Skip to main content

Posts

Showing posts from May 7, 2023

AJALI ZA BODA BODA, TANZANIA ZAONGEZA IDADI YA MAYATIMA, WAJANE, VILEMA, VIFO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ PAMOJA na kukua kwa uchumi, uimarishaji wa miundombinu ya barabara na ongezeko kubwa la vyombo vya usafiri, imebainika kuwa, kama Jeshi la Polisi na wananchi hawakushirikiana, vifo vitokanavyo na ajali za Piki piki (boda boda) hazitopungua nchini . Imeonywa kuwa, kwa kuliachia jukumu la kupunguza ajali za piki piki Jeshi la Polisi pekee, haitokuwa dawa ya kupunguza ajali hizo, ambazo pia husababisha vifo na vilema. TAKWIMU ZA AJALI ZA PIKI PIKI Uchunguuzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi, umebaini kuwa, kwa mfano kwa mwaka 2019 hadi mwaka 2020 kwa Tanzania, kulikuwa na ajali za piki piki 1,133 zilizosababisha vifo 674 , sawa na majeruhi 948 . Imebainika kuwa, kati ya ajali hizo, Tanzania bara kuliripotiwa ajali 964, zilizosababisha vifo 573 na majeruhi 767 kwa miaka hiyo miwili. Wakati kwa Zanzibar, kuliripotiwa ajali 169 sawa na vifo 101 huku idadi ya majeruhi wakiwa ni 181 . Katika kipindi cha Januari hadi Disemba pekee kwa mwaka 20

RUZUKU YA TASAF KWA WALENGWA PEMBA YAGEUKA KAA LA MOTO , TASAF YATOA UFAFANUZI

  NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ MFUKO wa Maendeleo ya Jamii Tanzania ‘TASAF’ kupiti mpango wa kunusuru kaya maskini, umekua ni kama kivuli, wakati wa kiangazi eneo la jangwani. Mpango huu wa kunusuru kaya masikini, toka kuanza kwake nchini umeweza kusaidia wananchi wengi, waliokuwa kwenye jua kali la kimaisha, na sasa wamepata kuvuli. TASAF kupitia miradi yake mbali mbali ya maendeleo, imeweza kuwakomboa wananchi wengi kiuchumi, ambapo wengi wao wamekomboka kimaisha. Wananchi wa shehi ya Ving’ambwa kijiji cha Vikunguni ni moja kati ya wanufaika wa mpango huo, ambapo baadhi ya wanufaika hao wameanza kupata mafanikio makubwa kupitia miradi hiyo. Iko misemo mingi ya kiswahili ukiwemo mtaka cha mvunguni sharti ainame’, wengine wakasema ‘abebwae hujikaza’ mgagaa na upwa hali wali mkavu ikiwa na maana pana kwa mujibu wa jambo lenyewe. WALENGWA VIKUNGUNI CHAKE CHAKE Fatma Khamis Mbarouk mkaazi wa Vikunguni shehia ya Ng’ambwa Chake Chake, ni miongoni mwa wanufaika, anasema kwa s