Skip to main content

Posts

Showing posts from November 5, 2023

WATU WENYE ULEMAVU WAKABIDHIWA VISAIDIZI

  Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Abeida Rashid Abdallah amesema Wizara hiyo itaendelea kusimamia maendeleo ya jamii ikiwemo kundi la watu wenye ulemavu ili kuona wanaishi katika mazingira mazuri na salama. Akizungumza kwa niaba ya katibu mkuu huyo Mkurugenzi Idara ya Uendeshaji na Utumishi Dkt. Salum Khamis Rashid wakati akikabidhi visaidizi vya watu wenye Ulemavu kwa Taasisi ya Maisha Bora Fondation, katika ukumbi wa Wazee Sebleni. Dkt Salum alivitaja visaidizi hiyo ikiwemo na lotion 72 kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa ngozi ALBINO, fimbo nyeupe 20 kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa uoni, pamoja na viti vya magurudumu mawili 30 (Wheel chair) kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa viungo Alisema Wizara itaendelea kutatua changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi kadiri hali itakavyoruhusu ili kuhakikisha hakuna kundi ambalo limeachwa nyuma. Alieza kwamba moja kati ya jukumbu la Wizara hiyo ni kujenga ustawi mzuri kwa jamii hivyo Wizara hiyo itaendele

MIAKA MITATU YA DK. MWINYI PEMBA WAJENGEWA KIWANDA CHA USARIFU MWANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ NOVEMBA 3 ya miaka mitatu iliyopita, ilikuwa ndio siku ya kwanza ya Rais mpendwa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuwasili ndani ya Ikuklu ya Zanzibar. Kwa wakati huo, hakuwasili akitokea nchi jirani..laaahasha alitokea kwenye viwanja alivyokula kiapo, kushika hatamu ya uongozi. Maana Dk. Mwinyi, baada ya kumalizika kwa kampeni za zaina yake, zilizotajwa kama za kisayansi kwa kule kukutana na makundi mbali mbali, kisha wananchi walimpigia kura. Baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa vyama vingi, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC, ilimtangaaza Dk. Mwinyi kuwa rais wa Zanzibar kwa kupata asilimia 76.27 na kuwaacha mbali wagombea wenzake. ‘’Nimepokea ushindi kwa mikono miwili na nawashukuru wananchi wa Zanzibar kwa kunichagua mimi na chama changu, kwa miaka mitano ijayo,’’alisema wakati huo. Kwa wananchi Zanzibar, kama alivyosema Mwenyekiti wa CCM mkoa wa kaskazini Pemba Mberwa Hamad Mberwa, kuwa duniani viongozi kama aina ya Dk. Mwinyi ni

MBUNGE ASIYA AWAKUMBUSHA JAMBO WAZAZI WA QAMARIA WETE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MBUNGE wa Viti maalum mkoa wa kaskazini Pemba Alhajjat Asiya Sharif Omar, amewakumbusha wazazi na walezi, wenye watoto wao Almadrassatul-Qamariyya ya Wete, kulipa ada za watoto wao kwa wakati, ili kuwapa uhakika waalim kufundisha kwa ufanisi. Alisema, maendeleo yaliopo katika madarassa hiyo, hayakuja bure, hivyo ili yawe endelevu, hakuna budi kwa wazazi na walezi kujikumbusha namna ya ulipa ada. Mbunge huyo aliyasema hayo, ukumbi wa zamani wa baraza la wawakilishi Wete, kwenye mahafali yalioambatana na siku ya wazazi kwa madrassa hiyo. Alisema, maendeleo endelevu katika madrassa hiyo, hayatokuja kwa haraka na kudumu, ikiwa wazazi watapuuzia suala la ulipa ada kwa watoto wao. Alieleza kuwa, madarassa hiyo haina mfadhili wala ruzuku kutoka serikalini, hivyo na inategemea moja kwa moja ada kutoka kwa wazazi na walezi, wenye watoto wao katika madrassa hiyo. “Nichukuwe nafasi hii, kuwasisitiza wazazi na walezi kuhakikisha wanalipa ada zao kwa wakati,