Skip to main content

Posts

Showing posts from September 1, 2024

DPP: ‘CHONGA ITAKUWA SALAMA KIUHALIFU WANANCHI MKIAMUA’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ AFISI ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar afisi ya Pemba, imewahakikishia wananchi wa shehia ya Chonga wilaya ya Chake chake, kuwa kama wako tayari kushirikiana na vyombo vya sheria, shehia yao itakuwa salama na vitendo vya kihalifu. Hayo yameelezwa  leo Septemba 6, 2024 na Mwendesha Mashtaka Dhamana wa mkoa wa kusini Pemba, kutoka afisi hiyo, Seif Mohamed Khamis, wakati akijibu hoja za wananchi hao, waliooneshwa kushindwa na vitendo vya kihalifu vinavyofanywa na watoto wao, kwenye mkutano wa kuwajengea uwezo wananchi hao. Alisema, kama kweli wananchi hao wameshakua tayari kuviondoa vitendo vya kihalifu kama wizi, utumiaji wa dawa za kulevya, wajitayarishe kuona mabadiliko muda mfupi ujao. Alieleza kuwa, atahakikisha ofisi yake, kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na kitengo cha dawa za kulevya, wataunda timu ambayo wanawategemea wazazi na walezi, ili kuiweka Kipapo salama. Alisema, hata wao watafurahishwa mno, ikiwa wazazi sasa wako tayari, kuhakik

VIKUNDI VYA KUHIFADHI MAZINGIRA VYAOMBA KUUNGWA MKONO

IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA WANAKIKUNDI cha kuhifadhi mazingira cha ‘Nyange Cooperative’ waliopo shehia ya Mjiniole wilaya ya Chake Chake wameiomba Serikali kuviunga mkono vikundi vyote vinavyojishughulisha na uhifadhi wa mazingira kwa kuwachukulia hatua za kisheria wananchi wanaokata miti ambayo hupandwa na vikundi hivyo kwa lengo la kuzuia maji ya bahari yasipande juu kwenye mashamba yao. Walisema kuwa, wamekuwa wakipoteza nguvu nyingi kupanda miti ya mikoko kwa ajili ya kurudisha uoto asili na kuzuia mabadiliko ya tabianchi, ingawa wamekuwa wakirudi nyuma kutokana na wananchi kuikata huku wakiendelea kuachwa bila ya kuchukuliwa hatua. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi wanakikundi hao walieleza kuwa, hakuna siku hata moja waliyoona watu wanaokata miti hiyo wakichukuliwa hatua za kisheria licha ya kuzifikisha kesi hizo sehemu husika. ‘’Kilichotushanga ni kwamba, siku moja tulikata miti kidogo ili tupate pesa angalau ya kununulia vifaa tunavyotumia lakini wananchi w

WEPO YAUNGANA NA SERIKALI KUPAMBANA NA UKATILI, UDHALILISHAJI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA MSAIDIZI wa Sheria Jimbo la Wete Pemba Khamis Faki Simai amesema, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzubar zimekuwa zikichukua juhudi mbali mbali katika kuhakikisha vitendo vya ukatili na udhalilishaji vinaondoka nchini, ingawa jamii bado haijawa tayari. Alisema kuwa, jamii inapaswa kuthamini juhudi za Serikali hizo katika kupambana na janga la udhalilishaji, kwani wanaoumia ni watoto ambao ndio legemeo lao la baadae na taifa kwa ujumla. Akizungumza wakati wa mafunzo kwa vijana yaliyofanyika katika Ukumbi wa skuli ya Chasasa Wete, Msaidizi huyo wa Sheria alisema kuwa, watu wamekosa hofu ya Mungu na ndio maana hata hawajali kwamba kufanya udhalilishaji ni kosa. ‘’Watu wamekosa imani na ndio maana haya matendo hayamalizi licha ya kupigwa vita na Serikali pamoja na wadau wengine, hivyo tuendelee kupambana ipo siku wanajamii wataelewa kuwa hili ni jambo baya,’’ alisema mkufunzi huyo. Akitoa mada msaidizi wa She

WANAUME WANAOPIGWA NA WANAWAKE CHAKE CHAKE WATAKA DAWATI KUTOA MALALAMIKO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAUME wa shehia za Kibokoni na Vitongoji wialaya ya Chake chake, wamesema wakati umefika sasa, wa kuanzishwa kwa dawati la siri la kundi lao, ili kutoa malalamiko, wanapopewa kichapo na wanawake. Ushauri huo wameutoa Septemba 5, 2024 kwenye kongamano la kujadili njia za kutokomeza ukatili na udhalilishahaji wa kijinsia, lililoandaliwa na Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ na kufanyika skuli ya sekondari ya Vitongoji wilayani humo. Walisema wapo baadhi yao, wanaopokea vipigo kutoka kwa wake zao, ingawa wamekuwa hawajui wapi wakaripoti madhila hayo. Walieleza kuwa, wapo wanawake wamekuwa wakatili kwa waume zao, ingawa wanapokumbumbwa na changamoto hizo, hushindwa wapi wakaripoti. Mmoja kati ya wanaume hao, Salim Ayoub, alisema wanaoa aibu kwenda moja kwa moja kituo cha Polisi kuripoti matukio hayo, hivyo kama wataanzishiwa dawati lao, watejenga uthubutu wa kuziripoti kesi hizo. Alifahamisha kuwa, kama serikali inataka kujua njia sahihi ya

VIWANJA VYA MICHEZO VITUMIKE KUIBUA VIPAJI, WATAALAMU

    IMEANDIKWA NA KHAULAT SULEIMAN, SUZA    WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Le i la Muhamed M ussa ame sema , kupitia viwanja vya michezo vitasaidia kuleta mageuzi katika S erekali na kuibua vipaji kisiwani P emba .   A liya sema hayo katika hafla ya u funguzi wa mradi wa ujenzi wa viwanja vya mpira katika uwanja wa skuli ya  Sekondari Mchangamdogo  wilaya ya W ete Mkoa wa Kaskazini Pemba.   Alisema kuwa, mtaala wa elimu ya michezo utasaidia kwa asilimia kubwa kutoa watalamu na vipaji mbali mbali kutoka skuli na hata mitaani kwa kuwajengea uwezo wa kitaalamu na kufanya mazoezi kwa wingi , ili kuleta mabadiliko katika sekta ya michezo.   "Wizara ya Elimu imejizatiti kusaidia kutumika viwanja hivyo kwa kuleta mabadiliko kwa wanafunzi hususa n masuala ya michezo , kwani michezo ni afya ambayo itawawezesha v ijana hao kujiajiri wenye we , ” alisema Waziri huyo.   Alisema kuwa, sasa ni jukumu la kila mzazi kuhakikisha mnatoa ushirikiano kwa wali