Skip to main content

Posts

Showing posts from September 3, 2023

WANANCHI KIDAGONI WAKOSA ELIMU KISA............

  ZANZIBAR     Na Nafda Hindi,  ZANZIBAR  @@@@  WANANCHI wa Shehia ya Kigongoni Wilaya ya Kaskazini 'A' Unguja walalamikia umbali wa masafa marefu kwa watoto wao wakifuata huduma ya Elimu. wameiomba serikali kuwajengea skuli karibu na makaazi yao ili Watoto wao wapate elimu ipasavyo na kuwaepusha na hali hatarishi.   Malalamiko hayo yamekuja kufuatia ziara ya kuibua changamoto za wananchi iliyoandaliwa na Chama cha waandishi wa Habari wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar kupitia mradi wa kuwainua wanawake katika  Uongozi, Strengthen Women In Leadership   (SWIL) unaotekelezwa na chama hicho.   Wazazi wa watoto hao wamesema kwa sasa Watoto   wanasoma skuli ya   mbali ambayo wanatembea Zaidi ya saa moja hali inayohatarisha usalama wao na wengine kushindwa   kufika skuli kuendelea na masoma na kuishia vichakani .   “Skuli iko mbali na sisi inabidi twende Fukuchani. Kidagoni au Kidoti hali ambayo ina hatarisha usalama wa watoto wetu, na sisi wazazi huwa hatuna Amani mp

Uzazi wa mpango ni haki inayopaswa kufurahiwa na wote

  Na Mwandishi wetu, @@@@ Dhana ya kupanga uzazi kama haki ya binadamu ni muhimu. Inapinga maoni yoyote potofu kwamba ni aina ya udhibiti wa idadi ya watu na itahakikisha kwamba vizazi vijavyo kamwe havichukui haki hii ya kibinadamu iliyopatikana kwa bidii kuwa ya kawaida. Katika kuhakikisha huduma za afya ya uzazi zinafikiwa kwa urahisi, mafunzo ya siku tatu kuhusu SRHR yalifanyika kwa waandishi wa habari, uhamasishaji ulifanywa kwa siku mbili, na vyombo vya habari vilijengewa uelewa kuhusu SRHR ikiwa ni pamoja na uzazi wa mpango. Hata hivyo, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, bado kuna changamoto katika upatikanaji wa huduma za afya ya uzazi. Kwa mfano, ingawa upatikanaji wa uzazi wa mpango ni haki ambayo inapaswa kufurahiwa na wote, lakini sio wote wanaofaidika na haki hiyo. Na ingawa ni wazi kuwa uzazi wa mpango unachangia katika kupunguza vifo vya uzazi na kuhakikisha kuwa akina mama na watoto wachanga wanakuwa na afya njema, wanandoa wengi bado wananyimwa haki ya kupanga uzazi n

Zanzibar contains shortage of HIV testing kits

  By Our reporter@@@@ THE government has contained the shortage of HIV rapid testing kits that faced public health facilities throughout the country in the past three months. The Isles Health Minister, Nassor Ahmed Mazrui, said that the kits have been already distributed in health facilities across the country and that the shortage is now under control. Mazrui said the reason behind the shortage of HIV test kits was attributed to the delay in importing medical supplies.  “The kits had already arrived and distributed in the hospitals and health centres from Monday,” he said. Earlier, service providers in health facilities said there was a severe shortage of HIV testing kits, leaving the country with incomplete data as new cases could be going unreported. As a result, some voluntary counseling and testing centres had to turn people away due to the shortage of the HIV testing kits. Some of the health facilities that had reported the shortage from June, 2023 are Mwera, Fuoni, Magirisi, Tun

Afya za Vijana ziko hatarini kukosekana Vipimo vya kupima virusi vya Ukimwi (HIV KITS)

  NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR@@@@ KUKOSEKANA kwa vipimo vya kupimia maambukizi yanayosababisha ukimwi (HIV Kits) Zanzibar ni jambo linalowarejesha nyuma vijana kujitokeza katika vituo vya Afya kupima afya zao. Hayo yamebainika kufuatia ziara iliofanywa na Chama Cha Waandishi wa habari Tanzania TAMWA,ZNZ wakati wa kutembelea vituo vya Afya na huduma Rafiki kwa vijana vilivyopo Wilaya ya Kati na Magharibi “B”.   Wakizungumza kwa nyakati tofauti watoa huduma za Afya kutoka vituo mbali mbali wamesema licha ya vijana kuwa na mwamko wa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya Afya kupima afya zao kwa sasa imekuwa ni tofauti kwa kukosekana vipimo vya maambukizi ya virusi vya ukimwi ambapo huvikimbia vituo hivyo. “Idadi ya vijana ilikuwa iko juu na inaongezeka kwa kasi kupima Afya zao katika kituo chetu hasa virusi vinavyosababisha ukimwi ila kwa sasa kila leo idadi inapunguwa kutokana na tatizo la kutokuwepo vipimo vya kupimia maambukizi hayo,(HIV KITS), “ Mtoa huduma kituo cha Afya Mwera

DK. MWINYI ATOA RAI KWA WASIO WATANZANIA

  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi amewataka   Wananchi   ambao sio raia halali wa Tanzania kufika katika   Ofisi za Uhamiaji kwa lengo la kujiorodhesha ili waweze kutambulika rasmi katika nchibya Tanzania.  Aliyasema hayo wakati wa kukabidhi vyeti vya Uraia Tanzania kwa Tajnisi hoko ikulu katika Mkoa wa Mjini Unguja, ambapo alisema baaadhi ya wanachi wanashi  Tanzania bila ya utambulisho wowote .   "Nawaomba Wananchi  ambao kwa namna moja au nyengine hawajafika kwenye Ofisi za Uhamiaji kujiorodhesha, ni vyema wakaitumia fursa hiyo ili waweze kutambuliwa rasmi. Serikali zetu zimedhamiria kulimaliza tatizo hili kutokana na athari zake ." alisema Dk Mwinyi Pia alisema Jumla  ya wananchi elfu tatu mia tatu na kumi na tisa  3,319 wamekabidhiwa vyeti vya uraia wa Tanzania tajnisi Ikiwemo Msumbiji,Comoro,Burudi na Ruwanda. " Kwa hakika, nchi, yetu leo inaandika historia mpya ya kulikamilisha jambo hili kubwa la kuwapa uraia

KIJALABU iSAVE ZANZIBAR WAWANOA VIONGOZI UCHUKUAJI MIKOPO

                                                                               NA MARYAM SALUM,PEMBA@@@@ VIONGOZI na wanachama wa vikundi vya kuweka na kukopa  Pemba,   wametakiwa kuondokana na woga na badala yake kuchukua mikopo kwa ajili  ya  kuendeleza biashara zao.  Akifungua mafunzo ya siku mbili juu ya ushirikishwaji kwa viongozi wa  vikundi vya maendeleo katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya TAMWA Pemba,  Mratibu wa Chama cha Waandishi wa habari TAMWA, Fat-hiya Mussa Said alisema kuwa lengo la mradi wa Kijaluba iSave Zanzibar ni kuwainua  kiuchumi wanavikundi hasa watu wenye ulemavu.  Alisema kuwa fedha zilizopo kwenye Hisa zinatakiwa kukopwa kwa ajili  ya kuendeleza biashara na sio kutazamwa tu. "Mradi wa Kijaluba iSave Zanzibar unakusudia kuwatoa woga,ili kuona  fedha zilizopo kwenye hisa munazichukua kwa mkopo kwa ajili ya  kuboreshea biashara zenu kwa maendeleo zaidi," alisema mratibu huyo. Alieleza kuwa fedha zilizopo zinatakiwa zitumiwe, na matumizi yenyewe  ni kwa