Skip to main content

Posts

Showing posts from July 23, 2023

WANAWAKE MLETENI WAKUMBUSHIA AHADI UJENZI KITUO CHA AFYA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAWAKE wa kijiji cha Mleteni shehia ya Kisiwani wilaya ya Wete, wameikumbusha serikali kuwajengea kituo chao cha Afya, kama ahadi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alivyoitoa wakati alipowatembelea. Walisema, tayari wameshakuwa na eneo ambalo walitakiwa kulitoa kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha afya, ingawa hadi sasa ni miezi zaidi ya mitano tokea Rais atowe ahadi, ingawa hakujaanza ujenzi. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, walisema wanahamu kubwa na kujengewa kituo hicho, ili sasa kwao iwe rahisi, kupata huduma mbali mbali zikiwemo za uzazi na mtoto. Walieleza kuwa, wamekuwa wakiifuata huduma hiyo eneo la Kisiwani ambapo pana umbali wa zaidi ya meli mbili, jambalo linalowapa ugumu, hasa kutokana na uchakavu wa barabara yao. Mmoja kati ya wanawake hao Aisha Nassir Sheha, alisema kutokana na umbali wa kituo cha afya hasa huduma za mama na mtoto, wengi wao wamekuwa hawamali

ELIMU YA AFYA YA UZAZI NI HAKI KWA KILA BINADAMU

   NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR   VYOMBO vya habari nchini vimetakiwa kuibua matatizo mbalimbali yanayohusiana na afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana jambo ambalo husababisha wanawake wengi kutojiunga na huduma ya afya ya uzazi.   Akifungua mafunzo ya siku tatu kwa vyombo vya habari kwa niaba ya Mkurugenzi wa chama cha  waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA ZNZ,  mjumbe wa bodi ya Chama hicho Shifaa Said Hassan, alisema ni wajibu kwa waandishi kufatilia na kuandika matatizo yanayowakabili wanawake hususani wanapotaka kujiunga na  huduma hizo ili waweze kujua njia bora na salama.     “Licha ya kuwepo kwa sera na seheria zinazosisitiza umuhimu wa mwanamke kupata huduma hizo lakini inaonekana asilimiia kubwa ya kundi hilo hawana uelewa wa kutosha juu ya matumizi sahihi ya huduma hiyo hivyo kupitia vyombo vya habari itakuwa chachu ya kuwaelekeza na kufikia malengo ya kuimarisha afya zao,”Shifaa Said, amesma.   Aidha aliwaomba   waandishi wahabari kuwa kusikiliza kwa m

HAKI YA AFYA YA UZAZI JUKUMU LA WOTE: TAMWA-ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JAMII imekumbushwa kuwa, suala la afya ya uzazi, sio jukumu la mwanamke pekee, kama wengine wanavyofikiria, bali linahusu jamii yote, ili kuwa na afya bora iwe ya kimwili au kiakili.   Kauli hiyo imetolewa leo Julai 29, 2023 na Afisa Mradi wa haki ya afya ya uzazi kutoka Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA- Zanzibar Zaina Abdalla Mzee, wakati akiutambulisha mradi huo, kwenye mafunzo ya siku tatu kwa waandishi wa habari, kisiwani Pemba. Alisema, imegundulika na tafiti zinaonesha kuwa, linapozungumza suala la haki ya afya ya uzazi, huangaliwa zaidi mwanamke, bila ya kumuhusisha mwanamme. Alieleza kuwa, hakuna suala la uzazi linalomgusa mwanamke pekee, na hasa likihusisha afya, kwani mwanamme asipowajibika, anaweza kusababisha madhara kwa mjamzito na mtoto wake. ‘’Hii ndio maana, TAMWA-Zanzibar imeibua mradi huu ambao sasa utawawezesha waandishi wa habari, kuieleza jamii, madhara ya kutozingatia haki ya afya ya uzazi na faida zake,