Skip to main content

Posts

Showing posts from April 6, 2025

WAZIRI PEMBE ALIPA RAI 'IAA' KUFIKIA MALENGO YAO

  Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma amelitaka Baraza la Uongozi wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), kuongeza  jitihada katika usimamizi na kuhakikisha malengo ya chuo ya muda mrefu na muda mfupi yanafikiwa kama ilivyokusudiwa. Waziri Riziki ameyasema hayo katika hafla ya uzinduzi wa Baraza jipya la Uongozi wa Chuo hicho iliyofanyika katika Ukumbi wa IAA, Arusha. Amesema Chuo cha Uhasibu Arusha kimeamua kujitofautisha na vyuo vyengine kwa namna mbalimbali ikiwemo kuanzisha mitaala ya kipekee mfano mitaala ya uanagenzi (apprenticeship), kuanzisha mitaala inayoandaa wataalam wanaoweza kujiajiri na kuajiri wengine, kutengeneza miundombinu na mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishia kuendana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia. Hivyo ametoa rai kwa Baraza hilo kuhimiza juhudi za kuboresha ubora wa elimu inayotolewa na chuo, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mitaala itakayoanzishwa katika kipindi cha utekelezaji wa majukumu yao ili inaendel...

WIZARA KUZIDI KUSHIRIKIANA NA POLISI: PEMBE

  Na Muandishi wetu Zanzibar@@@@ Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (WMJJWW) Mhe Riziki Pembe Juma amesema Wizara hiyo inaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi ili kuona upelelezi wa kesi ya Mtuhumiwa Ramadhani Hamza Hussein (28) Mkaazi wa Tomomdo, Unguja anayetuhumiwa kwa kosa la kumdhalilisha mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 13 inafikishwa Mahakamani ili haki itendeke. Kauli hiyo ameitoa jana wakati akimkagua mtoto huyo aliyelazwa katika Hospitali ya Mkoa, Lumumba Zanzibar, baada ya kufanyiwa  vitendo vya udhalilishaji huko Jang'ombe Mjini Unguja na Mtuhuhumiwa Ramadhani Hamza Hussein. Waziri Riziki amesema tukio hilo limetokea tarehe mosi, Machi, mwaka huu,  na kuripotiwa  tarehe 31/03/2025 katika kituo cha Mkono kwa Mkono pamoja na kufanyiwa uchunguzi wa kitaalamu na hatimae kupewa PF3. Ametoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano wa kutosha katika kupiga vita vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia kwani hatua hiyo itasaidia kupunguza ...