Skip to main content

Posts

Showing posts from September 17, 2023

MAKTABA ZA SKULI ZIWE CHEM CHEM YA UFAULU KWA WANAFUNZI

             NA TATU NAHODA, ZU@@@@ ……………fuata nyuki ule asali……………. Ndivyo walivyosema wahenga, wakimaanisha kuwa, unapaswa kufuata vitu, watu au sehemu zenye ujuzi, ili kufanikiwa katika malengo yako.   Msemo huu unatumika katika nyanja nyingi ikiwemo ya wanafunzi wanaofuta elimu, hasa kwa mfumo wa kupitia maktaba ziwe na skulini au maeneo mingine. Maktaba ni hazina pekee inayomtajirisha mwenye kuhitaji utajiri wa kitaaluma na kimaarifa, kwani mtumiaji hapitwi na wakati, na hupata taarifa muhimu juu ya mambo mbali mbali. Kwa wanafunzi na walimu wao, maktaba imekuwa ni hazina yao ya thamani, kama alivyosema mtaalamu Marcus Tallus Cicore " if you have a garden and library you have everything you need " ukiwa na tafsiri   isiyorasmi kuwa, kama una bustani na maktaba basi tayari una kila kitu. KWANINI MAKTABA NI MUHIMU SKULINI? Ahmed Khamis Ahmed mwanafunzi wa kidato cha pili skuli ya Madrasatul-Ahbaab Kisauni Unguja anasema, maktaba kwake ni suluhisho la ufumb

WANAOKULA DAWA KWA KUJIKADIRIA WENYEWE WAJICHIMBIA KABURI TARATIBU

    NA MOZA SHAABAN, ZU@@@@ KILA siku mwanadamu amekuwa akihangaikia afya yake na ustawi wake. Kwa karne zilizopita, mwanadamu alitumia mimea, mboga mboga na wanyama, ili kuponya magonjwa na maradhi mbali mbali yaliokua yakimsibu. Kwa vile wakati haugandi, sayansi inayochunguza faida na athari za vitu vya kemikali, kwa matibabu au kuzuia magonjwa, kupunguza maumivu na nyenginezo ilizuka. Na hapa dawa mbali mbali ambazo ni muhimu kwa matumizi ya binaadamu, zilianza kutengenezwa hususan zile za kemikali, ili kurekebisha au kuboresha hali ya afya ya mtu. DAWA NI NINI ? Dawa za binaadamu ni kitu chochote, ambacho binaadamu anatumia kwa lengo la kutibu au kukinga maradhi yasishambulie kinga za mwili. Zinaweza kuwa katika aina tofauti, kama vile vidonge, sindano, matone, creams au loshan pamoja na za unga unga. Kwa mfano, dawa za antibiotics hutumiwa kutibu maambukizi ya bakteria, za antiviras hutumiwa kutibu maambukizi ya virusi, na dawa za analgesic hutumiwa kupunguza m

WANAWAKE WALIMA MWANI PEMBA WADADAVUA MACHUNGU, SERIKALI YAJA NA NEEMA KWAO

     NA ABUU BAKAR, ZU@@@@ MWANI ‘sea weeds’ ni aina ya zao, lenye mnasaba na kiumbe hai, kinachopatikana baharini pekee. Kwa uasili wake viumbe hawa, huota na kukua kwenye fukwe zenye asili ya mawe au mchanga mzito, nyasi za baharini na kwenye matumbawe.   Kwa karne mbili na nusu zilizopita, zao la mwani, halikubeba thamani yake, na lilionekana kama vile ni bustani ya habarini yenye lengo la kuwapendezesha viumbe kama samaki. Kwa kule kucheza cheza kwao, kufanya mazalio, nyumba, sehemu za mapunziko na chakula kwa baadhi ya viumbe. Ilionekana, kama vile mwani ni viumbe vinayoota na kufa kila baada ya muda, na hakuna aliyefikiria kuwa, iko siku zao hilo linaweza kuwa sehemu ya kukuza pato la mtu au taifa. Baada ya kuonekana kuwa na thamani, sasa wataalamu wanatueleza kuwa, ziko aina mbali mbali za mwani, ambazo hutofautiana kutoka ukanda mmoja wa bahari na mwingine. Kwa mfano Tanzania, kuna aina mbili kuu za mwani, ule unaoitwa “ Eucheuma denticulatum ” au kwa jina jingin

WANAKAMATI, WAHAMASISHAJI JAMII MRADI WA SWIL WAIBUA MJADALA MZITO KWA WANAWAKE NA UONGOZI

    NA NUSRA SHAABAN Wahamasishaji jamii(CBs) pamoja na wanakamati walio katika mradi wa Kuongeza Ushiriki wa Wanawake kwenye Masuala ya Uongozi na Demokrasia (SWIL), unaofadhiliwa na Ubalozi wa Norway nchini Tanzania, wameibua mjadala huo kufuatia kikao kilichoandaliwa na   Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA)   katika ukumbi wa Skuli ya Turkey   Mpendae Zanzibar. Kikao hicho, kimewapa fursa wanakamati hao pamoja na Wahamasishaji jamii   hao, kuwasilisha ripoti zao za ufuatiliaji wa changamoto za kijamii na utendaji kazi wao kuanzia mwezi Januari 2023 mpaka Juni 2023. Jumla ya ripoti kumi zimewasilishwa   na kuibua mijadala tofauti   inayohusu wanawake na uongozi. Miongoni mwa maeneo yaliyozua mjadala mkubwa ni suala la wanawake wanaotaka kugombea nafasi za uongozi kuambiwa vyeti vyao ni feki. Akielezea kwa undani juu ya changamoto hiyo, Bi Sabahi   Bakari Hassan, Mhamasishaji   jamii kutoka Wilaya ya Kati, alisema kwa wanawake waliopo Wilaya ya kati changamo

ELIMU YA AFYA YA UZAZI KWA VIZIWI IKO NJIA PANDA, WIZARA YASEMA NENO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KUANZIA mwaka 1983 hadi 1992, hatua mbali mbali zilichukuliwa, ikiwani pamoja na maamuzi ya mwisho ya Umoja wa Mataifa, kuitangaza Disemba 3 ya kila mwaka, kuwa siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu . Siku hiyo, pamoja na mambo mengine, kundi la watu wenye ulemavu hujadili, mafanikio na changamoto zao, zikiwemo za huduma za afya. Kisha serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliunda Mkakati wa Kitaifa wa Ujumuishi wa mwaka 2010 hadi 2015, na sera ya taifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004, ukitaja ulazima wa huduma za afya kwa watu wenye ulemavu. Ipo sera ya kitaifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2018 kwa upande wa Zanzibar, ambayo Ibara ya 20, inasisitiza uimarishwaji wa upatikanaji huduma bora na endelevu kwa kundi hilo. Serikali ilitunga sheria ya Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2010, ambapo ilikuja kuharakisha huduma bora na endelevu za afya kwao. Kwa Zanzibar, ilikuwa na sheria ya watu wenye ulemavu, nambari 9 ya mwaka