Skip to main content

Posts

Showing posts from June 8, 2025

MJANE WA WATOTO SABA AOMBA MSAADA PEMBA

  NA FATMA HAMAD, PEMBA@@@@ MJANE mwenye watoto saba amewaomba wahisani na watu wenye uwezo, kumpa msaada wa bati na miti, kwa ajili ya kuezekea nyumba yake, ili apate kustirika na watoto wake. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi nyumbani kwake kijiji cha Madenjani Wilaya ya Wete Pemba, leo Juni 12, 2025 mama huyo Rehema Salum,  alisema nyumba anayokaa imeshakua mbovu, mvua yote inamnyeshea ndani mwake. Alisema anapatashida kwani mvua inaponyesha husimama barazani hata kama ni usiku mkubwa,kwa vile ndani hujaa maji na kukosa sehemu salama. ‘’Ndani hujaa maji, vitanda vyangu vyote vimeshaharibika sina hata pakulala na watoto wangu saba, naomba binadamu wezangu munisaidie nateseka,’’alilalamika. Alieleza tayari alishajenga vyumba viwili vya matufali, ingawa ameshindwa kuezeka, hivyo ameomba asaidiwe bati pamoja na miti kwa ajili ya kuezekea, ili apate kuishi sehemu anapostahiki   binadamu. Alifahamisha kuwa mume wake amemuacha na watoto saba, na kumuachia mz...

MAJENZI KENGEJA WAANZISHA MALEZI YA PAMOJA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa kijiji cha Majenzi shehia ya Kengeja wilaya ya Mkoani, wameamua sasa kuyarejesha malezi ya pamoja, ili kuwa na taifa la sasa na baadae, lenye malezi, makuzi na maadili mema.   Wakizungumza kwenye kikao cha pamoja kilichofanyika leo Juni 8, 2025 kijijini hapo, wameamua kuanzia sasa malezi ya vijana wao, yawe ya pamoja, ili kuona wanakuwa na taifa lenye viongozi wenye maadili.   Walisema, kwa sasa vijana waliowengi kijijini hapo, wamekuwa na malezi yasioendana na maadili, jambo ambalo linahatarisha usalama wao na wazazi wao.   Mmoja kati ya wazazi hao Habib Mohamed Habib, alisema ni jambo jema kuona wazazi kuanzia sasa wanakusudia kusaidiana malezi, maana mzazi mmoja pekee ni vigumu kufanikisha malezi.   ‘’Mimi naunga mkono suala la malezi ya pamoja, katika kijiji chetu, maana hali imekuwa mbaya ya maadili ya vijana wetu, na kusababisha uwepo viashiria vya uhalifu kama wizi,’’alisema.   Nae ...