NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WIZARA ya Katiba na Sheria ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imewataka wananchi wa Kisiwa cha Kokota shehia ya Mtambwe kusini wilaya ya Wete, kuendelea kuzitumia mamlaka za serikali, ili kupata ufumbuzi wa matatizo yao ya kisheria. Kauli hiyo imetolewa Juni 6, 2025 na Afisa Habari wa wizara hiyo, Pilly Nashon wakati akizungumza na wananchi hao, kwenye mkutano wa wazi, wa ufungaji wa kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria wa Mama Samia. Alisema, kwa wananchi hakuna namna ya kuzitumia mamlaka ya serikali kwa kutafuta haki zao, maana vyenginevyo wanaweza kupewa nyaraka, mfano wa vyeti vya kuzaliwa visivyohalali. Alieleza kuwa, nyaraka hizo pamoja na vyeti vya ndoa, hati za ardhi, vitambulisvyo ya taifa na vile vya ukaazi vya Zanzibar, vitaendelea kutolewa na mamlaka za serikali na wananchi wanapovihitaji waelekee huko. ‘’Jiepusheni na kuwatumia watu kwa umaarufu wao, mnapohitaji nyaraka mbali mbali, kama vile vitambulisho vya taifa na vyeti vy...