Skip to main content

Posts

Showing posts from October 22, 2023

UKUSANYAJI MAONI SERA YA MSAADA WA KISHERIA WATUA PEMBA

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WEMA ZANZIBAR YAPEWA RAI KUIMARISHA LISHE SKULINI

  ZANZIBAR Wizara ya Elimu imeombwa kuhamasisha na kutoa elimu ya kilimo cha mboga mboga mashuleni kwa lengo la kuboresha lishe bora kwa wanafunzi. Wakizungumza katika kaikao cha pamoja huko hoteli ya SEA CLIFF Mangapwani   kilichowashirikisha watendaji Sitini na tano kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kilichajadili mafanikio na changamoto zinazoikabili sekta ya kilimo hasa cha mboga mboga, VIUNGO na matunda na kutafuta ufumbuzi ili kuleta tija kwa jamii. Wamesema Wizara ya Elimu ya Zanzibar na Tanzania Bara washirikiane kwa pamoja kuongeza nguvu kutoa elimu kwa wanafunzi wa kulima kilimo cha bustani mashuleni kwa lengo la kuimarisha Afya zao kwa kupata lishe bora na kwa ajili ya   maisha yao ya baadae. Mapema Mratibu wa mradi wa Agriconnect Zanzibar Omar Abuubakar Muhammed amesema ipo haja kwa jamii kuhamasishwa juu ya ulaji wa lishe bora hususan kina baba ambao wanaongooza kupeleka majumbani kwao vyakula visivyozongatia lis

UWT TAIFA, WAMPA KONGOLE MBUNGE ASYA SHARIF PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania ‘UWT’ taifa Mery Pius Chatanda, amesema aina ya Mbunge wa viti maalum mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, katika kuwakomboa wanawake kiuchumi, ndio mfano unaofaa kuigwa, na wabunge wengine Tanzania. Alisema, Mbunge huyo ameendelea kutekeleza kwa vitendo maagizo ya UWT taifa, ya kuwakomboa wanawake kiuchumi, kufuatia kukabidhi mashine ya kuzalisha mikate na tosi na fedha taslim, kwa wanawake wa mkoa wake, yenye thamani ya shilingi million 10.5 Mwenyekiti huyo wa UWT taifa, aliyasema hayo leo Oktoba 25, 2023, Micheweni mara baada ya kukabidhi mashine hiyo, kuweke jiwe la msingi ofisi ya ushoni wa nguo na kukabidhi shilingi milioni 1, zilizotolewa na Mbunge huyo. Alieleza kuwa, anaamini kupitia uwekezaji wa Mbunge huyo, wanawake wa CCM mkoa wa kaskazini Pemba, watapiga hatua kubwa ya kimaendeleo, kupitia njia ya kujiinua kiuchumi. Alifahamisha kuwa, wakati umefika kwa wabunge wengine wa mikoa ya Tanzan

MRADI WA VIUNGO WALETA MAPINDUZI YA KIUCHUMI ZANZIBAR

  Na Nafda Hindi, Zanzibar @@@@ Uwepo wa mradi wa VIUNGO, mbogamboga na matunda   Zanzibar umesaidia wananchi   kujikita katika sekta ya   kilimo hali iliyoleta mapinduzi ya kiuchumi katika familia zao. Hayo yamebainishwa na wanufaika wa mradi huo mara baada ya kutembelewa na Kikosi Kazi cha ufundi kwa Taasisi zinazotekeleza mradi huo kwa   lengo la kugunduwa Mafanikio   pamoja na changamoto zinazowakabili wakulima na kuzitafutia ufumbuzi. Wamesena kuna mafanikio waliyoyapata kupitia kilimo ikiwemo kuimarisha Afya za familia kwa lishe bora kwa kula mboga mboga na kuongeza kipato kupitia mfumo wa biashara. Ali Shauri ni katibu wa uhirika wa kilimo hai kiitwacho TUMAINI LA KIJANI uliopo Chuini Zanzibar, amesema wao wanatengeneza bustani za nyumbani ambazo zinajumuisha mbogamgoga pamoja na mimea ya dawa lengo likiwa kukibadilisha kijiji kuwa   cha kijani na wananchi kurudi katika uasili wa kutumia dawa za mitishamba jambo linalotoweka kwa vizazi vijavyo. Amesema   sababu zilizow

