Skip to main content

Posts

Showing posts from July 14, 2024

AFANDI KHALFAN ATIMIZA AHADI KWA WAVUVI

      NA MWANDISHI WETU, PEMBA@@@@ WAVUVI wa bandari ya Tanda Tumbi Shehia ya Mjanaza Wilaya ya Micheweni Pemba, wametakiwa kufuata maelekezo yanayotolewa na mamlaka ya Hali ya Hewa, ili kuweza kujikinga na matatizo yanayoweza kutokea wakati wakiwa katika shughuli zao za uvuvi.   Hayo yalielezwa na Mkaguzi wa Polisi ambae pia ni Polisi shehia ya shehia ya Mjanaza Khalfan Ali Ussi, wakati akikabidhi simu kwa wavuvi hao, ikiwa ni ahadi iliyoitoa kwao hivi karibuni.   Alisema, kwa vile wao ni wavuvu anamatumaini makubwa kuwa,   simu hizo lengo lake ni kuwasaidia katika shughuli zao hizo, pindi wanapopatwa na majanga mbali mbali.   Alifahamisha kuwa, lengo la kutoa simu hizo ni kutokana na maafa mbali mbali, ambayo yanawapata wavuvi wakiwa katika shughuli zao, na kukosa chombo cha mawasiliano.   "Leo (jana), nimekuja kwa ajili ya kutimiza ahadi yangu, niliyoiweka kwenu kuwapatia simu ambayo itaweza kuwasaidia, pindi mnapotokezea kadhia yeyote ile wakati mkiwa katik

BARAZA LA WATOTO WAWI, LAKERWA ADHABU NYEPESI KWA WABAKAJI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ BARAZA la watoto la shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, limesema bado hawaridhishwi na hukumu nyepesi zinatolewa mahakamani, kwa washtakiwa wanaowabaka watoto na wanawake. Walisema, bado hukumu zinazotolewa na mahakma maalum za kupambana na udhalilishaji, zinawafaidisha wabakaji, jambo ambalo, linatishia kuendelea kwa matendo hayo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, walisema, Baraza la Wawakilishi mwaka 2018, lilipitisha sheria kali kwa watakaotiwa hatiani kwa udhalilishaji, ingawa bado mahakimu hawaitumii ipasavyo. Walisema, wamesomeshwa kuwa, mahkama ikimtia hatiani mshitakiwa kwa makosa ya ukatili na udhalilishaji, adhabu yake ni kuanzia kifungo kisichopungua miaka 30 au maisha, ingawa hakuna aliyetekelezewa adhabu hiyo. Mjumbe wa baraza hilo Aisha Mohamed Juma, aliema anashangaa kuona washtakiwa wanafungwa miaka kati ya 10 au 15 tu, jambo ambalo anashindwa kuwaelewa mahakimu. Alieleza kuwa, hajaona wapi mahakimu na ma

WATOTO WA KIKE BADO SANA USHIRIKI KWENYE SOKA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   BADO kuna ushiriki mdogo kwenye michezo kwa watoto wa kike, Kisiwani Pemba na sababu moja inayopelekea watoto wa kike kuwa nyuma katika sekta hiyo na hasa mpira wa miguu.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi Julai, 9, 2024, kwa nyakati tofauti, wadau hao walisema bado wanawake ushiriki wao ni mdogo, katika michezo ya aina mbali mbali, hasa soka   ambapo jitihada zinahitajika kuhakikisha nao wanashiriki.   Muhisin Omar Haji, Wawi Chake chake, alisema watoto wa kike huishia maskulini kushiriki michezo na wanapomaliza hawajiendelezi na wala hakuna mtu wala taasisi ya kuviendeleza vipaji hivyo.   Alisema wapo watoto wa kike wanakuwa wazuri kimichezo, kama mpira wa miguu, kikapu, mpira wa Pete na mengine, lakini cha kuumiza ni kuwa baada ya kumaliza skuli hawajiendelezi.   Asha Said Haji miaka 17, na Mwanaisha Haju Soud miaka 16 wote wakaazi wa Machomane, walisema kutokana na changamoto ya mavazi, kunasababisha kudumaza kwa michezo k