Skip to main content

Posts

Showing posts from February 8, 2026

KUTOKA SKULI YA MWANZO JAMBANGOME HADI MSITU, ILIHAMISHIWA UWELENI MIAKA 300 ILIYOPITA

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ KISIWANI Pemba, kuna kijiji kimoja chenye historia ya pekee, kijuilikanacho kwa jina la Jambangome. Kijiji hicho kipo katika maeneo ya karibu na Wambaa, wilaya ya Mkoani, mkoa wa kusini Pemba. Kipo umbali wa kilometa 31 kutoka mji mkuu wa Pemba wa kisasa Chake chake, ambapo ni umbali wa dakika 49   hadi saa moja, kwa usafiri wa gari   ambayo si ya abiria. Jambangome ina historia kubwa na yakuvutia inapoelezwa kwa vizazi vya sasa na wageni wanaoingia na kutaka kuujuwa kiundani mji huo. Kwani inaaminika mji huo, ndio wa kwanza kuhamiwa na kukaliwa na watu katika kisiwa hicho cha Pemba. Historia inatueleza kuwa, Jambangome ilikaliwa na wahindi wa jamii ya Mabohora, ambao asili yao ni “Wagujurati” kutoka India. Walihamia, baada ya kushauriwa na mababu zao kutafuta fursa mpya za kibiashara, katika ukanda wa Afrika mashariki, baada ya kupatwa na njaa kali huko katika jamii zao. Neno hili “Bohora” linatokana na neno la kigujurati le...

MAKABURI YA MAZRUI NA HADITHI INAYOTIA HURUMA PEMBA, MABAKI YAISHI KWA MIAKA 300 SASA

     NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MAKABURI ya Mazrui, ni sehemu ya kihistoria inayopatikana   Chwaka, shehia ya Tumbe mashariki wilaya ya Micheweni Kaskazini Pemba. Ni sehemu moja wapo ya kivutio cha kihistoria, hutembelewa na wageni wa ndani na nje ya nchi, ili kulinda urithi na utamaduni unaopatikana humo. Makaburi ya mazrui ni eneo la tatu la sehemu ya kihistoria, katika eneo hilo na lenye mabaki   ya utawala wa Mazrui waliohamia katika karne ya 18. Ni miongoni mwa mabaki yaliyopo hapo ni hayo makaburi yaliyokuwepo sehemu hiyo. Tukisema makaburi ni sehemu maalum ,iliyotengwa kwa ajili ya kuzikwa kiumbe kilichokufa na kuhifadhiwa, kwa safari yake ya milele. MAZRUI KUHAMA KWAO KUINGIA PEMBA Mohamed Yussuf Khamis, ni Afisa Mambo ya Kale anasema   Wamazrui kwa jina jengine wanaitwa (Waarabu), wa kabila la kimazrui, wanatokana na asili ya taifa la Oman. Anasema, walihama kwao na kuja katika upwa wa Afrika Mashariki kwa lengo la kufanya biashara na...