Skip to main content

Posts

Showing posts from April 16, 2023

KATIBU MKUU HABARI, AWAONESHA NJIA YA MAFANIKIO WAKUU WA WIZARA PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KATIBU Mkuu wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar Fatma Hamad Rajab, amewakumbusha wakuu wa vitengo vya wizara hiyo Pemba, kuendelea kufanyakazi kwa pamoja, kwani huo ndio msingi wa mafanikio. Alisema, changamoto ya udogo wa bajeti ya kutosha, uhaba wa watendaji katika vitengo vyao, pamoja na kikwazo cha usafiri, vinaweza kupata ufumbuzi, ikiwa wataendelea kufanyakazi kwa ushirikiano. Katibu Mkuu huyo, aliyasema hayo Gombani Chake chake, wakati akisalimiana na wakuu wa vitendo vya wziara hiyo, alipokuwa kisiwani Pemba, kwa mapunziko ya sikukuu. Alieleza kuwa, umoja na mshikamano ndio suluhisho la changamoto kadhaa zinazowakabili, na kinyume chake, wanaweza kuyumba kiutendaji. Alifahamisha kuwa, kama viongozi wakuu wa wizara hiyo wanashirikiana kwa karibu, ni vyema mwenendo huo wakauiga, kwani unaweza kuwapandisha juu kiutendaji. ‘’Niwalazimishe watendaji wenzangu, kuwa mkitaka kufanikiwa pamoja na changamoto kadhaa, jambo la msi

KAMISHNA POLISI ZANZIBAR AKEMEA WANAOJICHUKULIA SHERIA MIKONONI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KAMISHNA wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad, amesikitishwa na tabia ya watanzania, kuendelea kujichukulia sheria mikononi, jambo ambalo wakati mwengine husababisha vifo kwa watuhumiwa. Alisema, tabia hiyo sio mwenendo mzuri kwa watanzania, kwani serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanania na ile ya Zanzibar, zimeanzisha vyombo maalum, vya kushughulikia jinai na madai. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia simu, alisema zipo mahakama mbali mbali, jeshi la Polisi, ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka na ofisi za wapelelezi, ambazo zimewekwa kazi hiyo. Alieleza kuwa, sheria zinaelekeza wazi wazi mara baada ya jamii kumshutumu mtu kutenda kosa, liwe la jinai ama madai, ni kumlalamikia katika vyombo vya sheria, lakini sio kujichukulia sheria mikononi. Kamishna huyo alisema, anakerwa mno na jamii kuendelea kuwaondoshea uhai watuhumiwa wa makosa mbali mbali, kwani kazi ya kutoa hukumu, imepewa mahakama. ‘’Utamaduni wa kila mtuhumiwa ku

BIASHARA YA BODABODA ENEO JIPYA LA AJIRA VIJANA PEMBA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ “TULIKUWA tunazurura ovyo mitaani, kukaa vijiweni, hali ambayo ingeweza kuhatarisha maisha yetu, kwani tungejiingiza katika makundi hatarishi na hatimae jela, lakini kwa sasa tupo busy kutafuta pesa”, …hayo ni maneno ya baadhi ya vijana waliokabidhiwa mkopo wa bodaboda Wilaya ya Chake Chake Pemba. Vijana hao waliopatiwa mkopo wa bodaboda na Serikali kupitia benki ya CRDB kwa lengo la kuwainua kiuchumi, ambapo kwa sasa wameimarisha maisha yao kupitia ajira hiyo. Ali Issa Ali mwedesha bodaboda anasema, uendeshaji wa huo wa bodaboda umempa mafanikio kwa sababu kabla ya kupata mkopo huo alikuwa na maisha duni kiasi ambacho alikuwa hajui atapata wapi kazi ya kuendesha maisha yake. “Ilikuwa sina kazi hata moja, kazi yangu kubwa ni kuzurura tu mitaani, lakini kwa sasa nashkuru nimejiajiri na napata pesa ya kujikimu kimaisha, Dk. Mwinyi amefanya kitu cha muhimu kwetu vijana, tunampongeza”, anaeleza. Anasema, kipato anachopata kutokana na uendeshaji wa

NDOA KUVUNJIKA, JANGA LA UDHALILISHAJI KWANINI YAWAELEMEE WANAWAKE PEKEE?

