Skip to main content

Posts

Showing posts from October 26, 2025

MADC: WANAWAKE PEMBA, WAWAONESHA NJIA WANAWAKE NAMNA YA KUONGOZA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’HESHIMA, bidii ya kazi, upole, ustahamilivu na kufanya uamuzi sahihi, ndio njia moja wapo za kuwatumikia watu,’’anasema Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki. Anasema inawezekana waliowengi, wandhani ili uwe kiongozi mzuri, lazima uchupe mipaka, kimavazi, heshima, uondoe upole, ukiuke sheria, jambo ambalo ni tofauti. Anahadithia wakati wakiwa mtendaji wa Tume ya Uchaguzi, miaka 15 iliyopita, alichunga sana nidhamu na heshima yake, huku akihakikisha halazi kazi. Alizingatia mno kivazi cha heshima, kujenga mapenzi ya kazi kwa kila mmoja, na kuhakikisha kitengo chake hakifeli kwa jukumu, walilopewa. ''Kuna wakai tunasafirisha vifaa tena siku ya mvua, ilipofika majira ya saa 5:50 usiku, wapo walionitaka nirudi nyumbani kumpunzika na wao wataendelea na kazi, niligoma,''anakumbushia. Aliwaambia kama ni wakati wa kazi wanafanya kwa pamoja na wakati wa kumpunzika, wanapumzika kwa pamoja, maana kazi ndio kazi. ‘’Siku hiyo kila mmoj...

MCHAKATO WA KISIASA KWA WATU WENYE ULEMAVU BADO KITENDAWILI

   NA SAMIRA ABDALLA, ZANZIBAR UCHAGUZI mkuu wa mwaka 2025 unafanyika kesho, na suala la ushirikishwaji kamili wa watu wenye ulemavu, linazidi kuwa muhimu.   Zanzibar, kama sehemu nyingine ya dunia, imejitolea kuhakikisha haki za watu wenye ulemavu, zinalindwa na kutekelezwa, ikiwemo haki yao ya kupiga kura na kugombea uongozi. Makala haya yatafanya uchambuzi wa kina kuhusu ushirikishwaji wao, kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025. Licha ya kuwa wengi wetu walikuwa wakifikiria kwamba watu wenye ulemavu, hawana haki na wala hawafai kushiriki katika uchaguzi, jambo ambalo sio sahihi. Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kama sheria mama, inatoa msingi wa ulinzi wa haki za binadamu kwa raia wote kuanzia kifungu ch 11 hadi 25A. Ingawa haitaji moja kwa moja watu wenye ulemavu, inasisitiza usawa mbele ya sheria na kutobaguliwa kwa misingi yoyote. Hata hivyo, sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, inatoa mwelekeo mpana na wa kina zaidi kuhusu haki ...

KURA YA MAPEMA PEMBA YAFANYIKA KWA AMANI

    NA WAANDISHI WETU, PEMBA ZOEZI la upigaji wa kura ya mapema, lililofanyika Zanzibar, kwa upande wa Pemba liliripotiwa kwenda kwa amani na utulivu, katika vituo kadhaa, vilivyopangwa kufanyikwa kwa zeozi hilo, leo. Waandishi wa habari walishuhudia vikosi vya ulinzi na usalama, vikizunguruka katika miji, mitaa na vitongoji mbali mbali, kisiwani humo. Wakati zoezi hilo likiendelea kwa watu maalum, wakiwemo walinzi wa amani na watendaji wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ‘ZEC’, wananchi katika miji ya Chake chake, Mkoani, Wete na Micheweni waliendelea na shuguli zao. Ilibainika kuwa, maandalizi ya zoezi hilo lilofanyika leo Oktoba 28 yalifanyika kuanzia jana Oktoba 27, kwa watendaji, wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa upigaji kura, kufunga vifaa kwa wakati. Akizungumza na waandishi wa habari Mratibu wa ‘ZEC’ Pemba Ali Said Ali, alisema hadi leo majira ya saa 6:55 mchana, hakujaripotiwa tukio lolote, lililozuia au kuashiria kuzuia zoezi hilo. Alisema, watendaji waliote...

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA PANDANI AAHIDI KUBADILISHA PANDANI KUWA YA KISASA.

