Skip to main content

Posts

Showing posts from July 6, 2025

MKAGUZI WA POLISI SHEHIA YA PANDANI, AWAASA VIJANA KUJITENGA NA JINAI

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ MSAIDIZI shehia ya Pandani wilaya ya Wete, Inspekta wa Polisi Khalfan Ali Ussi, amesema, ushirikishwaji wa jamii katika dhana ya ulinzi shirikishi, kutasaidia vijana kujitambua na kuishi kwa kuzingatia madili katika jamii.   Aliyasema hayo mara baada ya kukamilika kwa bonanza la michezo, lilifanyika katika uwanja wa mpira katika kambi ya ‘FFU’ Finya wilaya Wete.   Alisema vijana ndio wahanga wakubwa katika jamii kwenye matokeo mbali mbali ya uhalifu, hivyo wanapaswa kupewa elimu itakayowawezesha kujitambua na kuacha matendo yaliyokinyume na maadili ya jamii.   Alieleza kuwa, kundi hilo nalo ni muhimu mno katika jamii ya leo na kesho, hivyo lazimalitazamwe kwa jicho pan ana kukua wakiwa na maadili mema.   "Mabonanza kama haya yakiendelea kufanyika yatawasaidia wao, kuhamisha akili yao katika matendo ya kihalifu na kushiriki katika michezo, ambayo tija yake ni kubwa,’’alifafanua.   Aidha aliwasisitiza vij...

SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR BADO NI KIZUNGUZUNGU

NA SITI ALI, ZANZIBAR@@@@ “Sheria ni msingi wa haki amani na maendeleo kwa kila nchi “Hayo si maneno yangu bali yalikuwa ni  maneno ya Raisi wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alipokuwa akizindua toleo jipya la juzuu za sheria mwezi  Aprili ,2025 jijini Dar es salaam. Anasema, bila ya sheria kuwa wazi uhakika wa ulinzi wa haki za raia unatoweka au unakuwa hauna uhakika na kusababisha uvunyifu wa amani.    Wandishi wa Habari Zanzibar wamekuwa wakidai sheria nzuri na rafiki ya habari bila ya mafanikio yoyote.Kutokana na kutumia sheria ya zamaani na iliyopitwa na wakati  iliyotungwa tokea miaka ya 1988 ambayo kwa sasa ni kikwazo kwa wandishi wa habari. Akizungumzia kuhusu sheria hiyo, mwandishi nguli wa habari visiwani Zanzibar, Salma Lusangi anasema ni muhimu kwa sasa sheria hiyo ibadilishwe ili iendane na wakati na kukidhi matakwa ya wakati husika. “Kwa kipindi kirefu tumekuwa tukifanya uchechemuzi wa sheria mbili kuu yaani sheria ya Wakala wa...

KUKUU KANGANI WAASWA KUJIEPUSHA NA WIZI WA KARAFUU

    BAKAR KHAMIS, PEMBA@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, wameaswa kuacha tabia ya wizi wa zao la karafuu, kwani kufanya hivyo pia wanaweza kuingizwa kwenye vitendo vya ukatili na udhalilishaji. Hayo yameelezwa na Mkaguzi wa Polisi Inspekta Hamad Ali Faki, kwenye kikao cha kuimarisha maadili ndani ya jamii, wakati akizungumza na wananchi wa shehia ya Kukuu Kangani wilaya ya Mkoani.   Alisema wapo baadhi wanajamii, wamekuwa na tabia ya kukwapua karafuu za wenzao wanapokuwa shambani, jambo ambalo linaweza kusababisha madhara zaidi, ikiwemo udhalilishaji.   Alieleza kuwa, zipo kesi kadhaa kila unapofika msimu wa uchumaji wa zao karafuu, hujitokeza zikiambatana na wizi wa karafuu.   "Ndugu zangu wanajamii, niwasihi sana kujiepusha na dhulma ya wizi wa karafuu, maana ndio chanzo cha udhalilishaji, ikiwemo watoto kupewa mimba, kulawitiwa na wengine kuhujumiwa kwa kipgo,"alifafanua.   Katika hatua nyingine, aliwakumbusha wazazi na walezi, kutowaac...