  NA HANIFA SALIM, PEMBA@@@@ UTELEKEZWAJI wa familia ni ukatili wa kijinsia, hali hii husababisha chuki, maradhi, udhalilisha na watoto kukosa haki zao za msingi. Jukumu la malezi ni la wazazi wote wawili, kupanga matumizi ya rasilimali za familia na mahitaji ya watoto ni jambo la kupewa kipaumbele. Katika jamii ya sasa, wanawake waliowengi tumeona wakiachwa na waume zao pamoja na watoto, jambo ambalo huleta athari, watoto kukosa haki zao wakati mwengine hata kufanyiwa matendo yasiofaa. Kutokana na kukosa huko huduma, kutoka kwa familia zao ndipo wanapodhalilishwa kwa kushawishiwa, kupatiwa jambo dogo ambalo alilikosa na alistahiki kupatiwa na familia yake. ATHARI ZINAZOIKUMBA FAMILIA ILIYOTELEKEZWA Zipo athari nyingi ambazo huikumba familia ambayo imetelekezwa ikiwemo mama kubeba mzigo mkubwa wa majukumu wa kuwatafutia watoto huduma muhimu kama vile chakula, matibabu, elimu na mengineyo. Watoto kukosa watu wa kuwadhibiti ambapo huweza kutumbukia katika majanga mbali

''MKIENDELEA KUWAFICHA, KUWATENGA WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI MNAZIDI KUWAFUBAZA''

    NA MWANDISHI WETU, PEMBA@@@@ JAMII imetakiwa kuendelea kuwasimamia na kuwapatia huduma stahiki ndugu zao ambao wamejaaliwa kuwa ni walemavu wa akili, kwani kuwatenga na kuwaficha kutazidi kuwafubaza kifkira na kimakuzi.   Wito huo umetolewa na Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Ahmed Abuubakar alipokuwa akizungumza na wazazi na walezi, wenye watoto wenye ulemavu wa akili na wananchi, waliohudhiria katika ftari ya pamoja iliyofanyika Tibirinzi Kiwanja cha Kufurahishia watoto wilaya ya Chake chake.   Alisema licha ya kujaliwa kuwa na ulemavu wa akili lakini, watu wa kundi hilo wanakuwa na mitazamo mizuri pale wanapokuwa hawatengwi na familia, au jamii kwa kuweza kushirikishwa katika mambo tofauti.   Mdhamini huyo alilisisitiza, umuhimu wa kuwatoa watoto na watu wenye ulemavu kujumuika na kupatiwa haki zao mbali mbali ikiwemo elimu, afya pamoja na kuweka mazingira ya kujichanganya na wenzao.   Hata hivyo amesifu mwamko wa wazazi na walezi wa kuwasimam

MBINU ZA KUWAOKOA WATOTO WANAOBAKWA PEMBA HIZI HAPA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ Serikali imetakiwa kuweka mazingira mazuri ili kuwalinda wasichana wadogo dhidi ya vitendo vya ubakaji kisiwani Pemba. Kati ya hayo, ikiwemo kutoa elimu ya kutosha, kuwafanya wasichana wajue haki zao, kuweka ulinzi dhidi ya wanaotaka kutoa taarifa na msaada wa kisaikolojia kwa walioathirika, imeelezwa. Mapendekezo haya yamekuja kufuatia ripoti ya uchunguzi ya gazeti hili, iliyoonyesha kwamba kesi nyingi zinazohusu kubakwa kwa mabinti wenye umri chini ya miaka 18 zinaishia njiani kwa wahusika kutochukuliwa hatua yoyote. Pamoja na hoja hizo zinazosemwa katika jamii, bado mtoto chini ya miaka 18 ni mtoto kutokana na sheria ya Zanzibar nambari 6 ya mwaka 2011 ilivyoeleza Jambo la kwanza ambalo wadau waliozungumza ni hili wamesisitiza ni umuhimu wa Serikali kuendelea kusisitiza kwamba kwa mujibu wa Sheria za nchi, mtoto wa kike maana yake ni mtu mwanamke mwenye umri wa chini ya miaka 18. Mkaazi wa Shehia ya Kiungoni, Ali Haji Omar alimwambia mwandis