Skip to main content

Posts

Showing posts from February 27, 2022

UTALII WA VISIWA VIDOGO VIDOGO MKOMBOZI WA UCHUMI KWA WANANCHI

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA SERIKALI ya awamu ya nane inayoongozwa na Dk. Hussen Ali Mwinyi imelichukua suala la uwekezaji wa visiwa vidogo vidogo Zanzibar katika hatua nyengine ambayo ni nzuri na yenye manufaa kwa nchi. Agosti hadi Septemba mwaka 2021, Serikali ilitangaza awamu ya kwanza ya uwekezaji, ambapo visiwa vinane (8) vilipata wawekezaji kati ya kumi (10) vilivyotangazwa. Visiwa hivyo ni Changuu, Pwani, Bawe, Pamunda A na B, Kwale, Chumbe, Misali, Njau na Matumbini A, ambapo kisiwa cha Njau na Matumbini A wawekezaji walishindwa masharti. Serikali imeweka vigezo maalumu kwa wawekezaji wa visiwa na ikiwa hakufikia, hatopatiwa kwani Serikali iko makini kwenye suala hilo. Anasema Mkurugenzi Uwekezaji Pemba Al-haji Mtumwa Jecha, awamu ya pili ilitangazwa mwaka huu, ambapo kwa Pemba ni kisiwa cha Matumbini, Jombe na Kwata Kusini na Kashani, Njau na Fundo Kaskazini.    Visiwa hivyo vitakodishwa muda mrefu ili vijengwe hoteli za kitalii zitakazotoa huduma mbali mbali na utakuw

KIKUNDI CHA 'KHERI LIWE" KENGEJA WAANZA KUONA MWANGA, WAIPA TANO TAMWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KIKUNDI cha ‘Kheri liwe’ kilichopo Likoni shehia ya Kengeja wilaya ya Mkoani Pemba, kimesema mafunzo, mawazo na fikra walizopewa na TAMWA-Zanzibar, sasa zimezaa matunda baada ya kujipatia zaidi ya shilingi milioni 2.8 ikiwa ni faida kwa miaka mitatu iliyopita. Wanakikundi hao, walisema baada ya kuanzisha mpango wa kuweka fedha na kukopa ‘ hisa ’ ambao walishawishiwa na TAMWA, na kufanya biashara ndogo ndogo, utengenezaji sabuni na kilimo cha mboga, sasa wameona matunda yake. Wakizunguma na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, wanakikundi hao, walisema kumbe walichelewa kujikusanya na kama wengeanza miaka ya nyuma zaidi, kwa sasa wengeshapiga hatua kubwa zaidi. Walieleza kumbe zipo fursa kadhaa endapo jamii itazifanyiakazi kupitia vikundi hivyo, na kisha kuwezeshwa kimafunzo na fikra za jinsi ya kukusanya fedha na kisha kujikopesha wenyewe. Mwenyekiti wa kikundi hicho Fatma Nahoza Juma, alisema sasa kila mwanachama ameshapata faida, iwe wakati wanap