NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@ JUMUIYA ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) imesema inaunga mkono tamko la maridhiano ya chama cha CCM na ACT Wazalendo kwani ni hatua ya msingi katika kuimarisha amani, umoja na maendeleo ya Zanzibar. Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo, Shekh Ali Abdalla Amour, aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Jamatkhan Vuga mjini Unguja. Alisema jumuiya hiyo imepokea kwa faraja na furaha maridhiano yaliyotangazwa hadharani Julai 9, katika viwanja vya Ikulu Zanzibar mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan. Aidha alisema ni vyema kwa viongozi hao kutofanya khiyana katika utekelezaji wa makubaliano hayo ili kuendelea kujenga amani, umoja na mshikamano kwa wananchi wa Z anzibar. Alieleza kuwa jambo hilo limeonesha utayari wa viongozi kuweka mbele maslahi ya Zanzibar na wananchi wake badala ya ...