Skip to main content

Posts

Showing posts from November 27, 2022

MZEE 'SODA' MIAKA 76, ATUNDIKWA MIAKA 10 CHUO CHA MAFUNZO KWA UBAKAJI PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: HATIMAE mahakama maalum ya kupambana na makosa ya udhalilishaji Mkoa wa kusini Pemba, imemswekwa chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 10, mshitakiwa Khamis Juma Chumu ‘ soda ’ (76) mkaazi wa Mtoni Chake Chake, baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mtoto wa miaka 13.   Hakimu wa mahakama hiyo Muumini Ali Juma, alisema kati ya adhabu hiyo, mshtakiwa atatumikia chuo cha mafunzo miaka 10 kwa kosa la ubakaji wa mtoto huyo.   Akisoma hukumu hiyo, alisema upande wa mashtaka ulifanikiwa kuwasilisha mashahidi watano kwenye kesi hiyo, akiwemo mtoto mwenyewe, ambae alitosha kwa kiwango kikubwa, ushahidi wake kuishawishi mahakama.   Alisema, mtoto ndio shahidi mkuu anayepaswa kuihakikishia mahakama kuwa, alibakwa na kutorosha ama laa, na sio mtu mwengine yeyote.   Hakimu huyo akiendelea kusoma hukumu hiyo alisema, wakati mtoto huyo wa miaka 13 anatoa ushahidi wake mahakamani hapo, akiongozwa na wakili wa serikali Ali Amour Makame, alieleza kwa kina, namna

KONGAMANO SIKU 16: ZLSC CHASIKITISHWA BABA, WAJOMBA KUWABAKA WATOTO WAO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KITUO cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ kimesikitishwa na kitendo cha baadhi ya baba wazazi, walezi na waalimu wa madrassa, kuwafanyia vitendo vya ukatili na udhalilishaji watoto walio na mamlaka nao. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Kituo hicho Harusi Miraji Mpatani, kwenye maelezo yake yaliotolewa na Mratibu wa kituo hicho Pemba Safia Salehe Sultan, kwenye kongamano la kuelekea siku 16 za kupinga ukatili, lililofanyika Kiwanda cha Makonyo Wawi Chake chake. Mkurugenzi huyo alisema, katika utafiti wa miezi tisa, uliofanywa na Chama cha Waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, watu 182 walifanyia usaili ili kupata taarifa hizo. Alisema, kati ya watu hao wanawake 115 na wanaume walifikiwa 67 kutoka kisiwa cha Unguja na Pemba, ambapo moja ya malengo ya utafiti huo ni k ufichua kesi zilizo jificha kutokana na muhali na mkwamo katika ngazi za chini mpaka kufikia muafaka wa kesi husika.   Alieleza kuwa, ameshtushwa na kubainika kwa baba waz

KONGAMANO SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI PEMBA LAWAONYESHEA VIDOLE WATOTO KUANZIA MIAKA 14

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: MAHAKAMA maalum ya kupamba na makosa ya ukatili na udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba, imesema kesi za udhalilishaji zinazowahusu watoto wenye umri wa kati ya miaka 14 hadi 17, ndio pekee zinazowatesa wao na ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka, kwa kule kukataa kutoa ushahidi. Kauli hiyo, imetolewa na Hakimu wa mahakama hiyo Muumini Ali Juma, wakati akitoa ufafanuzi wa baadhi ya masuali yalioulizwa na wananchi, kwenye kongamano la kuelekea siku 16 za kupinga ukatili, lililofanyika Kiwanda cha Makonyo Wawi. Alisema, mara matukio hayo yanapotekezea kwenye jamii, wazazi wao huwa na ari, kasi na hamu ya kuyafikisha mbele ya vyombo vya sheria, ingawa baada ya muda, hawaonekani mahakamani. Alisema, na hasa kesi za aina hiyo zinazowaweka njia panda ni zile zinazowakabili watoto wenye umri kati ya miaka 14 hadi 17, ambao kimatendo ni watu wazima. ‘’Hao wanaobahatika kufika mahakamani, basi wakati wa kutoa ushahidi hueleza kuwa, wale watuhumiwa waliodai kuwabaka

