Skip to main content

Posts

Showing posts from August 20, 2023

TAMWA- ZANZIBAR CHAWAJENGEA UWEZO WAANDISHI KUANDIKA HABARI ZENYE TIJA

  HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@  AFISA Mkuu wa Mawasiliano na Uchechemuzi kutoka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA- Zanzibar Sophia Ngalapi, amesema iwapo habari za kupinga udhalilishaji zitaandikwa na kufanyiwa ufuatiliaji (follow up) zitasaidia kupunguza vitendo hivyo nchini.   Akizungumza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari kisiwani Pemba, juu ya mbinu bora za kuandika habari za udhalilishaji, alisema habari hizo zimekuwa zikiandikwa kwa muda mrefu, ingawa imeonekana bado waandishi hawazifanyii ufuatiliaji.   Alisema kuwa, hali hiyo imebainika baada ya TAMWA kufanya utafiti kupitia vyombo vya habari, na kugunduwa kuwa zipo habari za udhalilishaji zilizoripotiwa, lakini hazina ufuatiliaji jambo ambalo, linarejesha nyuma juhudi za mapambano hayo.   "Utafiti mdogo wa miezi mitatu uliokusanya vyombo vya habari vya redio, magazeti na mitandao ya kijamii, lakini changamoto kubwa iliyoonekana, ni habari za udhalilishaji, kutofanyiwa uf

WANAWAKE WASHIKWE MKONO KUFIKIA MALENGO YAO

    Na Nafda Hindi, Zanzibar@@@@ JAMII imetakiwa kuwaunga mkono wanawake katika harakati wanazozifanya  za kuleta  maendeleo ili kufikia malengo waliyojiwekea. Hayo yalisemwa na muhadhiri wa kiislamu Visiwani Zanzibar, Ukhti Amina Salum Khalfan, wakati  akizungumza na baadhi ya wanawake katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kujitokeza kugombea nafasi za Uongozi, mafunzo ambayo yaliandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) huko Tunguu Wilaya ya Kati Unguja. Amesema wanawake wanahaki ya kushirikishwa katika harakati mbalimbali ikiwemo za kiuchumi, kijamii na kisiasa hivyo ni vyema wanapojitokeza katika maeneo hayo kuungwa mkono na kushirikishwa ipasavyo ili kuweza kufikia ndoto zao na kuleta maendeleo kupitia mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Amesema harakati za Uongozi kwa wanawake hazikuanza sasa na badala yake zilianza toka enzi za Mitume na  Mtume Muhammad ( S.A.W) ambapo alikuwa akiwapa elimu ya kujitambua na kuwapa haki zao ili kuona kama

MAAFISA KILIMO WAPEWA RAI

NA NAFDA HINID, ZANZIBAR@@@@ Maafisa kilimo wameshauriwa kutoa taarifa kamili kuhusu udongo bora wenye kukidhi viwango kwa lengo la kuzalisha mazao bora kwa wakulima. Kauli hjiyo imetolewa na   Mkuu wa Tathmini na Ufatiliaji kutoka mradi wa VIUNGO Ali Abdalla Mbarouk katika   kikao cha pamoja   kilichowashirikisha wadau wa mradi huo chenye lengo la kujadili mbinu bora na mikakati imara ya kuendeleza kilimo chenye tija kwa wakulima kilichofanyika jengo la Benki ya watu wa Zanzibar katika Ofisi za Mfuko wa Bima . Amesema ipo haja kwa Wizara ya Kilimo kufanya tathmini kwa wakulima kwa kila Wilaya kugunduwa changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi wa haraka ikiwemo kutokufahamu udongo sahihi kwa matumizi bora ya kiliomo. Mwenyekiti wa kamati ya Ushauri ya mradi wa Viungo (ZMAG) ambae pia ni Mkurugenzi Sera, Mipango na Kilimo Makame A. Makame amesema kwa sasa ipo haja kwa Zanzibar kuuza bidhaa zilizochakatwa nje ya nchi   badala ya mali ghafi kwa lengo la kuongeza thamani y

WANAFUNZI, WAALIMU SKULI YA UWELENI KUSAHAU SHIDA YA MAJI

  HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ WANAFUNZI 771 wakiwemo wanawake 354 na wanaume 417 pamoja na walimu skuli ya sekondari ya Uweleni wameondokana na huduma ya maji isiyokuwa ya uhakika, baada ya kukamilishiwa ndoto yao ya kuchimbiwa kisima. Kisima hicho chenye urefu wa mita 70 ambacho kitakuwa na uwezo wa kujaza 22,000 kwa saa mbili kimechimbwa na shirika la usaidizi wa moja kwa moja   Afrika ‘Direct Aid Association’. Kisima hicho pamoja na kuwanufaisha wanafunzi, tayari huduma hiyo imeshawanufaisha wanafunzi 768 wakiwemo 205 wa skuli ya maandalizi ya Uweleni na 563 wa madarasatul Nurudhalami pamoja na wanajamii wa shehia ya Uweleni. Akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa kisima hicho Msaidizi Mwalimu mkuu wa skuli hiyo Khamis Mohamed Ussi alisema, kuwepo kwa huduma hiyo ya kudumu skulini hapo, ni tunu haikuwepo kwa zaidi ya miaka 90 tokea kuanzishwa kwa skuli hiyo. Alisema skuli hiyo, tokea kuanzishwa kwake mwaka 1931 haikuwa na huduma ya uhakika ya maji, kutokana na kutegemea hu

WAHAMASISHAJI JAMII PEMBA WAONESHWA WALIPO WANAWAKE WA KUANDALIWA KIUONGOZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MWENYEKITI wa Bodi ya Jumuiya ya Utetezi wa Mazingira na Jinsia Pemba ‘PEGAO’ Alhajji-Amran Massoud Amran, amewashauri wahamasishaji jamii kudai haki zao za uongozi, demokrasia na siasa ‘Citizen bragged’ kisiwani Pemba, kuelekeza nguvu zao ngazi ya vyuo, ili kuwaibua wanawake wenye nia ya kugombea nafasi za uongozi. Alisema, wanafunzi wanawake ambao wanajitayarisha kuja kuitumikia jamii, wako katika skuli za sekondari na vyuo vikuu, hivyo ni vyema kwa wahamasishaji hao, sasa kuhamia katika eneo hilo kufanya uhamasishaji. Mwenyekiti huyo wa bodi, aliyasema hayo leo August 20, 2023 ukumbi wa mikutano wa Jumuiya ya ‘KUKHAWA’ wilaya ya Chake chake, wakati akizungumza na wahamasishaji hao, mara baada ya kuwasilisha utekelezaji wa shughuli zao, kwa kipindi cha miezi mitatu iliyopita. Alisema, wanawake walioko ngazi ya elimu ya sekondari na vyuo vikuu, ndio tegemeo kubwa kwa jamii, hivyo ikiwa watawezeshwa mapema, kuingia katika nafasi za uongozi, itakuwa