Skip to main content

Posts

Showing posts from December 17, 2023

SORAGA AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA POLISI MKOANI, AACHA UJUMBE WA MAPINDUZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Nchi, Ofis ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar,   Mudrik Ramadhan Soroga, amesema miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar, imemletea heshima mzanzibari, kwa kupata haki zake bila ya ubaguzi, ikilinganishwa na kabla ya mwaka 1964. Alisema, kwa sasa kila mmoja anapata haki ya kuwasilisha lalamiko lake, katika vyombo vya sheria na kupokelewa kwa heshima na kisha kusikilizwa na uamuzi kutolewa kwa haki. Waziri Soraga, aliyasema hayo leo Disemba 22, 2023  mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la kituo cha Polisi cha wilaya ya Mkoani cha daraja ‘B’ ikiwa ni sehemu za shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar ya mwaka 1964. Alisema, sasa mzanzibari anatembea kifua mbele, akijua kuwa inapotokezea kubinywa kwa haki zake, anapopakukimbilia na kufungua mashauri, ambayo yanaendeshwa kwa haki kuanzia mwanzo hadi mwisho. Alieleza kuwa, waasisi wa taifa hili walipigania haki za wazalendo na mwendo huo unaendelezwa hadi leo ndani ya serikali ya Ma

Wanahabari wanawake wapewa mbinu kukwepa mitego ya udhalilishaji mitandaoni

  Na Amina Mchezo, Zanzibar@@@@ Waandishi wa habari wanawake wananafasi na mchango mkubwa katika kuielimisha jamii kupitia mitandao ya kijamii kukizingatiwa usalama wao. Akifungua mafunzo ya siku mbili  Kwa waandishi wa habar wanawake Zanzibar mkufunzi na mwanahabar mkongwe kutoka nchini Kenya  Cecilian Maundu amesema wanahabar wanawake wamekuwa wakipitia wakati mgumu wakiwasilisha kazi zao za kimtandao ukilinganisha na wanahabar wakiume. Amesema hali hiyo huwawia vigumu baadhi ya waandishi kuendelea na kazi yao na wengine kuathirika kisaikolojia kutokana na baadhi ya wafuasi wa kimtandao kuwatolea maneno ya kashfa pasi na wao kuridhia. Maundu amesema hali hiyo inaweza ikaondoka au kusaidiwa endapo kutakuwa na ushirikiano wa pamoja kati ya waandishi na taasisi za kihabar ili kuunda kikosi kazi ambacho kitamlinda mwandishi pale tu anapopata kadhia ya kimtandao. "Zanzibar mnapaswa kutumia taasisi hizi kama ZPC, TAMWA, MCT na nyengine ili pale kuona mnashambulia Kwa pamoja mitandaoni

SHAMATA AZINDUA SOKO LA KISASA MTAMBILE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Shamata Shaame Khamis, amewaagiza wakulima wa ndizi wilaya ya Mkoani, kuepukana na vishoka wa biashara hiyo, na badala yake walitumie soko jipya la Mtambile, ili kupata bei kubwa. Waziri Shamata aliyasema hayo jana, mara baada ya ufunguzi wa soko la mboga na matunda la Mtambile wilaya ya Mkoani, ikiwa ni sehemu za shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar ya mwaka 1964. Alisema, kuanzia sasa waachane na wanunuzi wa ndizi wanaowalalia kibei, na badala yake sasa walitumie soko hilo, ili kuzipandisha thamani ndizi zao. Alieleza kuwa, ndani ya soko hilo mtakuwa na mnada maalum wa mazao mbali mbali, ikiwemo ndizi, muhogo, matikti, nyanya, chungwa na ndimu, hivyo ni wajibu kwa wakulima hao, kulitumia soko hilo. Waziri Shamata, alisema kwa muda mrefu, wakulima walikuwa wanalaliwa kibei na wachuuzi wanaosafirisha bidhaa hiyo nje ya kisiwa cha Pemba, kwa kueleza kuwa kunaanguko la bei. ‘’

HIVI NDIVYO WILAYA YA CHAKE CHAKE, ILIVYOZINDUA SHAMRA SHAMRA ZA MIAKA 60 YA MAPINDUZI ZANZIBAR

  MKUU wa mko wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud na Mkuu wa wilaya ya Chake chake Rashid Abdalla Ali, leo waliungana na baadhi ya viongozi wa chama, serikali, vikosi vya ulinzi na usalama na wananchi wingine pamoja na wafanyakazi wa serikali, katika usafi uliofanyika barabara ya uwanja wa ndege Pemba. Ambapo zeozi hilo ni ishara ya uzinduzi wa shamra shamra za kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, yalioasisiwa Januari 12, mwaka 1964. Kisha Mkuu huyo wa Mkoa aliwahutubia wananchi na kuwataka wayalinde mapinduzi ya Zanzibar, kwani ndio yaliowakomboa wanyonge wa taifa hili. Lakini akawakumbusha wannachi kuwa, ndani ya miaka hii 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, mkoa unao miradi ya maendeleo 23, ikiwemo miradi tisa ya uwekaji mawe ya msingi, miradi 10 itafunguliwa na miradi minne itazinduliwa ndani ya mkoa huo pekee. Akaeleza kuwa, zoezi la kufanya mapainduzi ya Zanzibara hapo mwaka 1964, lilikuwa gumu na zito, ingawa waasisi wa taifa hili walifanikiwa na sasa kila mmoja ameshayaona mat