AANGUKA GHAFLA MAHAKAMANI HAKIMU AKIJITAYARISHA KUMSOMEA HUKUMU

    NA HAJI NASSOR, PEMBA:: MTUHUMIWA wa ubakaji Mohamed Ali Hassan miaka 19, aliyekataa kusomewa hukumu yake Novemba 21, mwaka huu kwa madai ya kuuguliwa na mzazi wake, juzi tena Novemba 24, mahakama imeshindwa kumsomea, baada ya kuanguka ghafla mahakamani hapo.   Mtuhumiwa huyo, alifika mahakamani hapo akiwa mzima, hadi ilipofika wakati wake aliitwa na kupanda juu ya kizimba cha mahakama ya makosa maaluma ya udhalilishaji ya mkoa wa kusini Pemba, ili kusubiri kusomewa hukumu yake.   Wakati Hakimu Muumini Ali Juma wa mahakama hiyo, akijitayarisha kuweka mambo sawa na mtuhumiwa huyo akiwa tulia kuangali kinachoendelea, ndipo ghafla alipoanguka.   Mtuhumiwa huyo alianza kuelezea kuwa hali yake imeshabadilika ghafla, huku akilalamikia maumivu jambo ambalo liliishughulisha mahakama.   ‘’Mheshimiwa Hakimu, kwa hakika hali ya afya yangu imeshaharibika na sijiskilii, huku akishikilia baadhi ya viungo vyake, akielezea kupata maumivu makali,’’alilalamikia.   Kisha mtuhumi

VIZIWI PEMBA WATAKA ELIMU YA UKIMWI KUWE NA WAKALIMANI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA WATU wenye ulemavu uziwi kisiwani Pemba, wameomba kuwekewa wakalimani wa lugha ya alama, kila aina ya kipindi au taarifa yoyote, inayohusu elimu ya Ukimwi, ili iwe rahisi kwao kufuatilia kwa ukaribu.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, kuelekea siku ya Ukimwi duniani Disemba 1, walisema bado elimu ya kujikinga na vurusi vya ukimwi kwa kundi lao, hijawafikia vizuri.   Walisema, tume za Ukimwi ile ya Zanzibar na ya Tanzania bara, hazijaweka kipaumbele juu ya kuweka wakalimani wanaporushwa vipindi, juu ya masuala ya Ukimwi.   Mmoja kati ya viziwi hao, Omar Khamis Juma wa Ole, alisema wanakosa elimu kubwa ya kujikinga ama mapambano ya virusi vipya ya Ukimwi, kutokana na kuachwa nyuma.   Alieleza kuwa, ijapokuwa kupitia shirika la Utangaazaji Zanzibar ‘ZBC’ kuna baadhi ya vipindi kunawekwa wakalimani, lakini bado sio vipindi vyote.   ‘’Tunataka kila kipindi, hutuba, tangaazo au wito unaogusa suala la Ukimwi, VVU, unyanyapaa au dawa za

HABARI ZA HIVI PUNDE KUTOKA MAHAKAMANI CHAKE CHAKE PEMBA

 TAARIFA za hivi punde kutoka ndani ya viunga vya mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji ya Mkoa wa kusini Pemba, zinaeleza kuwa mshtakiwa Khamis Haji Chumu 'soda' miaka 76, wa Chake chake amehukumiwa chuo cha mafunzo kwa miaka 15 baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka 13. Ilkuwaje hadi mzee huyo kukutwa na kisanga hicho, endelea kufuatilia www.pembatoday.blogspot.com maana sisi kukuhabarisha ni fahari yetu

HUKUMU ALIYEDAIWA KUMBAKA MTOTO WA KAMBO CHAKE CHAKE LEO

   NA HAJI NASSOR, PEMBA:: SHEMSA Hakim Khamis wa Chanjamjawiri wilaya ya Chake chake, ameiambia mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji ya mkoa wa kusini Pemba kuwa, mume wake hajambaka mtoto wao wa kumlea, bali ni uongo alioutengeneza mtoto huyo.   Alidai kuwa, mtoto huyo amekuwa muongo mzoefu na mzushi, maana siku ambayo, alidai amebakwa na mumewake, alikuwa safarini kikazi kisiwani Unguja.   Shemsa ambae ni shahidi nambari nne kwenye shauri linalomkabili mumewake (mtuhumiwa Said Abdalla Issa ), alidai kuwa mumewa alikuwa kisiwani Unguja kikazi siku hiyo aliyodaiwa kubaka.   Alidai kuwa, mtoto huyo ambae ni wa kulea, amekuwa muongo na alishawahi kumsingizia jirani wao mwanamme, kuwa alishawahi kumvulia nguo na kumuonesha sehemu zake za siri, ingawa walipofuatilia, haikuwa sahihi.   Mke huyo wa mtuhumiwa, alidai kuwa mtoto huyo pia alishawahi kukamatwa na barua ya mahaba, ndani ya mkoba wake wa mabuku ya skuli, akiashiria kuwa mtoto huyo alishaanza kubadilika kit