Skip to main content

Posts

Showing posts from October 15, 2017
Ujumbe wa serikali ya Oman ambao upo nchini kwa ziara ya siku 10 leo unakwenda Bagamoyo mkoani Pwani kuangalia eneo la ujenzi wa viwanda, ili uwekezaji huo uanze mara moja. Hatua hiyo ambayo ilielezwa katika taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais  inaleta matumaini ya kumwagika kwa ajira mbalimbali ndani ya muda mfupi ujao. Akizungumza Ikulu, jijini Dar es Salaam baada ya majadiliano na Rais John Magufuli, taarifa hiyo ilisema, Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman, Dk. Mohammed Hamad Al Rumhy alisema yeye na ujumbe wake wa watu 300 watakwenda Bagamoyo leo kuangalia eneo la ujenzi wa viwanda, ili kazi hiyo ianze mara moja. “Mhe. Rais tunataka kushirikiana nanyi kuendeleza ukanda wa uwekezaji wa Bagamoyo,” taarifa ya Ikulu ilimkariri Dk. Al Rumhy akisema. “Tunataka Bagamoyo isiwe eneo la bandari tu, bali pia liwe ni eneo ambalo tutajenga viwanda mbalimbali, tuzalishe mbolea na tununue mazao ya wakulima na kuyasafirisha. “Sisi tupo tayari na kesho (leo) tunakwenda kuangalia en

Dk. Shein amuapisha Naibu mkuu KMKM

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amemuapisha Kepteni Khamis Simba Khamis kuwa Naibu Mkuu wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM). Kapteni Khamis Simba Khamis aliteuliwa hivi karibuni na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kushika wadhifa huo. Hafla hiyo,ilifanyika Ikulu mjini Zanzibar ambayo imehudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali akiwemo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd,  Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee. Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali, Wakuu wa Vikosi vya SMZ, Washauri wa Rais wa Zanzibar, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib pamoja na viongozi wengine wa Serikali. Ra

Polisi waua watuhumiwa watatu Kibiti

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewaua kwa kuwapiga risasi watuhumiwa watatu wa ujambazi, lilipokuwa katika doria ya kuwasaka watu wanaotuhumiwa kuhusika na mauaji ya Kibiti mkoani Pwani. Polisi wamesema baada ya kuwapekuwa, watuhumiwa hao walikutwa na mabomu saba, SMG moja ikiwa imefutwa namba zake na ‘magazine’ moja ndani yake ikiwa na risasi 16, maganda 10 ya SMG na pikipiki aina ya Fekon. Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, aliwaambia waandishi wa habari jijini jana kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa Jumatatu maeneo ya Msongola wilayani Ilala. Mambosasa alisema askari wake wakiwa katika doria ya kusaka watuhumiwa wa mauaji ya Kibiti, walitilia shaka pikipiki iliyokuwa imebeba watu watatu ikiwa haina namba. “Polisi walianza kuifuatilia na walipogundua kuwa wanafuatiliwa waliongeza mwendo na kukatisha njia kuingia barabara ya vumbi na walianza kufyatua risasi na polisi walijibu mashambulizi na kuwajeruhi,” alisema. Kamanda Mambosasa alisema baada ya wa