KASORO ZA KISHERIA ZAWAWEKA NJIA PANDA WATU WENYE ULEMAVU KUPATA HAKI ZAO

  HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ KATIBA ya Zanzibar ya 1984 kifungu 11 (1) imeeleza kuwa binadamu wote ni huru, na wote ni sawa na kila mtu anastahiki heshima ya kutambuliwa   na kuthaminiwa utu wake. Ikafafanuliwa tena kifungu cha 12 (1) kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria   na wanayo haki   bila ya ubaguzi   wowote , kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria. Katiba ya Jamuhuri ya Muungano ibara ya 12 (1) nayo imeelezea kuwa binadamu wote huzaliwa huru na wote ni sawa, na kila mtu anastahiki heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake. Tena kwenye Ibara ya 13 (4) ikaweka marufuku kwa mtu yoyote kutobaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji   wa kazi au shughuli yoyote ya nchi. Kimataifa upo Mkataba wa haki za watu wenye ulemavu   katika ibara ya 5, imeeleza kutokuwepo ubaguzi, na kwamba watu wote ni sawa mbele ya sheria.   Mkataba huo pia unapinga aina zote za ubaguzi zilizojengeka katika misingi ya ule

KATIBU MKUU ABEIDA AWAPA USIA NZITO WATOTO WA KIKE WENYE ULEMAVU

  Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Abeida Rashid Abdallah   amewataka Watoto wakike wenye ulemavu kutoona hali hiyo kwamba ni kikwazo cha kutosoma  na kukatisha  ndoto zao za Maisha. Akizungumza katika uzinduzi wa vyoo rafiki vya Watoto wa kike wenye ulemavu uliyofanyika leo katika skuli ya Sekondari ya Jangwani Dar Es Salaam, hafla hiyo imeandaliwa na Taasisi ya Maisha ya Amani kwa watu wenye ulemavu, amesema anaelewa changamoto zinazowakabili wasichana hao lakini hawatakiwi kukataa tamaa katika kutafuta elimu ili wawe viongozi wa baadae. Amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zinazungumza masuala ya watu wenye ulemavu kwenye vyombo vya maamuzi ili kuhakikisha watu wenye ulemavu hawajaachwa nyuma. Amesema Tanzania ni nchi moja wapo  ambayo inatekeleza mingozo mbali mbali inazungumzia  masuala ya watu wenye ulemavu ikiwemo  UN Covection on the right of People with disability  pia kunasheria  ya Tanzania Bar

KAMATI NGAZI YA SHEHIA ZAPEWA NENO NA PEGAO

  NA MARYAM NASSOR, PEMBA@@@@                           KAMATI zilizomo kwenye shehia zimetakiwa kushuka kwa wananchi na kuibua matatizo    yanayowakabili ili kuyapatia ufumbuzi unaofaa. Kauli hiyo, imetolewa na Mkurugenzi wa Asasi za Kiraia inayoshughulika na Mazingira, Utetezi wa Kijinsia Pemba (PEGAO) Hafidh Abdi Said katika mafunzo ya kuwapatia uwezo wajumbe wa Kamati hizo kutoka wilaya nne kisiwani Pemba. Alisema, iwapo kamati hizo zilizoundwa zitashuka   chini kwenye jamii kutafuta matatizo yanayowakabili wananchi na kushirikiana na viongozi kuzitatua, shida nyingi zitapungua. ‘’Kamati hizi zinatakiwa kuwa karibu na wananchi ili kuibua changamoto zinazoikumba jamii na kuzifikisha kwa viongozi husika kupatiwa ufumbuzi,’’ alisema. Aidha alisema kuwa, Serikali haiwezi kujua yote yanayoikumba jamii, hivyo watakapoyaibua na kuyapeleka kwa viongozi yatafanyiwa kazi kwa haraka. Nae, muwezeshaji katika mafunzo hayo Habibu Ali Khamis alisema, mpango wa kuchochea maendeleo kati

USHIRIKA MWANZO MGUMU FURAHA, TUNDA ADHIMU LA MRADI WA KIJALUBA PEMBA

  NA HAJI NASSSOR, PEMBA@@@@ SHERIA ya watu wenye Ulemavu Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (e) kimeweka wazi, haki ya watu wenye ulemavu, kujumuishwa kwenye harakati za uchumi. Ikaelezwa kuwa, mtu mwenye ulemavu ana haki ya kujitegemea na kujumuishwa katika shughuli za kijamii, kiuchumi na siasa. Kifungu chingine ni kile cha 30, kinachotoa wajibu wa kila mmoja, kulinda na kutetea haki za watu wenye ulemavu, zikiwemo cha kiuchumi. Hata kifungu cha 31, kimepiga marufuku, mtu yeyote kumbagua mtu mwenye ulemavu, kwa namna yoyote ile, tena kwa sababu ya ulemavu wake. Kwenye kifungu cha 42 cha sheria hiyo, kimekataa kumficha mtu mwenye ulemavu, kwa lengo la kumzuia asishiriki katika moja ya haki zake, zikiwemo za kiuchumi. Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu, Ibara ya 27, ikasisitiza nchi zilizoridhia mkataba huo, lazima ziweke mazingira sawa na wasiokuwa na ulemavu, katika ajira na kujiajiri. Haya yalikuja kulindwa na Katiba ya Zanzibar ya mwaka