Skip to main content

Posts

Showing posts from December 25, 2022

FEDHA ZA UVICO19 ZAPUNGUZA MSONGAMANO WA WANAFUNZI MADARASANI PEMBA

  NA BAKAR MUSSA, PEMBA:: MARCH   2020 Tanzania, iligundua kesi ya mwanzo ya ugonjwa Corona baada ya dunia kugubikwa na janga kubwa la uwepo wa gonjwa huo, 'UVICO19' ambalo ulianza mwezi disemba 2019 nchini China. Licha ya Zanzibar kupoteza roho za watu wake kadhaa, lakini pia kwa kiasi fulani, iliathirika kiuchumi, ijapo kwa asilimia ndogo kutokana na watalii kutoingia kwa kasi kama ilivyozoeleka. Ikumbuke kuwa, ugonjwa huo unaelezwa unasambaa kwa kasi kutokana na kuwepo kwa makaazi ya watu karibu (msongomano) na hivyo kuwepo na hadhari ya kutokukaa karibu na kuvaa Mask (Barkoa).   Kwa vile ugonjwa huo ulitawala dunia nzima, ni wazi kulitokea mtikisiko wa uchumi, ingawa waswahili husema ‘Mwenyeezi Mungu akikupa kilema hukupa na mwendo’. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ilipata mkopo wa fedha kutoka Umoja wa Mataifa, baada ya kuonekana nchi nyingi kukumbwa na ukosefu mkubwa rasilimali fedha za kujiletea maendeleo kutokana na kuwepo ugonjwa huo. Zanzibar ikiwa

MWANAMKE WA KIJIJINI NI ROBOTI LISILOTUMIA UMEME?, WANAUME WAPUUZA MAJUKUMU YAO

  NA BAKAR MUSSA, PEMBA Kama ilivyo kawaida kwa samaki, hawezi kuishi bila ya kupata maji, ili  yaweze kumsaidia kuishia na ndio mwanamke anavyohitaji kupata mwanamme ili kuanzisha na kuendeleza familia. Kwa mujibu wa taarifa ya kidunia,watu bilioni 1.7 wanaishi vijijini  duniani kote, huku zaidi ya asilimia 40 ya nguvu kazi katika kilimo ni wanawake. Ambao wanatajwa na kuiwakilisha na kuindeleza jamii lakini wanabakia kuwa ndio masikini wakubwa. Hiyi ni kauli ya Bi Cornelia Richter,Rais wa mfuko wa Kimataifa wa maendeleo ya Kilimo ‘IFAD’ wakati akizungumza na ‘UN news’ miongoni mwa mikutano ya hali ya wanawake duniani. “Endapo umasikini ungekuwa  na sura basi ingekuwa ya mwanamke wa kijijini, sisi hapa ‘IFAD’ tunajaribu kuwekeza katika uwezo wa wanawake na sio kuwadhalilisha wanawake”, alisema Bi Cornelia. Katika mkutano huo, alisisitiza kuwa kuboresha maisha yao ni muhimu ili kutokomeza umasikini, jambo ambalo litahitaji mtazamo tofauti na hatua mbalimbali kulifanikisha. Mwanamke kam

CHANGAMOTO HEDHI SALAMA KWA WANAFUNZI PEMBA ZAELEKEA KUWA HISTORIA

NA BAKAR MUSSA, PEMBA::: HEDHI ni hali ya mabadiliko katika mwili wa mwanawake ambayo hutayarisha nyumba ya uke kupata ujauzito.   Kila mwezi mji wa uzazi hupata kokwa ambapo mwanamke akipata ujauzito, mtoto ataweza kukuwa. Ingawaje mwanamke asipo pata ujauzito, kokwa haihitajiki damu itatokea ukeni na hiyo huitwa damu ya hedhi. Wanawake wengi walio komaa, hupata hedhi, na wasichana hupata hedhi zao kati ya miaka tisa (9) na miaka 16, lakini huacha kupata hedhi wanapotimia miaka 50. Mwanamke, akiwa na hedhi anapaswa kutumia visodo au pedi kuzuia damu, ambazo  zimeundwa na vifaa vya laini zinazo nyonya damu hiyo. Kutokana na umuhimu wa jambo hilo Umoja wa Mataifa imetenga kila tarehe 28 mwezi Mei, dunia huadhimisha siku ya hedhi safi na salama. Usafi ni jambo muhimu katika maisha ya mwanadamu, awe mke au mume lakini mwanamke inasisitizwa sana, kwa vile akifikia balegh huingia katika mazingira fulani ambayo humlazimu kila wakati kuhakikisha yuko msafi. Wizara ya Elimu n

KHADIJA: MJASIRIAMALI ANAYEUSARIFU UKINDU, AKIZALISHA MAKAWA, VIPEPEO VYA ASILI

    NA ZUHURA JUMA, PEMBA:::: NI majira ya saa 6:00 za mchana nikiwa katika harakati zangu za kazi, nilijikuta naibukia katika kijiji cha Tumbe Mashariki Wilaya ya Micheweni Pemba. Muda huo kijua kilikuwa kinawaka mithili ya moto uliomwagiwa maji kutokana na vuke lililokuwepo. Wakati macho yangu yakiangaza huku na kule, punde nilimkuta mama mmoja wa makamo, akiwa amekaa pembeni ya mlango wake wa mbele akishona makawa. Kumbe alikuwa ni mama wa miaka 46 aliejulikana kwa jina la Khadija Sleyum Mtawa anaejishugulisha na ushonaji wa makawa ya nyiti tangu akiwa mtoto. Bila kujali alinielezea ushonaji wa makawa ya nyiti kwamba ni kazi anayoipenda ambayo inampatia angalau pesa ya sabuni. Uso wake ukionesha tabasamu anasimulia ni kazi aliyoianza tangu akiwa na miaka 11, wakati huo akiwa darasa la tano mwaka 1985. Makawa hayo anatengeneza kwa kutumia ukindu mzima uliopasuliwa, rangi na kamba inayojulikana kwa jina la unu ambayo hupatikana kwenye kuti la mnazi. Kilichomsukuma

PPC YAFANYA MKUTANO MKUU MAALUM, MAAZIMIO 10 YA UTPC YARIDHIWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: MWENYEKITI mstaafu wa Klabu ya waandishi wa habari Pemba ‘PPC’ Said Mohamed Ali, amewakumbusha wanachama kulipa ada zao kwa wakati, kwani ndio uimara na uhakika wa kuwepo kwa PPC.   Mwenyekiti huyo aliyasema hayo Disemba 24, 2022 kwenye mkuatano mkuu maalum wa PPC, uliofanyika ukumbi wa Maktaba Chake chake Pemba.   Alisema uhai wa ‘PPC’ unategemea mno uhai wa wanachama wanaolipa ada, kwani sio vyema klabu hiyo kuendeshwa kwa michango na miradi ya wafadhili pekee.   ‘’Wafadhili kama Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania ‘UTPC’, Interenews na hata Baraza la Habari Tanzania ‘MCT’ wanaweza kuja na kuondoka, lakini sisi wanachama ndio wenyewe,’’alishauri.   Katika eneo jingine, Mwenyekiti huyo mstafu aliwakumbusha waandishi hao kufanyakazi kwa kufuata maadili na sheria zao, ili wasiwe chanzo cha uvunjifu wa amani.   Mapema Mwenyekiti wa sasa wa ‘PPC’ Bakar Mussa Juma, akielezea mwelekeo wa ‘UTPC’ pamoja na yatokanayo na mkutano uli

WAZIRI RAHMA AWASHUTUKIZIA MADALALI CHANZO MIGOGORO YA ARDHI ZANZIBAR

    Na Sabiha Keis ,Zanzibar WAZIRI wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Rahma Kassim Ali amesema asilimia 80% ya migogoro ya ardhi katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar yanasababishwa na baadhi ya madalali kwenda kinyume na taratibu za kisheria zilizowekwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ). Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliyofanyika katika ukumbi wa Wizara hiyo Maisara   jana, Alisema asilimia kubwa ya migogoro ya ardhi inachangiwa na madalali kwa kuuza viwanja bila kufuata taratibu za kisheria zilizowekwa katika uuzaji na ununuzi hali ambayo inasababisha migogoro ya ardhi kuendele kujitokeza nchini. Alisema kutokana hali hiyo wizara yake inajipanga kuandaa utaratibu maalum wa kuweza kudhibiti tatizo hilo ambalo linarudisha nyuma jitihada za kuleta maendeleo. Lakini kuanzia sasa mtu akijulikana anauza kiwanja kinyume na utaratibu sheria itachuka mkondo wake. "Napenda kuwasihi wananchi wanapotaka kununua ardhi katika maeneo mbali mbali ya Unguja na