WAZIRI RIZIKI PEMBE ATOA DARSA NZITO KUDUMISHA UTAMADUNI ZANZIBAR

  WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma ameitaka jamii kuacha tabia ya kuiga tamaduni za kigeni ambazo haziendani na mila,silka na utamaduni wa kizanzibari ikiwemo suala la mavazi na malezi. Mhe. Pembe ameyasema hayo katika Maonesho ya mavazi ya wiki ya ya Mafunzo ya Amali yanaliofanyika katika viwanja vya Mapinduzi Square Michenzani Mjini Unguja, amesema mavazi ya staha ni moja ya Utamaduni wa wazanzibari hivyo ni vyema kuendelezwa na kuacha kuiga mavazi ambayo hanastaha. Amefahamisha   kwamba mavazi ya staha na malezi bora ni njia moja wapo ya kuzuia    vitendo vya ukatili na dhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto ambavyo vinajitokeza kila mara ndani ya jamii. “suala la kuiga tamaduni zisizo za kizanzibari ambazo baadhi yake ndio sababu kubwa ya mporomoko wa maadili ya nchi na kusababisha vitendo vya udhalilishaji kuongezeka kila siku ni vyema kuachana nazo na badala yake kuendeleza mila, silka na Utamaduni wa Zanzibar” Alisema Waziri hu

TUME YA UTANGAAZAJI, WADAU PEMBA WAJADILI SHERIA YA TUME

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WADAU wa Tume ya Utangaazaji Zanzibar, kisiwani Pemba, wamekutana na watendaji wa Tume hiyo, tayari kwa ajili ya kuanza mchakato, wa kuifanyia mabadiliko sheria yao nambari 7 ya mwaka 1997. Kwenye kikao hicho, kilichofanyika leo Disemba 19, 2023 ukumbi wa wizara ya Habari Gombani Chake chake, pamoja na mambo mingine, watendaji hao wa Tume, waliwasilisha mapendekezo yao, na kisha kupokea ya wadau wao. Akizungumza kabla ya upokeaji wa maoni hayo, Katib Mtendaji wa Tume ya Utangaazaji Zanzibar Suleiman Abdalla Salim, alisema, wanakusudia kuwa na sheria rafiki kwa vyombo vya habari vya utangaazaji na vile vya mtandaoni. Alisema, ndio maana Tume imeanza kuwashirikisha wadau wa Unguja na Pemba, ili nao kupata nafasi ya kutoa maoni yao, kuelekea sheria mpya hapo baadae. Alieleza kuwa, haikuwa busara kwa Tume kujifungia ndani na wataalamu wake na kisha kuwasilisha rasimu ya sheria ngazi ya Makatibu wakuu, bila ya kukutana na wadau wao. ‘’Tume kwa sas

IPA: ‘’WAALIMU ENDELEENI KUJIPAMBA KWA TABIA NJEMA’’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ CHUO cha Utawala wa Umma Zanzibar ‘IPA’ tawi la Pemba, kimewakumbusha waalimu, wa skuli za wilaya ya Chake chake, kuendelea kuwa kioo, kwa kuwa na maadili mema ndani ya jamii. Ushauri huo umetolewa Disemba 18, 2023  na Mkuu wa chuo hicho tawi la Pemba, Juma Haji Juma, wakati akiwasilisha mada ya maadili kwa watumishi wa umma, kwenye mafunzo ya uthibitisho wa kazi, kwa waalimu hao, mafunzo yaliyofanyika skuli ya sekondari Madungu wilayani humo. Alisema, jamii inategemea na kusoma kila kitu kutoka kwa Mwalimu, hivyo ni wajibu wake, hilo kulijua na kuhakikisha anaendelea kung’ara ndani ya jamii, kwa kujipamba na maadili mema. Alisema, Mwalimu anaangaliwa kuanzia kivazi, matendo, jinsi anavyokula na mazungumzo yake katika jamii, hivyo anapaswa kuhakikisha anakuwa makini saa 24 kwenye maisha yake. Alieleza kuwa, miongozo ya sheria na kanunu za kiutumishi, zipo kwa ajili ya kutoa muongozo zaidi, lakini Mwalimu mwenyewe analazimika kuongeza wigo, wa kujipam

Wawakilishi wanawake waupiga mwingi majimboni 'Watatua changamoto lukuki, wananchi wafurahia'

    NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@   Katika majimbo mengi Unguja na Pemba ni kawaida kusikia malalamiko ya waliochaguliwa kuingia Baraza la Wawakilishi, Bunge na Udiwani nadra kuonekana, tafauti na walipohangaika kuchaguliwa.   Hii ilipelekea majimbo mengi kuzorota kimaendeleo kwa vile hapakuwepo watu waliohangaikia shida zao na kilichosikika ni wananchi kulalamika kwamba waliowachagua kupeleka mbele madai yao hawaifanyi kazi kama walivyotarajia.   Hali ilianza kubadilika hivi karibuni kutokana na kuibuka wanawake majasiri na wanaojituma kuhangaikia kero hizi baada ya kushika hatamu za uongozi katika ngazi mbali mbali.   Wapo watu waliodiriki kusema laiti zamani kungekuwa na wawakilishi wanawake kama hawa waliopo sasa, matatizo ya majimbo mengi yangepatiwa ufumbuzi na yangepungua.   Licha ya kuwepo viongozi wanawake wachache, lakini kazi waliyoifanya wengi wao ni kubwa na inathibitisha maelezo ya kwamba siku zote mama huwa na huruma na ndio maana wawakilishi wanawake