Skip to main content

Posts

Showing posts from September 25, 2022

WANANCHI PEMBA WAONESHWA NJIA KUJIKINGA 'TB'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WANANCHI kisiwani Pemba, wametakiwa kuendelea kuchukua hatua za kuchunguuza afya zao mara kwa mara, ili wajielewa ikiwa wanaishi na vimelea ambavyo vinaweza kusababisha ugonjwa wa kifua kikuu ‘TB’.   Ushauri huo umetolewa na m taalamu kutoka kitengo shirikishi cha maradhi ya ukoma, kifua kikuu na Ukimwi Zanzibar, Said Khamis Ahmada, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi.   Alisema, moja ya njia ya kujikinga ama kuwahi matibabu ya ugonjwa huo, ni kuwa na tabia ya kuchunguuza afya mara kwa mara, ii upatikane ufumbuzi kwa wataalamu wa afya.   Alieleza kuwa ugonjwa wa kifua kikuu kitaalamu unaoitwa (‘ Tuberculosis’ TB) ni miongoni mwa magonjwa 10 yanayosababisha vifo kwa wingi duniani kote.   Alifahamisha kuwa tafiti zilizofanywa na Shirika la Afya Ulimwenguni ‘WHO’ zinaonesha kuwa, inakisiwa watu milioni 10 wameugua ugonjwa huo, duniani kote, na hadi mwaka 2020, na kati ya hao watu milioni 1.5 wamefariki dunia.   ‘’Utafifi huo ukagund

MATAMU HAYA HAPA RIPOTI YA 'CAG' MASHIRIKA YA UMMA ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::: MOJA ya mashirika ya serikali yaliotajwa kuongeza mapato yake, kupitia ripoti ya Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, ni Shirika la Umeme Zanzibar ‘ZECO’ lililongeza mapato yake, kutoka zaidi ya shilingi bilioni 33.579 mwaka 2019/2020, hadi kufikia zaidi ya shilingi bilioni 34.344 mwaka 2020/201. Hayo yamebainika, kwenye ripoti hiyo ya mwaka 2020/2012, ambayo iliwasilishwa mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za serikali, Dk. Othman Abass Ali. Ripoti hiyo imebainisha kuwa, kwa upande wa ZECO kulikuwa na ongezeko la zaidi ya shilingi milioni 764.207 sawa na asilimia 2, huku kwa mwaka 2020/2021, shirika hilo limepata faida ya zaidi ya shilingi bilioni 16.171, ikilinganishwa na faida iliyopatikana mwaka 2019/2021, ambayo ni zaidi ya shilingi bilioni 19.863 na upungufu ikiwa ni shilingi bilioni 3.692 sawa na asilimia 19. Shirika jengine ambalo mapato yake yameta

MAJAJI WAMALIZA KAMBI KUSIKILIZA RUFAA ZA MWAKA 2018 PEMBA

NA ZUHURA JUMA, PEMBA::: MAJAJI wawili wa mahkama kuu Zanzibar, wamemaliza kambi ya mwezi mmoja kisiwani Pemba, iliyokuwa na lengo la kusikiliza kesi za rufaa, zikiwemo za jinai ambazo zimefikishwa mahakamani kuanzia mwaka 2018 hadi mwaka 2021. Akizungumza na waandishi wa habari hizi, Naibu Mrajisi wa Mahkama kuu Pemba Faraji Shomari Juma alisema, baada ya uchunguzi mdogo uliofanywa na mahkama, uligundua kuwa kuna mrundikano mkubwa wa kesi za rufaa za mahkama kuu kisiwani humo. Alisema, licha ya majaji kuwa na utamaduni wa kwenda Pemba kwa ratiba zao za kawaida kufuatilia kesi, lakini Jaji mkuu ameona ni vyema, kuwapeleka Pemba majaji wawili kwa muda wa mwezi mmoja, ili kupunguza kesi. “Baada ya kuonekana kuna kesi nyingi ndipo Jaji Mkuu amewaleta majaji wawili, ambao walipiga kambi kwa muda wa mwezi mmoja, tunashukuru kesi nyingi zimeshatolewa maamuzi”, alisema. Alieleza kuwa, wameona zipo rufaa zaidi ya 25 ambazo nyingine ni tangu mwaka 2018, jambo ambalo lilikuwa likiwates

'THE FUTURE LIFE FOUNDATION' YAMWAGA MSAADA KWA WATOTO 320 PEMBA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA:::: MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali amesema, jamii inapaswa kuweka mifumo na mipango imara ya kuondoa huzuni za watoto yatima kwa kuwapatia haki zao za msingi. Alisema kuwa, watoto hao wamekuwa wakikumbana na kadhia mbali mbali ikiwepo kufanyiwa udhalilishaji, hivyo kuna haja ya kushirikiana pamoja katika kuhakikisha wanapata haki stahiki kama watoto wengine wanaoishi na wazazi wao. Akikabidhi msaada wa mcehele kwa watoto 320 uliotolewa na taasisi ya kusaidia mayatima, wajane, watu wenye ulemavu na wasiojiweza (The Future Life Foundation) , Mkuu huyo alisema, watoto yatima wanahitaji kusaidiwa kwa hali na mali ili wasiwe na huzuni katika maisha yao ya kila siku. “Mara nyingi watoto yatima wanadhalilishwa katika familia zile wanazoishi, hivyo ili kuona hawaishi na huzuni, tuwasaidie wajihisi kama wapo sawa na watoto wenzao”, alieleza Mkuu huyo. Aliishukuru taasisi hiyo kwa mambo wanayoyafanya kusaidia jamii na kusema kuwa atahakikisha anasaidia k