NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’NA mwaka 2030, najitupa tena jimboni, na napandisha ngazi, nitaomba Ubunge jimbo la Kojani,’’ndivyo alivyoanza Katija Mbarouk Ali . Akiwa pembezoni mwa nyumba yao, eneo la Kiuyu Minungwini, akijivalia kanga za chama cha Mapinduzi, huku akichezea simu yake. Katija, ni mcheshi, mweye sura ya bashasha pamoja na kwamba, anawania kuwa kiongozi, kwa sasa ni mjasiriamali. Akizungumza nami huku, akiangaza macho yake usoni kwangu, na kwa upole, analiambia safari ndio kwanza, inaanza. Kumbe kwa uchaguzi wa 2025, Katija pamoja na ulemavu wake wa viungo, aligombea nafasi ya Uwakilishi jimbo la Kojani, na kisha wajumbe kumkataa. ‘’Si wajumbe mara hii bado wameniona ni mchanga, mwaka 2030, roho zikifika najitupa tena jimboni humo, kwa nafasi ya ubunge,’’anasisitiza. Nilipomuuliza, kama ameyapata machungu kwa uchaguzi wa mwaka 2025, anasema, ameyaona kama mbolea na kumuongezea mwendo. ‘’Hakuna kuka...