Skip to main content

Posts

Showing posts from June 29, 2025

MBUNGE CUF PEMBA AJIUNGA CCM, AAZIMIA KUCHUKUA FOMU YA UBUNGE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la Pandani kwa tiketi ya Chama cha wananchi ‘CUF’ Maryam Omar Said, amsema kuaniza Juni 29, mwaka huu ametangaaza, kujiengua kwenye chama hicho na kujiunga na CCM, akidai amevutiwa na utekelezaji wa Ilani ya chama hicho, kwa miaka mitano iliyopita. Alisema, ameamua kurudi nyumbani, baada ya kuona yale yote aliyota ndani ya jimbo lake la Pandani, yamekelezwa ikiwemo miradi ya elimu, afya na maji safi na salama kwa miaka mitano iliyopita. Akizungumza na waandishi wa habari kisiwani Pemba alisema, hana sababu ya kubakia ndani ya CUF, na ameamua kuhamia CCM, ili kuungana na Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Alieleza kuwa, akiwa ndani ya CUF, hatakuwa na nafasi nzuri ya kushika bango la CCM na ndio maana, ameamua kwa hiari yake na bila ya kulazimishwa, kurudi ndani ya chama hicho. Mbunge huyo mstaafu wa CUF, alisema awali alikuwa mwana CCM, ingawa alitok...

WANAWAKE PEMBA WAKIWEMO WAANDISHI WA HABARI NAO MGUU SAWA UCHUKUAJI FOMU

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA ZOEZI la uchukuwaji wa fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi za ubunge, uwakilishi na viti maalum linaendelea kupamba moto, kwa wanawake,wakiwemo wanahabari kupishana ofisi za CCM wilaya za kisiwani Pemba . Zanzibar leo kisiwani Pemba, ambalo limepiga kambi katika ofisi hizo, limeshuhudia wandishi wabahari wanawake, wajasirimali, watendaji wa serikali na waachama wingine, wakitekeleza haki yao ya kidemokrasia. Akizungumza na gazeti hili, mmoja kati ya watia nia hao kwa nafasi ya ubunge Jimbo la Chake chake, Ashura Abdalla Simai 'mabodo', alisema moja ya sababu iliyomsukuma ni kutekeleza haki yake ya kikatiba ya kisiasa. Alieleza kuwa, pindi vikao vya chama vikiridhia jina lake na kurudi, atakwenda bungeni kuwatetea wanawake wenzake na wingine, kwani walio wingi hawajafanya hivyo. “Wanawake wamekuwa wakikosa matetezi kwa kina, wa mambo yanayotuhusu, hivyo nimechukuwa fomu hii kujaribu bahati yangu kwa mara ya tano,”alisema. Afisa hab...

WAISLAMU: ADHIMISHENI MWAKA MPYA WA KIISLAM KAMA ILIVYO ASILI

NA BAKAR KHAMIS, PEMBA@@@@   Waumini wa dini ya kiislamu,wametakiwa kuazimisha mwaka mpya kwa kulinganisha na historia ya uislamu. Hayo yameelezwa na imamu mkuu wa msikiti wa ng'ambwa wilaya ya chake chake mkoa wa kusini pemba sheikh Abdallah said mara baada ya khutba ya ijumaa Amesema waumini wa kweli hawana budi kujitathmini katika kipindi cha mwaka uliopita iwapo kuna mema waliyoyafanya waendeleze na mabaya wajikataze  "Kwa kweli hatuna budi kujitathmini katika kipindi cha mwaka uliopita wa 1446 kama kuna mema tuliyokua tukiyafanya tujitahidi kuyaendeleza na kuzidisha katika mwaka huu wa 1447 hijria kama shukran zetu kwa mola wetu" "Na pia maovu yote ya siri na ya dhahiri tujitahidi kuyaepuka ili tupate neema na salama". Kwa upande wake khatibu wa zamu Zahor Yahya Muhdhari, amesema maadhimisho mema ya mwaka mpya ni kusimamia malezi ya watoto na usimamizi wa familia. "Hakika watoto na wake zetu ni mtihani mkubwa kama ambavyo Allah s.w amesema kwa hivyo tu...

UWT YAWAALIKA WANAWAKE KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA

  BAKARI KHAMIS NA MOZA SHAABAN, PEMBA MAKAMu Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Zainab Khamis Shomari, amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uchukuaji wa fomu za kugombea nafasi mbali mbali za uongozi majimboni. Aliyasema hayo ofisi ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya Mkoa iliyopo Chake chake kisiwani Pemba, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea zoezi la uchukuaji wa fomu za lililoanza janaJuni 28. Alisema ni vyema wanawake kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo, kutokana na kuwepo kwa mazingira rafiki yanayowawezesha, kushiriki zoezi hilo bila kikwazo chochote. Alisema ushiriki wa wanawake katika kugombea nafasi za uongozi ni miongoni mwa matakwa ya ilani ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’, ambacho kipo madarakani, ambayo imeeleza kipaumbelechake cha uwepo wa wawakilishi wanawake kwa asilimia 50 katika vyombo vya kutunga sheria. Alieleza kwamba Umoja wa Wanawake Tanzania, umekua ukifanya jitihada mbali mbali katika kulitimiza takwa hilo,...