Skip to main content

Posts

Showing posts from January 7, 2024

MKURUGENZI USTAWI: 'TUTAENDELEZA USHIRIKIANO NA WADAU KWA MASLAHI YA JAMII'

  NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR@@@@ MKURUGENZI Idara ya Ustawi wa Jamii na Wazee ndugu Hassan Ibrahim Suleiman amesema Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha Ustawi wa jamii unakuwa na wananchi wanaishi katika mazingira mazuri na salama. Akifungua mafunzo juu Sera ya hifadhi ya Jamii, yaliyofanyika katika ukumbi wa Sebleni,Unguja amesema ni vyema Idara hiyo kujenga mashirikiana na wadau mbalimbali kwani mtoto anahitaji kukua katika makuzi mema yatakayomjenga kuwa Raia bora kwa Taifa lake. “Idara ya Ustawi wa Jamii na Wazee inabeba jukumu zito hivyo, wanawajibu wa kushirikiana na kusaidia na wadau wengine katika kukuza ustawi wa jamii ili jamii waishi katika mazingira mazuri, hivyo nakuombeni mtowe mawazo yenu juu ya Sera hii, kwani maoni yenu yatasaidia kupata Sera bora” Alisema Hassan. Alieleza kwamba jamii inahitaji mambo mengi hasa ukizingatia kundi la kinamama wanaotelekezwa na watoto wao, wanakuwa kati

WANAWAKE MGELEMA SASA WASHUSHA PUUMZI NI BAADA YA...............

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAWAKE wa shehia ya Mgelema wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema baada ya kukamilika kwa ujenzi wa barabara yao kwa kiwango cha lami, roho zao zimewatua na hasa inpotekezea kutaka kwenda hospitali kuu, kufuata huduma za mama na mtoto. Walisema, kwa karne zaidi ya moja, hawakuwa na furaha na wakielewa na machungu, inapotokezea wamepewa rufaa ya kwenda hospitali ya wilaya ya Chake chake, kutokana na shida ya barabara yao, ilivyokuwa. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, mara baada ya kufunguliwa kwa barabara yao ya Kipapo-Mgelema, na Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Massoud Othman, walisema sasa joto limewatua. Mmoja kati ya wanawake hao Maryam Mohamed Issa, alisema ijapokuwa ni mgeni kijijini hapo, lakini ameshatimiza miaka tisa ya mateso, shida na tabu ya kuitumia barabara hiyo. ‘’Binafsi, mara mbili nilipokuwa mjamzito, nilitakiwa niripoti hospitali ya wilaya ya Chake chake, kwa uchunguuzi zaidi, lakini nilishindwa

PEMBE AWATAKA MAMA NTILE WAWE WABUNIFU KIBIASHARA

  Na muandishi wetu @@@@ Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma amewashauri wajasiriamali nchini, kuendelea kutumia ubunifu wao wa kupika vyakula mbalimbali kwa ajili ya biashara zao za mama ntilie ili waweze kujikwamua na umasikini. Kauli hiyo ameitowa wakati akizungumza na wajasiriamali katika uwanja wa urafiki, Jimbo la Shaurimoyo, Unguja katika mashindano ya mapishi ikiwa ni shamrashamra za miaka 60 ya Mapainduzi ya Zanzibar. Mhe Riziki katika yeyete ile inahitaji ubunifu hivyo ni vyema mama ntilie wawe wabunifu katika mapichi mbali mbali katiba biashara ya chakula kwani hatua hiyo itasaidia kuongeza kipato na kujikwamua an umasikini. Waziri Pembe amewataka wajasiriamali hao kuitumia fursa ya mikopo iliyopo   ikiwa ni juhudi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la   mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi ya kuwawekea mazingira wezeshi wajasiriamali kwa nia ya   kufikia malengo waliyojiwekea. Aidha amesema Oryx Gas na Azania Group, wamea