Waziri wa Maliasili Dkt. Kigwangalla atembelea meli ya Mfalme wa Oman, Dar leo

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dkt.Hamisi Kigwangalla amesema  Tanzania na Nchi ya Oman wamefanya mazungumzo ya pamoja ya namna ya kukuza sekta ya Utalii baina ya nchi hizo mbili ambapo watashirikiana katika muingiliano wa Watalii watakaokuwa wakitokea moja kwa moja Oman na kuja Tanzania. “Tumeweza kuzungumzia ushirikiano wa sekta ya Utalii. Hii ni pamoja na kuanzisha soko la pamoja  kati ya Oman na Tanzania. Watalii wanaokwenda Oman wanaotaka kuja nchi za Afrika basi waunganishwe moja kwa moja kutoka Oman na kuja Tanzania kwani wenzetu wana watalii wengi kuliko sisi. Hivyo ujio wao hapa nchini ni faida kubwa kabisa na tumejifunza mengi katika sekta hii. "Pia tumeweza kujifunza namna wenzetu wanavyoitangaza nchi yao  na sisi tutatumia uzoefu huo kuboresha sekta hii ya Utalii kama dhamana tuliyopewa” alieleza Dk. Kigwangalla. Awali Dk. Kigwangalla aliweza kutembelea meli hiyo ya kifahari ya Mfalme wa Oman Mhe. Qaboos bin Said ‘Fulk Al Salamah’ iliyofika mapema jana

Historia Mpya Yaandikwa Kati ya Tanzania na Barrick Mine

Kampuni ya uchimbaji wa madini ya Barick nchini imekubali kulipa fidia ya dola  milioni 300 ambazo sawa na bilioni 700 za Tanzania, pamoja na kuweka mgao sawa wa faida wa 50/50 na serikali, kufuatia mazungumzo ya ripoti ya makinikia. Taarifa hiyo imetolewa leo na serikali wakati ikikabidhi ripoti ya mazungumzo hayo kwa Rais John Pombe Magufuli, na kusema kwamba licha ya makubaliano hayo, pia kampuni hiyo imekubali masharti yote yaliyowekwa kufuatia mazungumzo hayo, ili nchi iweze kunufaika na rasilimali zake. Pia kwenye ripoti hiyo imekubaliwa kuwa migodi yote itaweka fedha zake kwenye akaunti zilizopo hapa nchini, na serikali kubakia na umiliki wa madini yote yatakayokuwepo kwenye makinikia, ukiondoa dhahabu, shaba na fedha ambayo yatakuwa yanamilikiwa na Barrick kisheria. Pamoja na hayo makubaliano yaliyofikiwa yameitaka kampuni hiyo kuwapa ajira za kudumu wazawa wa eneo husika, na kuwapa stahiki zote kama wafanyakazi, na wamekubali kulipa kile kinachostahili kwenye hal

Serikali Yawapa Siku 7 Wavamizi Nje ya Nchi

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Hamisi Kigwangalla amefunguka na kuwapa siku saba wavamizi ambao wapo kwenye pori tengefu la Loliondo kuondoka mara moja ndani ya siku hizo kwani wasipofanya hivyo baada ya hapo mali zao zitataifishwa na serikali. Kigwangalla amesema uwepo wa wavamizi hao ambao wana ng'ombe zaidi ya 6,000 na matrekta zaidi ya 200 kutoka nchi ya jirani imekuwa sababu kubwa ya chanzo cha mgogoro wa ardhi baina ya vijiji na hifadhi hiyo.   "Kuna taarifa kwenye eneo lenye mgogoro la Pori Tengefu la Loliondo, kuna ng'ombe zaidi ya 6,000 na trekta zaidi ya 200 toka nchi jirani, yote kinyume cha sheria! Uwepo wao siyo tu unahatarisha uhai wa mfumo wa ikolojia ya Serengeti-Mara, bali pia unapunguza eneo la kuchungia kwa wenyeji wa Loliondo. Hivyo kuleta kiu ya wananchi wa Loliondo kuingia ndani zaidi ya eneo la hifadhi kutafuta malisho na hatma yake kuhatarisha uhai wa Serengeti. Uvamizi huu wa wenzetu kutoka nchi jirani ni moja ya sababu kubwa (ziliz

