NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ MSAIDIZI shehia ya Pandani wilaya ya Wete, Inspekta wa Polisi Khalfan Ali Ussi, amesema, ushirikishwaji wa jamii katika dhana ya ulinzi shirikishi, kutasaidia vijana kujitambua na kuishi kwa kuzingatia madili katika jamii. Aliyasema hayo mara baada ya kukamilika kwa bonanza la michezo, lilifanyika katika uwanja wa mpira katika kambi ya ‘FFU’ Finya wilaya Wete. Alisema vijana ndio wahanga wakubwa katika jamii kwenye matokeo mbali mbali ya uhalifu, hivyo wanapaswa kupewa elimu itakayowawezesha kujitambua na kuacha matendo yaliyokinyume na maadili ya jamii. Alieleza kuwa, kundi hilo nalo ni muhimu mno katika jamii ya leo na kesho, hivyo lazimalitazamwe kwa jicho pan ana kukua wakiwa na maadili mema. "Mabonanza kama haya yakiendelea kufanyika yatawasaidia wao, kuhamisha akili yao katika matendo ya kihalifu na kushiriki katika michezo, ambayo tija yake ni kubwa,’’alifafanua. Aidha aliwasisitiza vij...