Skip to main content

Posts

Showing posts from 2023

'WANAWAKE WAJASIRIAMALI WAANZISHIWA CHOMBO CHA KUDAI HAKI ZAO'

  NA MCHANGA HAROUB, WMJJWW-PEMBA IMEELEZWA kuwa, uanzishwaji wa jukwaa la wanawake wajasiriamali, kutasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto zinazowakabili akina mama hao, katika shehia mbali mbali Zanzibar .   Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Siti Abass Ali, wakati akizungumza kwa nyakati tofauti, na wajasiriamali wanawake wa wilaya nne za Pemba.   Alisema pamoja na juhudi kubwa inayochukuliwa na Serikali katika kumuendeleza mwanamke, lakini bado imeonekana kuna baadhi ya maeneo yamekuwa ni kikwazo kufikia maendeleo yaliokusudiwa.   Alieleza kuwa, pamoja na hayo, anaamini uanzishwaji wamajukwaa hayo, inaweza kuwa endelevu, ili kuwainua kiuchumi wanawake na hatimae taifa kwa juma.   Mkurugenzi huyo alifahamisha kuwa, uwepo wa majukwaa hayo kutatoa fursa kwa akina mama, kupata chombo madhubuti cha kuzungumza pamoja na kuwa na sauti moja wanapotafuta dawa ya changamoto zao.   Mkurugenzi Siti aliwasisitiza akina mam

OTHMAN AWEKA JIWE LA MSINGI SKULI YA GHOROFA KOJANI, ASEMA HIZO NI RASHA RASHA ZA MAPINDUZI

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Massoud Othman, amesema Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ndio yaliotengeneza mwanga, na kisha kufungua milango ya fursa sawa kwa wote, ikiwemo elimu bila ya ubaguzi. Alisema, Mapinduzi hayo ndio yaliyojenga ngome ya uhakika kwa kila mzanzibari, katika kupata elimu, matibabu na huduma nyingine za kijamii bila ya ubaguzi wowote. Makamu huyo wa Kwanza, aliyasema hayo leo Disemba 30, 2023 Kisiwa cha Kojani wilaya ya Wete Pemba, mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la skuli ya ghorofa ya msingi ya Kojani, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Alisema, ujenzi wa skuli hiyo pamoja na nyingine, ni mkakati endelevu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, wa kuhakikisha inawapatia wananchi wake haki ya elimu, waliyoikosa kabla ya Mapinduzi. Alieleza kuwa, elimu ndio msingi wa uhakika wa maendeleo ya mwanadamu, na ndio maana hata Muumba katika kuwaumba wanaadamu, kuliambatana na tendo la kupe

MACHANO ATOA RAI KUPUNGUZA AJALI ZA BODA BODA

  NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR@@@@   KIONGOZI Mkuu wa Matembezi ya UVCCM ya kuadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar Machano Ali Machano ,amewasihi Maafisa Usafirishaji(bodaboda) wa Mkoa wa Kaskazini Pemba kuwa makini wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ili kupunguza ajali.   Hayo ameyasema wakati akizungumza na kusikiliza changamoto za bodaboda katika Matembezi hayo Pemba.   Machano,alisema umakini ndio nyenzo pekee ya kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi kwa ufanisi.   Alisema kuwa UVCCM ina dhamana kubwa ya kuyasemea makundi mbalimbali ya vijana ili changamoto zao zitafutiwe ufumbuzi na taasisi husika.   Katika mKEEaelezo yake,Mkuu huyo wa Matembezi alisema Serikali ya awamu ya nane chini ya Uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Mwinyi,inaendelea kutoa fursa za mikopo yenye masharti nafuu hivyo kundi hilo wafuate utaratibu na UVCCM itawasemea kuhakikisha wananufaika na mikopo hiyo.   “Matembezi ya kuadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi ni jukw

MAKAMU WA KWANZA AIZINDUA BARABARA KIPAPO-MGELEMA, AWAKUMBUSHA JAMBO WANANCHI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Massoud Othman, amesema maono ya muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar, mzee Abeid Amani Karume, yanaendelea kutekelezwa kwa vitendo, ndani ya awamu ya nane, inyoongozwa na Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi. Makamu huyo wa Kwanza, aliyasema hayo leo Disemba 29, 2023 shehia ya Mgelema wilaya ya Chake chake Pemba, mara baada ya uzinduzi wa barabara ya Kipapo- Mgelema, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Alisema, ujenzi wa barabara za kisasa, skuli, miundombinu ya maji safi na salama na matayarisho ya ujenzi wa viwanja vya ndege na utanuzi wa bandari, yanayotekelezwa sasa, ndio azma na maono ya wasisi wa Mapinduzi. Aleleza kuwa, kila mmoja anayosababu ya kufurahia na kushangilia yanayofanywa sasa, na yale yaliokuwepo kabla, kwani yanalenga moja moja kutatua changamoto za wananchi. Alifafanua kuwa, ujenzi wa bara bara ya Kipapo– Mgelema na nyingine, ni mifano mizuri ya jitihada za ser

MWAKILISHI CHAMBANI, APIGIA CHAPUO KILIMO MATANGO BAHARI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MWAKILISHI wa Jimbo la Chambani wilaya ya Mkoani Pemba, Bahati Khamis Kombo, amewasisitiza vijana kuchangamkia kilimo cha matango bahari, kwani bei yake iko juu kuliko kilimo cha karafuu. Alisema, kama Katibu mkuu wa wizara ya Uvuvi na Uchumi wa Buluu, alivyosema kuhusu soko na bei, ni fursa kwa vijana wa jimbo la Chambani kuekeza kwenye kilimo hicho. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mara baada ya kuwekwa kwa jiwe la msingI la kituo cha kutotoleshea vifaranga vya matango bahari eneo la Dodo Pujini hivi karibuni, alisema sasa vijana washindwe wao. Alisema, kama kilo matangao (majongoo) bahari ni shilingi 100,000 ni wakati vijana kwenda kujikomboa kupitia sekta ya bahari. Alieleza kuwa, awali upatikanaji vifaranga ilikuwa ni changamoto kwa wakulima hao kuagizisia kisiwani Unguja, ingawa kwa sasa kituo cha uzalishaji kipo kisiwani Pemba. ‘’Changamoto kubwa ya kilimo cha matango bahari ilikuwa ni upatikanaji wa vifaranga, lakini sasa kituo c