TUCTA Wamjibu Msenaji Mkuu wa Serikali

Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania TUCTA limesisitiza  kuwa madai ya wafanyakazi  iliyowasilisha serikalini ni halali na litaendelea kufuatilia ili wahusika wapate stahiki zao. Akizungumza jijini  Arusha Rais wa TUCTA Tumaini Nyamhokya amesema wamesikitishwa na kauli ya Msemaji  Mkuu wa Serikali ya kutaka madai ya wafanyakazi yapuuzwe na kwamba kauli hiyo haikuwa na busara yoyote. Nyamhokya amesema kwamba madai yao wameyafanyia utafiti wa kina na wanaendelea kusisitiza kuomba serikali itekeleze ahadi zake za nyongeza ya mshahara, upandaji wa madaraja kwa wafanyakazi, nyongeza ya mshahara ya kila mwaka ambayo ipo kisheria na madai ya wafanyakazi yatokanayo na mishahara na yasiotokana na mishahara. "Tuna madai halali yaliyofanyiwa utafiti wa kina na bado tunahitaji utekelezaji wake kwa haraka ili kuleta nafuu ya wafanyakazi nchini," amesema. Nyamhokya amesema TUCTA inaendelea kutambua dhamira ya kweli ya Rais John Magufuli katika kutatua changamoto

CHADEMA Wajitoa Muhanga Sakata la Lowassa

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu amefunguka na kusema kwamba wanawaruhusu Chama cha Mapinduzi watumie nafasi ya Lowassa kuwepo Chadema kuwaita wao mafisadi kama jinsi wao walivyofanya kwa miaka mingi. Salumu amesema kwamba kuwataja watu ambao waliwaita vinara wa ufisadi na leo wapo nao kwenye chama chao ulikuwa ni wajibu wao kama chama cha upinzani kutumia upenyo wa udhaidfu wa chama cha mapinduzi kuonyesha wananchi madhaifu ya serikali.  "Lazima ukubali kwamba ni wajibu wetu kuonyesha madhaifu ya serikali, Kama tulikuwa tunampinga Lowassa kwamba ni fisadi ulikuwa ni wajibu wetu Chadema. Sasa kama leo hii Lowassa yupo kwetu ni wajibu wao CCM kuwaambia watanzania kuwa Chadema kina mafisadi. Kwa sababu Lowassa amekuja Chadema ni yule yule wala hajawa malaika kama jinsi ambavyo kelele zinavyopigwa," Mwalimu amefunguka Akizungumzia kuhusu chama kupwaya na kumtegemea mtu mmoja kuwa mkosoaji wa serikali iliyopo Madarakani, Mwalimu amesema kupan
Maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam, wamewahoji kwa zaidi ya saa sita, madiwani waliojiuzulu Chadema wanaotuhumiwa na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kuwa walipewa rushwa. Waliofika Takukuru ni Catherine Mtui, aliyekuwa diwani wa viti maalumu, Japhet Jackson (aliyekuwa diwani wa Ambuleni) na Bryson Isangya (aliyekuwa diwani wa Maroroni). Baada ya kuhojiwa hawakutaka kuzungumza chochote wakisema wanaacha uchunguzi uendelee. Pamoja nao, diwani wa Mbuguni, Ahimidiwe Rico anayedaiwa kuwa ndiye alirekodi sauti na picha wakati akishawishiwa na viongozi wa Serikali na wa Halmashauri ya Meru amehojiwa kwa zaidi ya saa tatu jana Jumanne Oktoba 17, 2017. Rico amesema amewaeleza Takukuru kila kitu ambacho anakifahamu katika sakata hilo, ikiwemo kuwarekodi viongozi ambao walimshawishi kujiuzuru udiwani. "Msimamo wangu ni kwamba, nachukia rushwa. Nimewaeleza kila kitu na wao waliniuliza kuhusu

