Skip to main content

Posts

Showing posts from October 15, 2023

MCHAKATO UKUSANYAJI MAONI MAREKEBISHO SHERIA YA MTOTO WAANZA

  Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Siti Abass Ali amesema Idara hiyo ipo katika mchakato wa kukusanya maoni kutoka kwa wadau mbali kwa ajili ya kuifanyia maboresho sheria ya Mtoto namba sita (6) ya mwaka 2011 ili iendane na wakati uliyopo.   Akizungumza katika kikao cha ukusanyaji wa maoni kilichowashirikisha   wadau mbali mbali wakiwemo viongozi wa dini, wanasheria, Jeshi la Polisi, n.k   katika ukumbi wa Skuli ya Kidonge Chekundu Unguja, jana alisema kutokana na vitendo vinavyojitokeza katika jamii,ikiwemo ajira za utotoni hivyo, idara hiyo imelazimika kuipitia sheria hiyo nakuja na maamuzi ya kuifanyia maboresha ili iendane na wakati . “Kwa kweli Sheria hiyo   imetusaidia sana na inaenaendelea kutusaidia, imezungumza umuhimu wa mtoto kupata haki zake za msingi ikiwemo haki ya kupata elimu, matibabu, chakula, malazi, malezi, pia imezungumzia jinsi gani mtoto ataepukana na masauali ya udhalilishaji lakini baada ya kuipitia sheria hiyo tumeona bora

MAOFISA WIZARA YA AFYA PEMBA ROHO KWATU KUFANYA KAZI NA WAANDISHI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAOFISA wa wizara ya Afya Pemba, wamesema sasa wako tayari kuzidisha ushirikiano kati yao na vyombo vya habari, kwa ajili ya kuwapa taarifa wananchi, juu ya shughuli mbali mbali zikiwemo za haki ya afya ya uzazi. Walisema, waandishi wa habari, ndio wasemaji wa wasio kuwa na suati, hivyo suala la kuongeza ushirikiano, kwa hilo wako tayari wakati wowote na kwa jambo lolote. Wakizungumza kwenye mkutano wa ufungaji wa mradi wa Haki ya afya ya uzazi, uliofanyikwa ofisi ya Chama cha waandishi wa Habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, walisema ni vyema, waandishi wakawafika wanapowahitaji kwa kutengena Habari mbali mbali. Walisema kupitia mradi huo, waandishi wa Habari walisaidia mno kuharakisha upatikanaji huduma, kama za afya ya mama na mtoto,   huduma za kuchuunguza afya hasa kwa virusi vya Ukimwi, jambo ambalo limewasaidia wananchi Daktari wa wilaya ya Chake chake ‘DMO’ Sharif Hamad Khatib, alisema kwa mfano suala la kukatika kwa hu

PEGAO, TAMWA YATOA RAI KUEPUKA VYETI 'FEK'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAKALA wa usajili na matukio ya kijamii Zanzibar, wilaya ya Chake chake, imekumbushwa kuwatumia waandishi wa habari na wadau wengine wa haki za binaadamu, ili kufikia jamii kwa lengo la kuielimisha na kuepukana na vyeti na vitambulisho vyenye mgogoro miongoni mwao. Wito huo ulitolewa leo Oktoba 17, 2023 na Mkurugenzi wa mradi wa kuihamasisha jamii kudai haki zao za uongozi, siasa na demokrasia ‘SWIL’ kutoka Jumuiaya ya Utetezi wa Mazingira na Jinsia ‘PEGAO’ Hafidh Abdi Said, kwenye mkutano wa kuwasilisha kero, zilizoibuliwa na wahamasishaji, uliofanyika ofisi ya TAMWA Mkanjuni Chake chake. Alisema kuwa, kutokana na jamii kutokuwa na ufahamu wa kutosha juu ya vielelezo hivyo, kumepelekea kuwepo kwa tatizo kubwa ambalo linahitaji kufanyiwa kazi, ili liweze kuondokana nav yeti bandia na vitambulisho vye mgogoro. Alieleza kuwa, tatizo hilo limekuwa ni la muda mrefu katika jamii, hivyo ni wakati sasa Wakala wa usahili na matukio ya kijamii kufanyaka kazi

WIZARA YA AFYA YAPEWA NENO KUFANYAKAZI NA WAANDISHI WA HABARI

  Na Nafda Hindi@@@@   Wizara ya Afya imeombwa kutoa mashirikiano mazuri kwa waandishi wa habari kwa lengo la kuleta mabadiliko katika jamii.   Akizungumza wakati wa uwasilishaji ripoti  ya elimu ya Afya ya Uzazi kwa wasichana na wanawake wa mjini na vijijini katika ukumbi wa Kificho Mwanakwerekwe Mkurugenzi wa chama cha waandishi wahabari wanawake Tanzania Zanzibar Dk. Mzuri Issa amesema watendaji wa Wizara husika kuepuka tabia ya usiri wa kutotoa taarifa muhimu zinazogusa maisha ya watu.   “ Kuna usiri wa taarifa kwa baadhi ya watendaji hivyo tunaiomba Wizara ya Afya iendelee kutoa mashirikiano mazuri kwa waandhishi wahabari kwa sababu masuala ya kinchi nay a kijamii ni lazima yasikike kupitia vyombo vya habari,’ Dk Mzuri Issa, Mkurugenzi TAMWA,ZNZ.   Dk Mzuri amesema  masuàla yànayohusu nchi pàmoja na jamii lazima yasikike kupitia vyombo vya habari kwa wananchi kupaza sauti zao   “ Ni haki ya kila mtu kupata taarifa na uhuru wa kujieleza na katiba zote mbili zi