Skip to main content

Posts

Showing posts from June 29, 2025

'TUZ': TUNAWASHIRIKISHA WADAU ILI KUFIKIA MALENGO'

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ MKURUGENZI Rasilimali watu utawala na mipango wa Tume ya Utangazaji Zanzibar ‘TUZ’ Zainab Sheha Khamis amesema, kushirikishwa kwa wadau mbali mbali katika kuchangia kanuni ya maudhui na udhibiti wa vituo vya utangazaji, kutasaidia kufikia malengo yaliyokusudiwa na  tume hiyo.   Aliyasema katika mkutano wa mafisa wa Jeshi la Polisi wa kitengo cha kupambana na uhalifu wa mtandaoni, kuhusu udhibiti wa maudhui kwa vituo vya utangazaji, kuelekea uchaguzi mkuu 2025 uliyofanyika ukumbi wa mikutano ZBC Mkoroshoni Chake Chake Pemba.   Alieleza kuwa, kwa kushirikiana na wadau hao kutasaidia kufikia malengo husika, ya kupambana na uhalifu wa kimitandao, kuhusu maudhui kwa vituo vya utangazaji, ili kuepusha migogoro inayoweza kutokezea.   "Tumeona wadau hawa ni muhimu, katika kushirikiana nao kwani wao ni sehemu moja wapo ya kuhakikisha wanadhibiti maudhui yaliyokua siyo na kupambana na uhalifu katika mitandao,"alifafanua. ...

'WEPO' 'JAMII IKIAMUA, LEO UDHALILISHAJI KWISHA KAZI WETE'

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ MRATIB wa mradi wa uwezeshaji na upatikanaji wa haki, Rashid Mshamata, kutoka Jumiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete ‘WEPO’ amesema bado jamii, ina muamko mdogo katika vita vya ukatili na udhalilishaji.   Alieleza hayo kwa wanafunzi na walimu wa skuli na madarsa, za Wete ukumbi wa skuli ya Chasasa, ikiwa ni muendelezo wa kampeni ya kupiga udhalilishaji katika jamii.   Alisema jamii bado ina mila na desturi kandamizi ambazo zinawafanya wasichana na wanawake waishi kwa hofu, na kukosa usawa na haki zao stahiki, jambo linalowapa mwenye wa kufanya maovu.   ‘’Kupitia kampeni hii, tunawaleta vijana kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia, ambapo tunawafundisha sio tu kujitambua, bali kushiriki katika kulinda haki za wenzao na kuripoti vitendo,"alieleza.   Mshamata alifafanua kuwa, mafanikio ya kampeni hizo skuli na madrassa, inadhihirisha kwamba vijana wakiwa na maarifa sahihi, wanaw...

WATUMISHI WATAKIWA KUTUNZA HESHIMA YA TAASISI ZAO

  NA MWANDISHI MAALUM. Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Eliakim Maswi, amewataka watumishi wa umma kuhakikisha wanatunza, kulinda na kukuza heshima ya taasisi wanazozifanyia kazi pamoja na Serikali kwa ujumla. Bw. Maswi ameyasema hayo alipofunga mafunzo elekezi kwa watumishi wapya na wale waliohamia Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, yaliyofanyika ukumbi wa Ali Hasan Mwinyi uliopo Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha mkoani Pwani Julai 3, 2025. Aidha, amewataka watumishi hao kuzingatia nidhamu kazini, ushirikiano na kufanya kazi kwa uaminifu ili kusaidia wananchi kupata huduma iliyobora. “ Nategemea mtakuwa na nidhamu ya kipekee kwani Serikali inawataka mutimize majukumu yenu kwa wakati na kwa nidhamu thabiti mkishirikiana kutekeleza maagizo” Alisema Katibu Mkuu Maswi. Bw. Maswi pia alisisitiza umuhimu wa watumishi kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma. Vi...

'THBUB' YAELEZEA NAFASI YAKE UCHAGUZI MKUU 2025

NA MWANDISHI MAALUM, @@@@ KAMISHANA  wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) Zanzibar, Mhe. Khatib Mwinyichande, amesema Tume hiyo, ina nafasi ya kikatiba katika kuhakikisha uchaguzi mkuu nchini unakuwa huru haki na kuzingatia misingi ya utawala bora. Mwinyichande ameyasema hayo alipozungumza na waandishi wa habari katika Maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), kwenye banda la Tume hiyo. Alibainisha kuwa jukumu kubwa la Tume hiyo ni kulinda na kuhifadhi haki za binadamu na misingi ya utawala bora, suala alilolieleza kuwa na nafasi ya moja kwa moja kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu. "Uchaguzi si tukio la kisiasa pekee, bali ni jambo linalogusa haki na msingi ya wananchi, kwa kuwa nchi yetu ya kidemokrasia hupatikana kupitia uchaguzi huru na wa haki". Alieleza Kamishna Mwinyichande.   Alisema jukumu kuu la kuu la THBUB ni kuhakikisha misingi ya kisheria na haki za binadamu zinalindwa katika kila hatua ya uchaguzi," Mhe. Mwinyichande...