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA KATIKA miaka ya hivi karibuni, wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika nyanja nyingi za uongozi, kuanzia siasa hadi biashara. Hata hivyo, safari yao haijakosa changamoto,Ingawa dunia imepiga hatua katika masuala ya usawa wa kijinsia, bado wanawake wengi wanakosa nafasi sawa za kushiriki katika maamuzi Dunia ya sasa imekua kiteknolojia hususa ni ushiriki wa wanawake katika kutoa mamuzi na hata kusimamia uwongozi wa nyanja mbali mbali nchi. Tanzanzia ni moja ya nchi ambayo kila ifikapo October   hufanya uchaguzi kila baada ya miaka 5 kuwapa nafasi wananchi ya kuchagua kiongozi wanaye mtaka.   Takwimu za Zanzibar   zinaonyesha kuwa katika uchaguzi wa mwaka 2020, waombaji wanawake walikuwa 135 kati ya jumla ya 601 waliojitokeza kuchukua fomu sawa na asilimia 22.4% na mwaka 2025 zaidi ya asilimia 75 ya wagombea wanawake wamejitokeza kugombania. Hii ni kutokana na elimu iliyotolewa na wadau mbali mbali wakiwemo wa haki za binadam...

DC. MJAJA AWATAKIA WANANCHI WAKE UCHAGUZI WA AMANI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKUU wa wilaya ya Micheweni Pemba, Khatib Juma Mjaja, amewatakia kheir na amani wananchi wa wilaya hiyo, kuelekea zoezi la kidemokrasia, la kuwachagua wagombea wa urais, ubunge, uwakilishi na udiwani. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, alisema zoezi hilo, lipo kwa mujibu wa sheria na kanuni, hivyo kwake yeye, ni kuwatakia kheir wananchi hao. Aliwataka wananchi hao, kuziacha nyumbani jazba, hasira, uchungu na chuki na badala yake, waliendee zoezi hilo, wakiwa na furaha na amani moyoni mwao. Mkuu huyo wa wilaya alieleza kuwa, zoezi la upigaji wa kura sio jambo geni kwa wananchi wa wilaya hiyo, sasa ni vyema wakaliendea kwa upole na shauku, huku ulinzi ukiimarishwa. Alifafanua kuwa, kwa vile Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na ile ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ‘INEC’ imeshateua wasimamizi, zoezi hilo litakuwa jepesi. ‘’Niwaombea sana wananchi wa wilaya ya Micheweni, wale wenye si...

POLISI KUSINI PEMBA, LAWAHAKIKISHIA ULINZI, USALAMA WAPIGA KURA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JESHI la Polisi mkoa wa kusini Pemba, limewataka wananchi wote wenye sifa ya kupiga kura, kujitokeza kwa wingi Oktoba 29, mwaka huu, kutumia haki yao ya kidemokrasia, huku ulinzi ukiimarishwa. Kauli hiyo imetolewa jana na Kamanda wa Polisi mkoani humo, Abdalla Hussein Mussa, ofisini kwake Madungu Chake chake, wakati akizungumza na waandishi wa habari,   juu ya namna jeshi hilo, lililivyojipanda na ulinzi. Alisema, Jeshi hilo lipo kwa mujibu wa kanuni na sheria za nchi, na likiendelea kuwalinda raia na mali zao, hivyo kwa wananachi wasiwe na hofu, kwa siku kupiga kura. Alieleza kuwa, tayari limeshajipanga kila eneo la mkoa huo na mipaka yake, ili kuwapa nafasi wenye sifa za kupiga kura kufanya hivyo, bila ya vitisho vyovyote. Kamanda huyo alieleza kuwa, haiwezekani hata kidogo kujitokeza kwa kundi la wananchi, kutaka kuwazuia wenzao wasitekeleza haki hiyo, ndani ya mkoa huo. ‘’Niwaombe wananchi wote wa mkoa wa kusini Pemba, kwanza ...

UKOSEFU WA RUZUKU KWA BAADHI YA WAGOMBEA ULIVYOSABABISHA KAMPENI YA NYUMBA KWA NYUMBA

    NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@  WAGOMBEA kisiwani Pemba wamesema, changamoto yao kubwa inayowakumba katika kipindi hiki cha kutangaza sera zao ni ukosefu wa ruzuku ambayo inasababisha kutokufanya mikutano ya kampeni ambayo wamepangiwa kuifanya. Walisema, mikutano ya kampeni ndio inayowatangaza kuwa wao ni wagombea, kwani hunadi sera zao ambazo ndizo zinazowafanya wananchi kuwachagua, hivyo kukosa ruzuku imesababisha wafanye kampeni nyumba kwa nyumba, jambo ambalo ni vigumu kuzimaliza nyumba zote kwenye Jimbo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wagombea hao wanasema, ruzuku ni muhimu kwao katika kuendesha mikutano yao ya kampeni ambayo wanajitangaza kwa lengo la kupata nafasi ya kuwa kunadi. Mgombea uwakilishi Jimbo la Wawi kupitia chama cha Wakulima AFP, Farida Juma Khamis alisema, ukosefu ruzuku ni changamoto kubwa iliyomkabili, ambayo inaweza kurudisha nyuma lengo lake. "Kwa vile nilikuwa na nia niliongozana na mgombea urais kila anapokwenda, hivyo ilikuwa nanadi ...