Haji Mnara: Bila CHADEMA na Tundu Lissu, CCM Italala

Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Timu ya Simba, Haji Manara ambaye ni mwanachama wa CCM amefunguka na kusema hajawahi kumshabiki Tundu Lissu wala CHADEMA lakini anaamini bila uwepo wake na CHADEMA basi chama chake CCM kitalala. Haji Manara amesema hayo leo baada ya kuona picha ya kwanza ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu akiwa hospitali jijini Nairobi nchini Kenya ambapo anapatiwa matibabu kufuatia kupigwa risasi Septemba 7, 2017 na watu wasiojulikana. "Ohhh God,mimi sijawahi kukushabikia wewe wala chama chako ila nakuombea kwa Mungu upone haraka kaka, urudi katika harakati zako nikiamini bila uwepo wenu chama changu kitalala" aliandika Haji Manara kupitia ukurasa wake wa Instgram. Mbali na Haji Manara watu wengine wengi wameonyesha kufurahishwa na hali ya Tundu Lissu baada ya kumuona kupitia picha ambazo zimeanza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, Mbunge huyo wa Singida Mashariki anatarajiwa kupelekwa nje ya nchi kwa matibabu ya awamu ya ta

Rais Magufuli amtumia ujumbe mfalme wa Oman

Rais John Magufuli leo Oktoba 18, 2017 amemtumia ujumbe Mfalme wa Oman Mtukufu Sayyid Qaboos bin Said Al Said na wawekezaji wengine wa Oman kuwa atafurahi kuona wanakuja kuwezeka nchini tena kwa haraka na kudai serikali itatoa ushirikiano. Rais ametuma ujumbe huo kwa mfalme wa Oman kupitia kwa Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman Mhe. Dkt. Mohammed Hamad Al Rumhy aliyeongozana na Waziri wa Uwekezaji wa Oman Mhe. Salem Ben Nasser Al Ismaily na Naibu Waziri wa Utalii Mhe. Maitha Saif Majid, ambao walikua Ikulu Jijini Dar es Salaam. Mfalme wa Oman Mtukufu Sayyid Qaboos bin Said Al Said amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuwa nchi hiyo ipo tayari kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuongeza uwekezaji katika viwanda, uzalishaji wa nishati, kuongeza thamani ya madini, kuendeleza sekta ya gesi na mafuta na kuendeleza ukanda wa uwekezaji wa Bagamoyo ili kukuza uchumi kwa kasi zaidi. “Mhe. Dkt. Mohamed naomba ukamwa

Orodha ya majina ya wanafunzi watakaopata mikopo ya HESLB Yakamilika

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imesema baada ya uchambuzi wa maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2017/2018, orodha ya awamu ya kwanza yenye wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza waliopangiwa mikopo imekamilika. Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Jumatano Oktoba 18,2017 amesema Sh34.6 bilioni zimetengwa kwa ajili ya wanafunzi hao 10,196. Amesema kwa jumla Sh108.8 bilioni zitatolewa kwa wanafunzi 30,000 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/2018. Badru amesema orodha ya awamu ya kwanza inapatikana kwenye tovuti ya Bodi ya Mikopo http://www.heslb.go.tz/ na itatumwa kwa vyuo husika. Amesema orodha nyingine (batches) zitafuata kwa kadri utaratibu wa udahili na uchambuzi unavyokamilika. “Lengo ni kutoa majina ya wote waliofanikiwa kupata mkopo kabla ya vyuo kufunguliwa mwishoni mwa mwezi huu wa Oktoba, 2017,” amesema. Mkurugenzi mtendaji huyo amesema orodha hiyo ya wana

Nape Ampa Neno Tundu Lissu

Mbunge wa jimbo la Mtama kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Nape Nnauye amefunguka na kusema amefurahi kumuona Tundu Lissu akiwa katika furaha na tabasamu na kumuomba kwa sasa asiseme lolote mpaka pale atakapona kabisaa.  Nape Nnauye amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter na kusema tabasamu la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiwa kwenye hospitali jijini Nairobi linatoa matumaini makubwa.  "Mjomba tunamshukuru Mungu kwa tabasamu hili la matumaini!Nakuombea afya iimarike kabla hujasema mengi! Tulia mjomba upone kabisa kwanza" alisema Nape Nnauye  Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alishambuliwa na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma nyumbani kwake na baadaye alipelekwa jijini Nairobi kwa matibabu zaidi ambapo mpka sasa anapatiwa matibabu huko.