NA ZUHURA JABIR Katika jamii, mara nyingi mafanikio hupimwa kwa kiwango cha elimu, mali au nafasi aliyonayo mtu. Hata hivyo, kuna watu ambao maisha yao yanatufundisha kwamba mafanikio makubwa huanza pale mtu anapoamua kujiamini, kupambana na changamoto na kutokubali mazingira yamzuie kufikia ndoto zake. Hii ni simulizi ya Fatma Suleiman Mussa, mwanamke mwenye ulemavu anayeishi Jumbi, Zanzibar, ambaye licha ya changamoto alizokutana nazo tangu akiwa mtoto, ameamua kutumia uwezo alionao kujiajiri, kusaidia familia yake na kuwa mfano kwa wanawake wengine wenye ulemavu. Safari yake imejaa changamoto, lakini pia ni ushahidi kwamba “ ulemavu si mwisho wa ndoto. ” SAFARI YA ELIMU NA MAISHA Fatma ni mtoto wa pili katika familia ya watoto wanne, wote wakiwa wa kike. Alianza elimu ya msingi katika Skuli ya Tunguu na baadaye aliendelea hadi kidato cha pili mwaka 2015. Alipata nafasi ya kuendelea na kidato cha tatu katika Skuli ya Kibele, lakini changamoto mbalimbali zil...