Skip to main content

Posts

Showing posts from March 31, 2024

TUME YA KUREKEBISHA SHERIA: MIFUMO YA SHERIA IWE JUMUISHI KWA WATU WOTE'

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TUME ya Kurekebisha sheria Zanzibar, imesema itaangalia kwa kina, juu ya mifumo ya sheria, ili isiwaweke nje ya utaratibu watu wenye ulemavu, katika mapambano dhidi ya udhalilishaji wa wanawake na watoto. Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu wa Tume hiyo, Mussa Kombo, wakati akikikfungua kikao kazi, cha kupokea maoni ya wadau wa haki jinai, kuelekea marekebisho ya Sheria ya Adhabu nambari nambari 6 ya mwaka 2018 na ile ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai nambari 7 ya mwaka 2018, kilichofanyika ukumbi wa wizara ya Fedha Gombani. Alisema, ni kweli watu wenye ulemavu wanaonekana kuwekwa nyuma kwenye mifumo ya haki jinai, kuanzia kuchukuliwa maelezo vituo vya Polisi, ushahidi mahakamani, kujitetea jambo ambalo, linaweza kuwa chanzo cha kuwakosesha haki zao. Alieleza kuwa, kupitia marekebisho hayo na kwa kuzingatia maoni yaliotolewa, watahakikisha kundi hilo sasa linawekewa kifungu maalum ndani ya sheria hizo, ili iwe sababu ya kuunga mkono mapambano hayo

WAZAZI WATAKIWA KUHOJI VYANZO VYA VIPATO KWA WATOTO WAO

IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA WAZAZI na walezi wa shehia ya Pandani Wilaya ya Wete Pemba wameshauriwa kujenga tabia ya kuhoji vyanzo vya vipato vya watoto wao, ili kuiepusha jamii kuingia katika vitendo vya kihalifu. Akizungumza na Kamati ya wazee wa kijiji cha Kwamwewe wakati wa muendelezo wa kutoa elimu ya kudhibiti vitendo vya kihalifu katika jamii, Mkaguzi wa shehia hiyo Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi alisema, kuna baadhi ya wazazi hawawezi kuwauliza kitu watoto wao, jambo ambalo sio jema. Alisema kuwa, ni vyema kila mzazi kujua tabia ya mtoto wake na kuhoji vitu au vipato walivyonavyo vinatoka kwenye vyanzo gani, hiyo itasaidia kuondoa vitendo vya uhalifu katika jamii kwani kila ambae anajihusisha na tabia mbaya ataweza kuziacha kwa haraka. "Tusiwagope watoto wetu, kujua vyanzo vyao vya mapato itatusaidia kujua wanafanya kazi gani na pia wenyewe watatafuta kazi za halali kwa sababu watajua tu kama wataulizwa na wazazi wao, hivyo naamin

DC WETE AWAPONGEZA WANANCHI KUDHIBITI VITENDO VIOVU

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA MKUU wa Wilaya ya Wete Pemba Dk. Hamad Omar Bakar amewapongeza wananchi wa Shehia ya Mlindo kwa uthubutu wao wa kujitolea katika kupambana na vitendo viovu ikiwemo udhalilishaji, wizi wa mazao na mifugo. Akikabidhi vitambulisho kwa vijana wa ulinzi shirikishi (Polisi Jamii) kwenye mkutano uliofanyika katika shehia hiyo, Mkuu huyo aliwataka wanakikundi cha Polisi Jamii kuvitumia vitambulisho hivyo kama ilivyokusudiwa kwa lengo ni kudhibiti vitendo viovu. Alisema kuwa, wananchi hao wamefanya jambo zuri la kujitolea kwa kuanzisha kikundi cha kupambana na vitendo viovu, hivyo ni vyema wakaendelea kushirikiana kuhakikisha wanavidhibiti na shehia I abaki katika hali salama. "Kuna vitendo vya udhalilishaji na wizi ambavyo vinawaliza wanajamii kila kona, lakini naamini kwa kikundi hiki mlichokiunda basi mtafanikiwa kiyadhibiti, nawapongeza sana," alisema Mkuu huyo. Aidha aliwataka wanajamii kuacha tabia ya kusuluhisha kesi za udhalilishaji majumbani

'ZITUMIENI KIVITENDO SIKU ZA MWEZI MTUKUFU ZILIZOBAKIA MTAPA NEEMA’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAUMINI wa dini ya kiislamu kisiwani Pemba, wametakiwa kuzitumia kimipango, siku zilizobakia za mwezi mtukufu wa Ramadhan, ili kujikurubisha kwa Muumba na kupata fadhila zake. Hayo yalielezwa na Msaidizi wa Katibu wa ofisi ya Mufti Zanzibar, ofisi ya Pemba Sheikh Said Ahmad Mohamed, wakati alipokuwa akitoa shukran kwa waumini, walioshiriki sawala wa Ijumaa, na Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, Machomanne Chake chake Pemba. Alisema, sio sahihi kuwa mwezi mtukufu wa Ramadhan umekwisha, bali siku zilizobakia zinaweza kumkomboa muumini na kupata malipo makubwa, iwapo atajipangia ratiba nzuri. Alieleza kuwa, kwa fadhali za mwezi huu, muumini hawezi kupoteza jambo hata kwa siku moja, ikiwa ataamua kujikurubisha kwa vitendo Muumba, kama wanavyofanya baadhi yao. Sheikh Said alieleza kuwa, siku moja katika mwezi mtukufu wa Ramadhan inathamani zaidi ya mara moja, kuliko siku nyingine, hivyo sio sahihi kuwa Ramadhan imekwisha na hakuna muda wa kufany