Skip to main content

Posts

Showing posts from September 11, 2022

NURU FOUNDATION YASAIDIA WATOTO WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU

                   Na Mwandishi wetu OMKR                                                                            Mwenyekiti wa Nuru Foundation Mama Zainab Kombo Shaib ambae pia ni mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais amesema Jumuiya yao imeamua kujikita zaidi kumuangalia mtoto wa aina yeyote hasa yatima na anaeishi kwenye mazingira magumu Ameeeleza hayo wakati alipofanya ziara ya kuwatembelea watoto wenye vichwa maji na mgongo wazi katika kituo chao cha nyumba ya matumaini iliyopo eneo la Mwanakwerekwe ndani ya Wilaya ya Magharibi B. Mama Zainab amesema kumlea mtoto mwenye kichwa maji na mgongo wazi kunahitaji elimu kwa mzazi na walezi ili kufahamu namna ya kumlea hatimae nae mtoto akuwe katika mazingira mazuri yaliyo salama katika hali zote Ameahidi kuwa taasisi ya Nuru Foundation ina kila sababu kuona inawasaidia kielimu kwa kutafuta njia za kupata ufadhili na kupata vifaa visaidizi pamoja na kumuandaa kisaikolojia mama au familia yenye mtoto mwenye ulemavu wa aina hii ili waw

KILIMO CHA MPUNGA CHAWEZA KUTOSHELEZA KWA CHAKULA NCHINI IKIWA....

  NA HAJI NASSOR-PEMBA  +255777 870191 email: kakahaji2016@gmail.com WANANCHI wa Zanzibar 40, kati ya kila 100, wamejiajiri moja kwa moja kupitia sekta ya kilimo na vivyo hivyo 70 kati ya kila 100 wanategemea kilimo moja kwa moja kwenye maisha yao ya kila siku, kama ilivyothibitishwa ofisi ya Mtakwimu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 2016/2021 Ndio maana mwaka wa fedha 2016/2017 sekta hii ilichangia asilimia 25.7 ya pato la taifa na ilikua kwa asilimia 5.7 ikilinganishwa na asilimia 2.5 ya mwaka 2015/2016. Kutokana na umuhimu wa sekta hiyo, kwa uchumi wa nchi na ustawi wa wananchi, Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, ina dhima kubwa ya kuhakikisha inawawezesha wakulima wote ili kufikia malengo. Wizara hiyo lazima iweke mikakati maalum kwa ajili ya uzalishaji wa mpunga hapa Zanzibar, kwani ndicho chakula chenye kutumiwa na kupendwa zaidi na sehemu kubwa ya jamii ya Wazanzibari. Tunapozungumzia mpunga ambao unazalisha mchele wenye kutoa chakula kinachoitwa w

DYNAMITE FISHINGi: THREAT TO SUSTAINABLE BUE ECONOMY

                                                        By   HAJI MOHAMED .PEMBA-ZANZIBAR -TANZANIA Fishing is a legal money earning activity for many people around the world that sustains livelihood. It is practiced in the seas, oceans, lakes, ponds and rivers. However, human beings who are not satisfied with what they catch a day, have come up with what we call illegal fishing which is very destructive. There are many activities of illegal fishing in the world. Some of them are using cyanide, fishnets with small eyes and one of the most destructive is dynamite fishing or blast fishing. It is also known as bomb fishing. As Zanzibar is implementing a blue economy policy, the government needs to be alerted on dynamite fishing due to its destruction to the marine ecosystem as our country expects rapid development in the fishing industry. This article intends to show how blast fishing is dangerous for the sustainable fishing industry by taking an example of the Philippines

SMZ YATANGAAZA NAULI MPYA GARI YA ABIRIA

        TAARIFA YA MABADILIKO YA NAULI NA BEI ELEKEZI ZA VYOMBO VYA USAFIRI WA UMMA BARABARANI ZANZIBAR Ndugu Wananchi Asalam Alaykum Warahmatullah Wabarakatu Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa,   kutujaalia uhai na afya njema na kutuwezesha kuiona siku ya leo, Aidha napenda kuchukuwa fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa kuendelea kuiongoza nchi yetu ikiwa katika hali ya amani na utulivu unaowezesha wananchi kuendelea kufanya shughuli zao bila matatizo zikiwemo shughuli za Usafiri na Usafirishaji. Ndugu Wananchi, Baada ya kutoa shukurani hizo, Naomba sasa nitoe taarifa fupi juu ya mabadiliko ya nauli na bei elekezi za vyombo vya usafiri wa umma barabarani   Zanzibar ikiwemo Magari ya shamba, Daladala na Taxi. Ndugu Wananchi, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa ikichukua jitihada mbali mbali katika kudhibiti upandaji wa bei za mafuta na bei za nauli za vyombo vya kusafiri

KAMATI YA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI CHAKE CHAKE YAKOLEZWA 'SPEED'

                                                     NA HAJI NASSOR, PEMBA:::: AFISA Mipango wilaya ya Chake chake, Kassim Ali Omar amesema, bado juhudi zaidi zinahitajika kufanywa, na kamati ya kupambana na ukatili na udhalilishaji wilayani humo, ili kundi la wanawake na watoto, libaki salama na matendo hayo, kama yalivyo makundi mengine.   Hayo aliyasema leo Septemba 14, 2022 ukumbi wa TASAF mjini Chake chake, wakati akifungua kikao cha kamati hiyo, kwenye uwasilishaji wa ripoti kwa taasisi zinazounda kamati hiyo, ikiwemo ya kituo cha Mkono kwa mkono, viongozi wa dini, shirika la SOS na wizara ya elimu na Mafunzo ya amali.   Alieleza kuwa, wananchi wa wilaya ya Chake chake wakiwemo wanawake na watoto, wanaingalia kamati hiyo, ili kutafuta mwarubaini wa matendo ya udhalilishaji yanayojitokeza siku hadi siku, hivyo lazima mkazo uwekwe.   ‘’’Bado jukumu la kipekee litakuwa kwa kamati ya kupambana na ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto ya wilaya, hivyo lazima ngu