Skip to main content

Posts

Showing posts from December 18, 2022

WAJAWAZITO WAELEZEA MATUNDA KUJIFUNGULIA HOSPITALI, WANAOBAKI MAJUMBANI ROHO MKONONI

      HABIBA ZARALI, PEMBA:::   LICHA ya serikali kuimarisha huduma za akina mama na watoto mijini na vijijini, ili wajifungulie hospitali, bado jitihada hizo zinaonekana kubezwa na baadhi ya akina mama hao.   Tayari Unguja na Pemba serikali imesogeza karibu vituo vya afya na kutowa elimu afya ya uzazi tofauti na zamani, wapo akina mama hujifungulia majumbani wakisaidiwa na wakunga wa jadi.   Ni dhahir kuwa akina mama wanapobeza maelekezo hayo na kuamuwa kubakia majumbani hadi kujifunguwa kunaweza kuwaletea madhara yatokanayo na uzazi.   Na ndio maana serikali kupitia wizara ya Afya, wakawataka wakunga wa jadi kuwasindikiza mama wajawazito hadi katika vituo vya afya na sio kuwazalisha wakiwa majumbani.   Na ndio maana hata Raisi wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi katika hutuba zake za mara kwa mara, huitaka wizara ya Afya kutowa huduma bora na kuona kwamba kunapunguwa vifo vya mama na mtoto.   Uchunguzi wa makala hii umebaini kuwa bado wapo akina mama ambao

USHIRIKA ENEO LILILOPUNGUZA FOLENI YA AJIRA SERIKALINI WANAWAKE, VIJANA WAVAMIA SEKTA HIYO

  NA MARYAM SALUM, PEMBA::: WALIOSEMA ‘umoja ni nguvu utengano ni udhaifu’ wala hawakukosea.   Waliaamini kuwa, watu wanapofanyakazi kwa pamoja, maendeleo na ushindi kwa kweli hupatikana. Sheria namba 15 ya mwaka 2018 iliundwa kwa ajili ya kuipa nguvu   sekta ya ushirika, ili iweze kuimarika zaidi   kwa nia ya kuwafanya wananchi wapate ajira na kipato.      HISTORIA YA VYAMA VYA USHIRIKA Sekta ya ushirika iliasisiwa hapa Zanzibar tokea miaka ya 1923 hadi mwaka 1925, ingawaje haikupewa kipaumbele kikubwa kwa wakati huo, kutokana na ukosefu wa sera makini. Ambapo kwa wakati huo, jamii haikuwa ikiona manufaa kwa kuwepo kwa sekta hiyo, hali iliyotajwa kupana foleni ya ajira kubwa serikalini.                         HALI YA SASA Miaka ya hivi karibuni sekta hiyo, imepewa mkazo mkubwa na kujengewa mazingira na kuundiwa sera madhubuti baada ya kuonekana ni fursa mzuri kwa wananchi kuweza kupata pahala pa kujiajiri bila ya kusubiri ajira kutoka serikalini. Sera hiyo ili

MAZIWA YA MAMA LULU YA KIPEKEE KWA MTOTO

      HABIBA ZARALI, PEMBA: KILA mwanzoni mwa wiki ya mwezi wa Agosti, ya kila mwaka, dunia huwa na wiki ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama.   Lengo la wiki hii, huwa ni kusisitiza umuhimu wa maziwa ya mama kwa watoto wachanga na wadogo, kiafya.   Afya ni kitu muhimu katika maisha ya mwanadamu na kinyume chake, ni kuzalisha maradhi kadhaa yanayodhoofisha mwili na kiakili.   Katika kuhakikisha afya ya mwanadamu inaimarika, msingi wake huanzia tokea mtoto anapokuwa tumboni na mara anapozaliwa, kwa kuhakikisha anapewa mahitaji ya msingi ikiwemo maziwa ya mama.   Maziwa ya mama yana kinga kamili ikiwemo ya vitameni A vya kutosha ambavyo huwa ni kinga ya maradhi mbalimbali kwa mtoto mchanga.   Ingawa wapo baadhi ya akina mama hawapendi kunyonyesha na huamuwa kumuachisha ziwa mtoto mara tu, anapojifunguwa, kwa sababu tofauti ikiwemo kuhofia maziwa yake kuanguka, kupoteza haiba na muonekano wake.   Katika hatuwa ya kumlisha mtoto chini ya miezi sita kunaweza kumsa