WATIA NIA UBUNGE, UWAKILISHI CCM PEMBA WANAWAKE 71 KATI YA 270

  NA WAANDISHI WETU, PEMBA@@@@ WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi CCM, 270 wakiwemo wanawake 71 na wanaume 199, wamejitokeza kuomba nafasi za Ubunge na Uwakilishi katika majimbo 18 kisiwani Pemba.   Kati hao 270, walioomba nafasi ya Ubunge wote walikuwa ni 147, kati ya hao wanawake ni 40 na wanaume 107, huku kwa nafasi ya Uwakilishi wote waliomba ni 123, wakiwemo wanawake 31 na wanaume 92.   Waandishi wa shirika la Magazeti ya serikali ambao walifika ofisi za CCM za wilaya za Micheweni, Wete, Mkoani na Chake chake, walibaini kuwa, wilaya ambayo wanawake walijitokeza kwa wingi ni wilaya za Micheweni na Mkoani ziliokuwa na watia nia idadi sawa ya 19 kwa nafasi ya Ubunge na Uwakilishi kila wilaya.   Wilaya iliyoshika nafasi ya tatu kwa wanawake wa CCM kujitokeza kwa wingi ni wilaya za Wete, iliyoibua wanawake 17, huku wilaya ya Chake chake ikishika nafasi nne kwa watia nia 16. Aidha wilaya ambayo wanawake waliojitokeza kwa wingi kwa nafasi ya Ubunge ni wil...

WAWILI WAFARIKI WAKICHIMBA MAWE MICHEWENI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WATU wawili wamefariki dunia, baada ya kufukiwa na kifusi wakati wakichimba mawe, shehia ya Mjini Wingwi wilaya ya Micheweni Pemba. Taarifa za mashuhuda zinaeleza kuwa, jana majira ya saa1:30 asubuhi watu hao, waliondoka nyumbani kwao na kwenda eneo hilo, kwa ajili ya kutafua mawe kama ilivyo kawaida yao. Mashuhuda hao, wakizungumza na waandishi wa habari, walisema wakati wapatwa na ajali hiyo wakiendelea kuchokoa mawe hayo, juu yao kulikuwa na mlima mkubwa wa kifusi. Mmoja wa manusura wa tukio hilo, Said Hamad Shoka, alisema wakati wanakata jiwe kubwa, juu yao kulikua na mapande ya kifusi, na kisha kuwafunika. ‘’Ni kweli kifusi ndicho kilichowafunika, wakati wao wakiwa chini wanachoko mawe, kwa ajili ya kokoto,’’alisema. Nae manusura Khatib Juma, alisema kama sio nguvu za Muumba kuwapa pumzi za kukimbiwa wakati kifusi kinaporomoka, idadi ya waliokufa yenge ongezeka. ‘’Wakati kifusi kinaporoka kilikuwa mbele yangu, nilitoka mbio nyingi sana...

TUME YA UTAANGAZAJI YAWAPA 'DILI' WAMILIKI WA REDIO

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ TUME ya Utangaazaji Zanzibar ‘TUZ’, imewataka wasimamizi na wamiliki wa vituo vya redio nchini, kukubali kubadilika kwa haraka, na kutoka mfumo wa sasa wa kidijitali na kuacha mafumo wa zamani wa analogia, kwani jamii imehamia huko.   Hayo yameelezwa jana, na Afisa kutoka Tume hiyo Zanzibar, Abubakar Mohamed Chwaya, alipokuwa akitowa mafunzo kwa wadau wa  vituo vya radio katika ukumbi wa Shirika la Utaanzaji Zanzibar ‘ZBC’ Mkoroshoni Chake chake Pemba.   Alisema mfumo mpya wa kisasa ‘digital’ utawawezesha wasambazaji hao, kurahisisha kuondosha muingiliano ya miundo mbinu ya sauti na  kazi zao, baina ya kituo kimoja na chingine. Alieleza kuwa, kutumia mfumo huo utaondosha matumizi makubwa ya gharama katika urushaji wa maudhui ‘content’ na utarahisha na matumizi madogo ya miundombinu. "Mfumo mpya wa kisasa ya kidigitali, utawawezesha wasikilizaji wako, kujua mapema kupitia kioo cha radio kupata kujua jina la radio, pam...