MAJUKUMU MAZITO YA FAMILIA CHANZO CHA WANAWAKE KUTOGOMBEA UONGOZI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA Jamii ya Tanzania, kama ilivyo katika nchi nyingi nyengine, imejenga mazoea ya kuwa mwanawake ni mama wa nyumbani tu na hapaswi kushiriki au kushirikishwa katika mambo ya maendeleo.   Kwa maana nyengine mwanamke amekuwa kama abiria katika basi na hana maamuzi juu ya safari, seuze ya kupewa usukani wa kuongoza hicho chombo.                      Mtazamo huu uliokuwa unatumika kwa muda mrefu umeiathiri jamii na kumuacha mwanamke kuwa nyuma, jambo ambalo sio sahihi kabisa.   Hali hii ipo kinyume na mafunzo na maelekezo ya dini mbali mbali.    Kwa mfano, katika dini ya Kiislamu mwanamke hatakiwi kuachiwa pekee mzigo mzito wa nyumbani na pamekuwepo matokeo ya mwanamke kupewa uongozi hata katika masuala mazito, kama ya kuongoza kikosi kwenye vita.   Zipo hadithi sahihi na simulizi nyingi juu ya namna wanawake walivyoongoza kwa mafanikio, wakiwa kama majeshi.   Mzigo mzito wa nyumbani wanaoachiwa akina mama umekuwa sababu kubwa ya ku

INSPEKTA KHALFAN: ATAKA UDHIBITI MAJANGA YA MOTO

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@   MKAGUZI wa shehia ya Pandani wilaya ya Wete Pemba, Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi, amewataka wananchi kuchukua tahadhari na kujikinga na majanga mbali mbali yanayoweza kutokea ikiwemo ya moto.   Alisema kuwa, ni vyema kufuata utaratibu nzuri, wakati wanapoamua kujenga nyumba katika maeneo yao, kwa kuweka nafasi ya kutosha baina ya nyumba moja na nyingine, ili linapotokea janga la moto lisiweze kuathiri nyumba nyingi.   Aliyasema hayo wakati akikabidhi msaada wa vifaa vya skuli, kwa watoto wa familia ya mzee Mwalimu Kombo Said wa kijiji cha Madebeni shehia ya Pandani wilaya ya Wete, kufuatia tukio la moto lililounguza nyumba yao Novemba 11 mwaka jana.   Alisema kuwa, familia hiyo ilipata janga la moto ambao uliunguza nyumba yao na kuteketeza kila kitu kilichokuwemo ndani, hali iliyomfanya kuiahidi familia hiyo kuwanunulia watoto vifaa vyote vya kusomea.   "Nawapongeza wananchi kutafsiri kwa vi

MAKAMU WA PILI AZINDUA BANDARI YA MKOANI, ASEMA NYINGINE TATU KUJENGWA PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, amesema, serikali inampango wa kuzijenga bandari za Wesha, Wete na Shumba, ikiwa ni miongoni mwa maono ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kukifungua kisiwa cha Pemba kiuchumi. Alisema kwa kuanzia, tayari shughuli kadhaa zimeshafanyika kwa awamu ya kwanza, kuelekea ukamilishaji wa upanuzi wa bandari ya Mkoani, ikiwemo ujenzi wa njia za kupitia abiria, ujenzi wa eneo la kuwekea makontena pamoja na ununuzi wa mashine za kushushia makontena hayo. Makamu huyo wa Pili, aliyasema hayo Disemba 7, mwaka 2024, bandarini Mkoani Pemba, mara baada ya uzinduzi wa bandari hiyo, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, Alisema, ili kuelekea uchumi mzuri, serikali inayodhamira ya kweli ya kuhakikisha bandari nyingine za kisiwani Pemba, zinajengwa na zinakuwa za kisasa, ili wananchi watanue wigo wa usafiri na usafirishaji. Alieleza kuwa, kazi hiyo inatarajiwa kuanza

SPIKA ZUBEIR AWAONESHA NJIA VIJANA KUPATA 'MAOKOTO'

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Zubeir Ali Maulid amewataka vijana kutumia vyema fursa zilizopo, ili kustawisha uchumi wa nchi na kujiletea maendeleo. Aliyasema hayo Disemba 6, mwaka 2024 wakati akifungua kongamano la miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar lililoandaliwa na Wizara  ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo katika Ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake Chake Pemba. Alisema kuwa, Zanzibar imepiga hatua kubwa kimaendeleo katika sekta zote tofauti na kabla ya Mapinduzi, ambapo Serikali ya awamu ya nane imeweka mazingira mbali mbali ya kuwawezesha wananchi wake kiuchumi,  hivyo ni vyema wakazitumia zaidi fursa hizo kwa ajili ya kujiimarisha. "Hatua hii tuliyofikia sasa inaenda sambamba na mafanikio ya Mapinduzi yetu matukufu ya Zanzibar, hivyo hatuna budi kuyaenzi na kuyaendeleza kwa maslahi bora ya Taifa letu," alisema spika huyo. Aidha alieleza kuwa, ni wajibu wa kila mwananchi kuwa na uzalendo, kulinda amani ya nchi na kuwa tayari k