Skip to main content

Posts

Showing posts from November 26, 2023

WANAODAIWA KUUA KWA MAKSUDI WAWI, KUUKARIBISHA MWAKA MPYA WAKIWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WATUHUMIWA wa kesi ya kuua kwa makusdi, inayowakabili vijana wanne akiwemo Ali Mussa Omar ‘Mkapa’ na wenzake, wote wakaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake, wamerejeshwa tena rumande, baada ya Jaji anayesikiliza kesi yao kutokuwepo mahkamani. Watuhumiwa wingine waliorejeshwa rumande hadi Januari 23, 2024 ni Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 na Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, ambao wanatuhumiwa kumuua kwa maksudi kijana Said Seif Kombo. Mara baada ya kuwasili mahakamani hapo wakitokea rumande, walitulia tuli wakisubiri taratibu za mahakama kuu ziendelee, ingawa Mwanasheria wa serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Awamu Zubeir Awamu, alidai kuwa Jaji husika hayupo mahakamani hapo. Wakili huyo wa serikali, alimueleza hakimu wa mahkama ya mkoa Chake chake anayeshughulikia makosa ya udhalilishaji Ziredi Abdull-kadir Msanifu, juu ya dharura ya Jaji husika wa kesi hiyo. ‘’Mheshimiwa Hakimu, ilikuwa kesi hii leo

WANAWAKE WAWAONESHA WENZAO NJIA KUINGIA KWENYE SIASA, CHANGAMOTO ZIGEUZENI FURSA SAFARI IENDELEE

    NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@ UONGOZI ni haki ya kila mtu, awe mwanaume au mwanamke. Tena hapa tunajifunza kuwa, hata kundi la watoto wa kike ama wakiume, wanaweza kuwa viongozi kwa aina yao na sehemu waliyo ndani ya jamii yao. Jamii imeshazowea kuona mwanaume ndio anaeweza kuwa kiongozi na kusimamia nchi katika hali zote, kuliko wanawake na hii kutokana na mitazamo yao isijengwa kimamtiki. Ingawa mtazamo huu, unaweza ukaondoka kwasababu mwanamke ameweza kuongoza familia na kuweza   kusimama imara,   kwahivyo hatoshindwa kuisimamia nchi nzima. Mfano hai na wa kweli kwa sasa ndani ya taifa la Tanzania, rais anayewaongoza wananchi wastani wa milioni 60 ni Dk. Samia Suluhu Hassan (mwanamke), na kila mmoja ni shahidi hajatetereka kwenye nafasi hiyo. Tena anasimamia vyema familia yake, pamoja na wananchi wake na kutatua changamoto mbalimbali zinazotokea katika nchi na mengi yameongelewa kuhusu yeye bali hakukata tamaa. KWA NINI WANAWAKE HAWAONEKANA KWENYE SIASA? Asiat

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwani ik

WANAKONGAMANO: ‘’TUITUMIENI TUME YA KUREKEBISHA SHERIA KUTOA MAONI KWA SHERIA MUITAKAYO’

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, wameshauriwa kuitumia Tume ya Kurekebisha sheria wanapokuwa na vikao vyao vya kupokea maoni, ya kutaka kurekebishwa sheria, ili kuwa na sheria zinazoendana na dunia ya sasa. Ushauri huo umetolewa na wanakongamano la siku moja, la kuelekea siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji, lililoandaliwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria, wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’, na kufanyika ukumbi wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba. Walisema, ni vyema wananchi wanapokutana na Tume hiyo, kuacha jazba na kuzitolea maoni sheria, ambazo zimeshapitwa na wakati, ili kueleza wanavyotaka ziwe, kwa mujibu wa mazingira ya sasa. Mjumbe wa Jumuiya ya TUJIPE Pemba, Sheikh Abdalla Nassor Maulid, alisema utoaji wa maoni katika tume hiyo, ni njia muhimu kwa jamii kuwa na sheria rafiki. ‘’Tume ya kurekebisha, hupita katika maeneo yetu, sasa sisi wananchi tuitumieni ili kutoa maoni, juu ya sheria ambayo tuna

ZAWADI AMOUR NASSOR, MWAKILISHI KONDE ALIYEPITIA MENGI KABLA YA KUINASA NAFASI HIYO

  NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@ KILA mwanadamu huwa na malengo katika maisha na huhitajika mipango na ujasiri kuweza kuitekeleza. Ujasiri ni silaha nzito kuibeba, lakini ina faida kama utakuwa na sulubu ya kuibeba. Neno ujasiri limebeba maana kubwa kwenye tafsiri ya mtu aliefanikiwa katika maisha yake. Mmoja wa wanawake aliyeweza kupata mafanikio kutokana na kuwa na ujasiri ni Zawadi Amour Nassor . Mwana mama huyu, ambaye ni mtoto wa kwanza katika watoto tisa wa familia yao,amezaliwa   1978 katika kijiji cha Konde Pemba na kupata elimu yake ya msingi katika Skuli ya Kinyasini, Unguja, mwaka 1991. Aliendelea na elimu ya sekondari katika Skuli ya Konde mwaka 1994 na kupata elimu ya juu katika chuo cha Zanzibar Muslim College, Mazizini hadi ngazi ya stashahada na shahada. Vile vile amesomea uwalimu katika Chuo Kikuu Huria Tanzania ‘OUT’. Alisomesha katika skuli ya msingi za Pangale na Konde"A" kuanzia mwaka 2000 hadi 2020. Jasiri huyu alianza kuwa mwalimu wa s