MBUNGE CUF PEMBA AJIUNGA CCM, AAZIMIA KUCHUKUA FOMU YA UBUNGE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la Pandani kwa tiketi ya Chama cha wananchi ‘CUF’ Maryam Omar Said, amsema kuaniza Juni 29, mwaka huu ametangaaza, kujiengua kwenye chama hicho na kujiunga na CCM, akidai amevutiwa na utekelezaji wa Ilani ya chama hicho, kwa miaka mitano iliyopita. Alisema, ameamua kurudi nyumbani, baada ya kuona yale yote aliyota ndani ya jimbo lake la Pandani, yamekelezwa ikiwemo miradi ya elimu, afya na maji safi na salama kwa miaka mitano iliyopita. Akizungumza na waandishi wa habari kisiwani Pemba alisema, hana sababu ya kubakia ndani ya CUF, na ameamua kuhamia CCM, ili kuungana na Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Alieleza kuwa, akiwa ndani ya CUF, hatakuwa na nafasi nzuri ya kushika bango la CCM na ndio maana, ameamua kwa hiari yake na bila ya kulazimishwa, kurudi ndani ya chama hicho. Mbunge huyo mstaafu wa CUF, alisema awali alikuwa mwana CCM, ingawa alitok...

WANAWAKE PEMBA WAKIWEMO WAANDISHI WA HABARI NAO MGUU SAWA UCHUKUAJI FOMU

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA ZOEZI la uchukuwaji wa fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi za ubunge, uwakilishi na viti maalum linaendelea kupamba moto, kwa wanawake,wakiwemo wanahabari kupishana ofisi za CCM wilaya za kisiwani Pemba . Zanzibar leo kisiwani Pemba, ambalo limepiga kambi katika ofisi hizo, limeshuhudia wandishi wabahari wanawake, wajasirimali, watendaji wa serikali na waachama wingine, wakitekeleza haki yao ya kidemokrasia. Akizungumza na gazeti hili, mmoja kati ya watia nia hao kwa nafasi ya ubunge Jimbo la Chake chake, Ashura Abdalla Simai 'mabodo', alisema moja ya sababu iliyomsukuma ni kutekeleza haki yake ya kikatiba ya kisiasa. Alieleza kuwa, pindi vikao vya chama vikiridhia jina lake na kurudi, atakwenda bungeni kuwatetea wanawake wenzake na wingine, kwani walio wingi hawajafanya hivyo. “Wanawake wamekuwa wakikosa matetezi kwa kina, wa mambo yanayotuhusu, hivyo nimechukuwa fomu hii kujaribu bahati yangu kwa mara ya tano,”alisema. Afisa hab...

WAISLAMU: ADHIMISHENI MWAKA MPYA WA KIISLAM KAMA ILIVYO ASILI

NA BAKAR KHAMIS, PEMBA@@@@   Waumini wa dini ya kiislamu,wametakiwa kuazimisha mwaka mpya kwa kulinganisha na historia ya uislamu. Hayo yameelezwa na imamu mkuu wa msikiti wa ng'ambwa wilaya ya chake chake mkoa wa kusini pemba sheikh Abdallah said mara baada ya khutba ya ijumaa Amesema waumini wa kweli hawana budi kujitathmini katika kipindi cha mwaka uliopita iwapo kuna mema waliyoyafanya waendeleze na mabaya wajikataze  "Kwa kweli hatuna budi kujitathmini katika kipindi cha mwaka uliopita wa 1446 kama kuna mema tuliyokua tukiyafanya tujitahidi kuyaendeleza na kuzidisha katika mwaka huu wa 1447 hijria kama shukran zetu kwa mola wetu" "Na pia maovu yote ya siri na ya dhahiri tujitahidi kuyaepuka ili tupate neema na salama". Kwa upande wake khatibu wa zamu Zahor Yahya Muhdhari, amesema maadhimisho mema ya mwaka mpya ni kusimamia malezi ya watoto na usimamizi wa familia. "Hakika watoto na wake zetu ni mtihani mkubwa kama ambavyo Allah s.w amesema kwa hivyo tu...

UWT YAWAALIKA WANAWAKE KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA

  BAKARI KHAMIS NA MOZA SHAABAN, PEMBA MAKAMu Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Zainab Khamis Shomari, amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uchukuaji wa fomu za kugombea nafasi mbali mbali za uongozi majimboni. Aliyasema hayo ofisi ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya Mkoa iliyopo Chake chake kisiwani Pemba, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea zoezi la uchukuaji wa fomu za lililoanza janaJuni 28. Alisema ni vyema wanawake kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo, kutokana na kuwepo kwa mazingira rafiki yanayowawezesha, kushiriki zoezi hilo bila kikwazo chochote. Alisema ushiriki wa wanawake katika kugombea nafasi za uongozi ni miongoni mwa matakwa ya ilani ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’, ambacho kipo madarakani, ambayo imeeleza kipaumbelechake cha uwepo wa wawakilishi wanawake kwa asilimia 50 katika vyombo vya kutunga sheria. Alieleza kwamba Umoja wa Wanawake Tanzania, umekua ukifanya jitihada mbali mbali katika kulitimiza takwa hilo,...