Skip to main content

Posts

Showing posts from February 25, 2024

''TUNATAKA KUONA WANAWAKE WANAJITEGEMEA' WAZIRI PEMBE

  Salha ZJMMC@@@@ Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mh e . Riziki Pembe Juma amesema S erikali imeamua kuwawezesha wanawake jasiri ili kuwawezesha kiuchumi na kuweza kujitegemea weneyewe ili kuondokana na hali ya utegemezi katika jamii. Ame yasema hayo wakati akifungua mafunzo ya wanawake shupavu wa amali ya Zanzibar yaliyofanyika B weni katika Chuo cha Ufundi Karume Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Magharibi , Unguja. Amesema kutoa mafunzo kwa wanawake wenye ujasiri kunaongeza uwezo zaidi wa kuweza kuzalisha bidhaa zao zenye ubora. Pia ametoa wito kwa wataalamu jasiri wanaopatiwa mafunzo ya kuwa walimu kwa wanawake wengine ambao hawajapata fursa ili kuwawezesha wanawake wengi kuweza kujiajiri na kuondokana na utegemezi katika familia zao. Hata hivyo ametoa wito kwa wanawake kuwapenda, kuwaongoza, na kuwalinda watoto wote ili kuwasaidia kuepukana na vitengo vya   ukatili wa kijinsia na udhalilishaji . Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Kazi n

TAMWA YALIPONGEZA JESHI LA POLISI KUKEMEA UVUNJIFU WA MAADILI ZAZNAIBAR

  Chama cha waandishi wahabari wanawake Tanzania Zanzibar TAMWA,ZNZ kinalipongeza jeshi la Polisi kwa kuchukuwa hatua za haraka kushughulikia suala la uvunjaji wa maadili lililofanywa hivi karibuni na kusambaa katika mitandao ya kijamii. Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Mkurugenzi wa chama cha waandishi wahabari wanawake Tanzania Zanzibar, TAMWA ZNZ Dk Mzuri Issa amesema kutokana na tukio lilotokea hivi karibuni na kutoa taswira mbaya ya kimaadili, kinidhamu na Udhalilishaji nchini, hivyo TAMWA imeliomba Jeshi la Polisi kuwakamata wote waliohusika na Sheria kuchukuwa mkondo wake. Amesema TAMWA ZNZ inaomba hatua kali zichukuliwe dhidi ya wahusika kwa mujibu wa sheria zilizopo ili kuwa funzo kwa wengine wanaotaka kujaribu na hivyo kulinda mila, silka na maadili ambazo ni moja kati ya tunu muhimu za Zanzibar. “Ni dhahiri kwamba vitendo hivyo kamwe havikubaliki na vinaweza kuleta athari na madhara makubwa ya hivi sasa na baadae katika kuimarisha yetu na   vizazi vya leo na hapo

WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII ZANZIBAR KUSHIRIKI MKUTANO WA 'MMMAM'

  Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inarajiwa kuwa mdau katika Mkutano wa Kimataifa wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (MMMAM) unayotarajiwa kufanyika Mwezi Machi mwaka huu , jijini Dar es Salaam, Tanzania. Akizungumza ofisini kwake Kinazini Unguja na Viongozi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum bi Abeida Rashid Abdallah amesema Wizara hiyo imefanya jambo jema kuishirikisha Wizara yake kuwa mdau katika mkutano huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 11-14 Machi 2024 Katika ukumbi   wa Kimataifa ya Mwalimu Julius Nyerere. Amesema ni wazi kwamba S erikali zote mbili, Serikali ya M apinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Jamhuri ya Mungano wa Tanzania (SMT) kwa pamoja zinalengo la kuisaidia jamii katika M alezi, M akuzi, na Maendeleo ya Mtoto . Kwani mtoto ndio tegemeo la taifa la kesho. Aidha bi Abeida ameshauri katika mkutano huo ni vyema kuwashirikisha na Wizara zingine za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ikiwemo Wizara Afya,

HIZI HAPA CHANAGAMOTO ZINAZOWAKWAZA WANAWAKE KUTOKUWA VIONGOZI MAJIMBONI

  NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR Hali ya wanawake, ikiwa pamoja na kushika nafasi za uongozi zinatafuatiana duniani kutokana na sababu nyingi. Miongoni mwa hizi sababu ni sera za nchi hizo, sheria, mila, tamaduni na dhana potofu ya kumchukilia mwanamke kama mtu ambaye haki zake kama binaadamu hazistahili kuwa sawa na zile za mwanamume. Matokeo yake ni kuona wanawake wengi wanakosa haki zao nyingi, ikiwa pamoja na za elimu, urithi , kushika nafasi za uongozi na kuwa na sauti inayosikika na kuheshimika katka kufanya maamuzi. Ripoti ya mwaka 2018 inayohusu uwiano wa kijinsia ulimwenguni imeweka picha halisi ya haki za wanawake katika siasa, uchumi na elimu ili kuutanabahisha ulimwengu kasoro ziliopo na kuelezea umuhimu wa kufanyika marekebisho. Hivi sasa ziaonekana zinafanyika jitihada mbalimbali kurekebisha dosari hizi ili kuhakikisha mwanamke, anakuwa ni sehemu ya uongozi, ikiwemo kwenye mambo ya kisiasa kwa vile huko ndiko anapofanyika maamuzi muhimu ya kimaisha, kisiasa na kiuch

SMZ yakumbushwa kuzifanyia marekebisho Sheria zinazominya uhuru wa habari Zanzibar

NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Znz Dk Mzuri Issa amesema kuwepo kwa uhuru wa habari na kujieleza ni haki ya msingi ya binadamu ambayo itachochea kuleta maendeleo. Dk Mzuri ameyasema hayo wakati akifunguwa mkutano wa uchambuzi wa sheria zinazokwaza uhuru wa habari Zanzibar uliowashirikisha wadau wa masuala ya habari na waandishi wahabari uliofanyika katika Ofisi za Tamwa Tunguu, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja. Amesema suala la kupata habari kwa Zanzibar limeanzia tokea enzi za karne zilizopita, kinachorudisha nyuma kwa sasa kutopata habari ni kuwepo sheria zisizo rafiki kwa waandishi wahabari na hata wananchi. “Zanzibar ni kitovu cha Utamaduni wakupata habari, na hata waandishi wahabari wanawake walianzia Zanzibar enzi hizo,’’ Dk Mzuri Issa. Akiwasilisha ripoti hiyo ya Uchambuzi wa sheria zinazokwaza uhuru wa habari Muhadhir kutoka Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZU) Said Suleiman amesema kuna baadhi ya sheria zimepitwa n