SPIKA ZUBEIR AWEKA JIWE LA MSINGI SKULI YA GHOROFA MWAMBE KISHA AACHA UJUMBE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Zubeir Ali Maulid, amewataka wananchi wa Mwambe wilaya ya Mkoani, kuyaenzi na kuyalinda mapinduzi ya Zanzibar, kwani ndio mkombozi wa upatikanaji wa huduma mbali mbali, ikiwemo elimu. Spika Zubeir, aliyasema hayo leo Disemba 28, 2023 Mwambe wilaya ya Mkoani, mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la skuli ya ghorofa mbili iliyopo Chanjaani, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Alisema kabla ya Mapinduzi hayo, watawala walitoa huduma hizo kwa matabaka na kuwafanya watoto wa wanyonge, kukosa huduma mbali mbali ikiwemo elimu na matibabu. Alieleza kuwa, madhila hayo na mingine ndio yaliyowafanya waasisi wa Mapinduzi hayo, kuamua kufanya kila juhudi ili kuhakikisha wanauondoa utawala uliokuwepo, ili kuwarejeshea heshima wazalendo. ‘’Leo tukiwa ndani ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar wananchi wa Mwambe na maeneo mingine, tunayokila sababu ya kuyalinda, kuyaenzi mapinduzi hayo, maana nd

KATIBU MKUU ABEDA ATOA DARSA KWA WAZAZI ULINZI WA WATOTO

  Na Muandishi Wetu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto bi Abeida Rashid Abdallah amewataka Wazazi na Walezi Wanawake kuwachunguza watoto wao sehemu za siri katika miili yao ili kuhakikishwa kwamba mtoto hao wako salama na hawajafanyiwa vitendo vya udhalilishaji vya aina ya ngono. Kauli hiyo ameitowa katika mafunzo ya kuwajengea uweza kikundi cha Banaty yaliyofanyika Michenzani Mall Unguja mara baada ya mtaalam wa Afya Dkt Ummulkulthum Omar kuwasilishaji mada ya afya ya mfumo wa uzazi pamoja na kueleza kwamba katika utekelezaji wa majukumu yake anakutana na kesi za watoto wachanga   wa miezi minane wameingiliwa kinyume na maumbile na kuharibiwa. Bi Abeida amesema kwa vile Wazazi na Walezi Wanawake hawana vibakio ni vyema kuwa karibu na watoto hasa watoto wa kiume waliyofikia umri wa balegh kwa kuwauliza masuali bila ya kuona haya pamoja na kuwaangalia sehemu zao za siri kama ziko salama na hazijafanyiwa udhalilishaji wa aina ya ngono. “Tuwe karibu

NAIBU SPIKA ZANZIBAR KUFUNGUA MIRADI MIWILI ASUBUHI HII PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHAMRA shamra za kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, yaliofanyika mwaka 1964, zinatarajiwa kuendelea tena asubuhi hii, katika wilaya za Chake chake na Wete, kwa ufunguzi wa miradi miwili. Shamra shamra hizo, zitaanzia kwa wilaya ya Chake chake, ambapo Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mgeni Hassan Juma, anatarajiwa kufungua soko la samaki na mboga eneo la Machomane wilayani humo. Shughuli hiyo inatarajiwa kuanza majira ya saa 2:00 asubuhi, kwa kuwasili wananchi na wageni wingine mashuhuri, kabla ya Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za ‘SMZ’ Issa Mahafudhi, kumpokea mgeni rasmi. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwa vyombo vya habari, na Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, alisema tayari kila kitu kilichopangwa kwa ajili ya hafla hiyo, kimekaa sawa. Alisema, tayari mgeni rasmi wa ufunguzi wa soko hilo, alishapatikana mapema, na kilichobakia ni kwa wananchi na wafa

WATU WENYE ULEMAVU WATAKA NAFASI MAJIMBONI SIO VITI MAALUM PEKEE

  NA ASIA MWALIM, ZANZIBAR @@@@   NCHI nyingi hupanga mipango yake ya Kimaendeleo na kiuchumi kwa kuzingatia mambo mengi.Hii ni pamja na idadi ya watu wake na zaidi mahitaji yao, ikiwa pamoja na kuzingatia maumbile.   Katika hayo mazingatio limo kundi la watu wenye mahitaji maalum katika maisha yao ya kila siku na miongoni mwao ni wale wenye ulemavu.   Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonesha takriban asilimia 15 ya watu duniani ambao ni zaidi ya bilioni moja ni wenye ulemavu, wengi wakiwa wanawake.   Kati ya hawa zaidi ya watu milioni 80 katika Bara la Afrika ni wenye aina moja au nyengine ya ulemavu.   Hata hivyo, kundi hili bado halijapewa umuhimu unaostahiki katika baadhi ya maeneo, hali inayowanyima haki zao za kikatiba na kidemokrasia.   Miongoni mwa malalamiko yanayosikika hapa kwetu ni ya vyama vya siasa kushindwa kuwasimamisha watu wenye ulemavu majimboni na badala yake kutegemea nafasi za viti maalumu pekee.   Wapo wanaouliza kama Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama.