NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ KISIWANI Pemba, kuna kijiji kimoja chenye historia ya pekee, kijuilikanacho kwa jina la Jambangome. Kijiji hicho kipo katika maeneo ya karibu na Wambaa, wilaya ya Mkoani, mkoa wa kusini Pemba. Kipo umbali wa kilometa 31 kutoka mji mkuu wa Pemba wa kisasa Chake chake, ambapo ni umbali wa dakika 49 hadi saa moja, kwa usafiri wa gari ambayo si ya abiria. Jambangome ina historia kubwa na yakuvutia inapoelezwa kwa vizazi vya sasa na wageni wanaoingia na kutaka kuujuwa kiundani mji huo. Kwani inaaminika mji huo, ndio wa kwanza kuhamiwa na kukaliwa na watu katika kisiwa hicho cha Pemba. Historia inatueleza kuwa, Jambangome ilikaliwa na wahindi wa jamii ya Mabohora, ambao asili yao ni “Wagujurati” kutoka India. Walihamia, baada ya kushauriwa na mababu zao kutafuta fursa mpya za kibiashara, katika ukanda wa Afrika mashariki, baada ya kupatwa na njaa kali huko katika jamii zao. Neno hili “Bohora” linatokana na neno la kigujurati le...