‘WEPO’ YAWAFIKIA WANANCHI 473 KAMBI YA MSAADA WA KISHERIA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI 473, kati yao wanawake 295 na wanaume 178, wa shehia za Kigongoni na Kiuyu Minungwini, wamefikiwa na elimu, ushauri na msaada wa kisheria, ikiwemo utaratibu wa upatikanaji cheti cha kuzaliwa, kwenye kambi ya msaada wa kisheria, iliyowekwa na Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete ‘WEPO’. Kambi hiyo ya siku moja, iliyofanyika leo Julai 7, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 9:30 jioni, wengi wa wananchi waliofika, walikuwa na malalamiko ya kukosa vyeti vya kuzaliwa. Ilifhamika kuwa, wingine ni wanaolalamikia kukosa vitambulisho vya mzanzibari mkaazi pamoja na vile ya taifa. Akizungumza na waandishi wa habari, Msaidizi wa sheria kutoka ‘WEPO’, Siti Faki Ali, alisema kambi hiyo imewasaidia kuwapa mwanga, wa aina ya changamoto iliomo ndani ya jamii. Alisema, kambi hiyo imewaamsha kwamba, kazi ya kuwaelimisha wananchi kupitia wasaidizi wa sheria, inahitaji kuongezwa nguvu, kwani wapo ambao hawajui hata utaratibu wa kupata nyaraka hizo ...

WATIA NIA CCM : 'MSIJIPITISHE PITISHE KWA WAJUMBE TULIENI MAJUMBANI'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ CHAMA cha Mapinduzi CCM mkoa wa kusini Pemba, kimepiga marufuku kwa watia wa nafasi mbali mbali, kuacha kujipotisha pitisha kwa wajumbe, na kuanza kampeni za chini kwa chini, kwani wakati wake haujafika.   Akizungumza na mwandishi wa habari katibu wa CCM mkoani humo, Kajoro Vyohoroka, alisema huu sio wakati kwa watia nia kujipitisha karibu na makaazi ya wajumbe na kuanza kampeni.   Alisema, CCM inaomfumo mzuri wa kidemokrasia wa kuwapata wajumbe watatu, ambao ndio watashushwa chini kwa ajili ya kupigiwa kura, na sio sasa kuanza kufanya jambo lolote.   Alieleza kuwa, ni marufuku kwa sasa kwa watia nia hao, kufanya jambo lolote linaloashiria kampeni ama kuingilia utaratibu wa vikao vya chama, na badala yake wawe watulivu majumbani mwao.   ‘’Ni kweli kuwa, hatua ya kwanza ya kuwapata wagombea wetu kwenye uchaguzi mkuu, umeshakamilika hivyo, watia wastahamili waanze kishindo cha kuwasilimu wajumbe, huu wakati wake bado,’...

'WEPO' KUENDESHA KAMBI YA MSAADA WA KISHERIA KIGONGONI, KIUYU MINUNGWINI ASUBUHI HII

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JUMUIYA ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete Pemba ‘WEPO’ asubuhi hii, inatarajia kuendesha kambi ya siku moja, ya msaada wa kisheria kwa wananchi wa shehia za Kigongoni na Kiuyu Minunwgini wilayani humo, bila ya malipo. Kambi hiyo, ambayo inatarajiwa kuwakusanya zaidi ya wananchi 500 wa shehia hizo, ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa kupambana na ukatili na udhalilishaji, chini ya ufadhili wa shirika la UNDP. Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Mratibu wa mradi huo, Rashid Hassan Mshamata, alisema kambi hiyo itawahusisha wataalamu wa masuala ya ardhi, mahakama, ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka, ofisi ya Mwanasheria mkuu. Alieleza kuwa, wataalam wingine watakaokuwepo kwenye kambi hiyo ni Jeshi la Polisi, dawati pamoja na wasaidizi wa sheria, kutoka Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete Pemba ‘WEPO’. Aliwataka wananchi wa shehia hizo na nyingine, kufika kwenye kambi hiyo ya siku moja, ili kuwasilisha matatizo yao ya kisheria...