambapo ni miaka 54, sasa imeshapita.   Iliasisiwa wakati wa mkutano wa Stockholm wa Umoja wa Mataifa, tena kuhusu mazingira ya binadamu nchini Sweden.   Inafafanuliwa kuwa, pia mkutano huo, ulipitisha azimio la kuunda  United Nations Environment Programme (UNEP),  ili kuongeza juhudi za kimataifa za kupamba na uhifadhi wa mazingira.   Aidha mtandao wa dcc.go.tz unaripoti kuwa, sherehe rasmi ya kwanza, ilifanyika mwaka wa 1973 chini ya kaulimbiu “Dunia Moja Pekee ”.   Tena tarehe hii, imekuwa jukwaa la kimataifa la kuhamasisha jamii, kuchukua hatua za kulinda , kuhifadhi mazingira na kuendeleza uendelevu wa rasilimali za asili.   UNEP, inahimiza jamii kuchukua hatua kali dhidi ya wale wachafuzi, wah...

WAUMINI WAMBAA, CHUMBAGENI WAPONGEZA NYAMA YA SADAKA KUWAFIKIA KWA WAKATI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANUFAIKA wa sadaka ya nyama ya Ng’ombe, zaidi ya 189 wa shehia za Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wamepongeza hatua ya jumuiya ya udhu-hiya ya shehia hizo, kwa kukamilisha bila ya kasoro, zoezi la ugawaji wa sadaka hiyo. Walisema, wamefakiniwa kupata nyama hivyo kwa ajili hya kukamilisha mlo wa sikukuu, tena kwa wakati, jambo ambalo walijiona sawa na wingine, wenye uwezo wa kifedha. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, kwa mashatri ya kutochapishwa majini yao, mara baada ya kupokea sadaka hiyo, walisema walipatiwa wastani kilo 1.5, ambayo wingi wao walipata na sikukuu ya pili. Walisema, uwepo wa Jumuiya hiyo, kwa miaka mitatu mfululizo sasa, imekuwa ikiwahakikisha kupata kitoweleo, jambo ambalo kama sio sadaka hiyo, wapo wanaokula dagaa kavu ama samaki siku hiyo. Walisema, hatu hiyo imekuwa ikiwarahisishia maisha walau kwa siku mbili za sikukuu, jambo ambalo hujiona ni sawa na wingine wenye uwezo. ‘’Kwa hakika, juzi nilipokea...

THBUB YAWAPA DARSA YA HAKI ZA BINAADAMU WANAFUNZI 454 WA SEKONDARI 'ZENJ'

  NA MWANDISHI MAALUM, UNGUJA Maofisa kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ofisi ya Zanzibar, wamewapa elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora Wanafunzi 454 wa Skuli za sekondari kwa Mikoa mitatu ya Unguja. Wakizungumza kwa nyakati tofauti kupitia Serikali za wanafunzi wa Skuli 11 za mikoa hiyo, Maofisa hao waligusia zaidi katika mada za kukuza, kulinda, kuheshimu, na kuhifadhi haki za wengine. Pia maofisa hao waliwaeleza wanafunzi kwa upana kuhusu THBUB, kazi na majukumu yake katika kulinda haki za binadamu sambamba na wajibu wa wanafunzi hao katika kuzitekeleza na kuziishi haki hizo. Akiizungumzia haki ya msingi ya mwanadamu, haki ya kuisha Ofisa Sheria THBUB, Fatma Sultan Mwesimba aliwaeleza wanafunzi hao kwa haki hiyo inaaza mara moja baada ya binadamu kuzaliwa nakuongeza kuwa haki hiyo haipokonyeki ina inapaswa mtu kuendelea kuishi nayo na haipaswi kuvunjwa kwa namna yoyote ile isipokua iamuliwe kupitia sharia za nchi. Pia aliongeza kwa ...
 BY HAJI NASSOR Misi Mwalimu Faki is a woman farmer from Gombeume Mchangamdogo village in Pemba who, despite living with a physical disability, is actively engaged in climate adaptation through agroforestry. Her work challenges deep-rooted assumptions about disability, gender, and who can lead climate action at the community level. At 58 years old , Misi Mwalimu Faki is a woman with a physical disability, living with one arm, a mother of nine children , four sons and five daughters , and the wife of a man who has been chronically ill for many years . Her daily life has long been shaped by care, responsibility, and resilience under difficult circumstances. For years, her household faced deep vulnerability. Limited income, growing climate stress, and declining soil productivity made farming increasingly challenging. Feeding a large family was often uncertain, and each season carried new risks. Beyond economic hardship, Misi also experienced social exclusion . In her communit...

KAMATI YA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI CHAKECHAKE YAWAJIA JUU WAZAZI WANAOWARUHUSU WATOTO KUTEMBEZA BIASHARA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KAMATI ya kupambana na udhalilishaji kwa wanawake na watoto ya wilaya ya Chake chake, imepiga marufuku kwa wazazi na walezi wilayani humo, kuwapa biashara za kutembeza watoto wao, kwani ni njia moja wapo ya kufanyiwa vitendo viovu. Kauli hiyo imetolewa leo Mei 25, 2026 na Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Kassim Ali Omar, wakati akifungua kikao kazi, cha wajumbe hao, kilichofanyika ukumbi wa zamani wa TASAF Chake chake. Alisema lazima kamati, isimamie hilo maana wapo wazazi wamekuwa wakiwatumia watoto wao, kutembeza biashara mitaani, na kisha huishia kudhalilishwa. Alieleza kuwa, hasa kuelekea kipindi hichi cha sikukuu na skuli kufungwa, wazazi hutumia fursa hiyo, jambo ambalo sio sahihi. ‘’Niitake sana kamati hii, ihakikishe inasimamia sana, maana wapo wazazi na walezi, wamekuwa wakiwatumia watoto wao, kutembeza biashara majumbani, jambo ambalo ni hatari kwao,’’alifafanua. Katika hatua nyingine, Kaimu Mwenyekiti huyo Kassim Ali Omar, ...

UFUGAJI MATANGO BAHARI AJIRA YENYE GHARAMA NAFUU, 'TUMUOMBE MOLA' MBIONI KUVUNA 20/=MILIONI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘…….SEA Cucumbers’ ama matango bahari…... Na wingine huliita jongoo la pwani, ama kiazi bahari. Ni aina ya wanyama ama kiumbe, kinachoendesha maisha yake baharini. Kitango bahari, kina ngozi ngumu kiasi na mwili mrefu ambapo muonekano na maumbile yake ni sawa na kitango kinacholiwa nchi kavu. Kitango bahari, kinaendelea kufafanuliwa kwenye vitabu na mitandao kuwa, kina mwili mrefu wenye via vya uzazi, moja iliyo na matawi. Wanyama hawa, wanapatikana kwenye sakafu za bahari duniani kote, wakiwa wamegawanyika kwenye spishi zaidi ya 1,717. Ingawa nyingi zao, zinapatikana eneo la Asia-Pasifiki, ambapo kwa Zanzibar utafiti umeonesha zipo zaidi ya aina 35. Vitango bahari, huishi kwa kutambaa kwenye sakafu ya bahari, na kuweka hifadhi na kujisitiri kwenye matumbawe.   Maisha ya viumbve hawa, waliokua hawakuwa na thamani kwa zaidi ya karne moja Zanzibar, maisha yao yana mchango mkubwa katika ikolojia ya bahari, hasa katika kuisafisha. ...