Skip to main content

Posts

Showing posts from January 28, 2024

WANANCHI SHUNGI: 'MAJI YA ZAWA ''BUL BUL'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema kwa muda mrefu sasa, hawana shida tena ya huduma ya maji safi na salama, kufuatia urekebishaji mkubwa uliofanywa na Mamlaka ya Maji Zanzibar ZAWA, tawi la Pemba. Walisema kwa sasa wanapata nafasi ya kujipangia muda wao wa shughuli za kilimo, biashara, wajasiriamali na wanaokwenda ofisini, baada ya kuwepo kwa huduma hiyo ya uhakika. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, walisema haijawahi kutokea, kwa mud mrefu kuwa na huduma hiyo kwa uhakika, ingawa sasa miaka karibu mitatu hawana wasi wasi. Walisema, kuwa shughuli zao za kujitafutia huduma za chakula na safari nyingine sasa, zimekuwa zikipangika vyema, kwani hapo awali walikuwa wakisuumbuka kutokana na huduma hiyo. Mmoja kati ya wananchi hao Asma Said Abdalla wa Chanjamjawiri, alisema kwa upande wake sasa, amepata utulivu wa kujipangia shughuli zake, kutokana na uwepo wa uhakika wa huduma yam aji safi na salama.

SERIKALI YA WANAFUNZI ‘IPA’ PEMBA YAPATA VIONGOZI WAPYA

  NA MARYAM NASSOR, PEMBA@@@@ UONGOZI wa serikali ya wanafunzi Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar, (IPA) tawi la Pemba, wamewataka viongozi wa chuo hicho, kutatua changamoto zinazowakabili kwa wakati. Ombi hilo, limetolewa na Naibu waziri mkuu wa Serikali ya wanafunzi chuoni, Rashid Khamis Yussuf, mara baada ya kuapishwa na kupata cheo hicho huko mjini Chake chake. Alisema, chuo hicho kinakabiliwa na changamoto lukuki, ambazo zinashindwa kupatiwa ufumbuzi kwa wakati sahihi, jambo ambalo linakwamisha maendeleo kwa wanafunzi. Alisema kuwa, kuna kipindi walikuwa na shida ya huduma maji katika chuo hicho, na ilidumu kwa muda mrefu na muhasibu alishindwa kuchukuwa fedha, ili kulitatua tatizo hilo. “Kuna wakati tulikuwa na shida ya maji katika Chuo chetu, na tatizo hilo lilidumu kwa muda, bila ya kupatiwa ufumbuzi na muhasibu yupo, ingawa alishindwa kulishughulikia,”alisema. Mwanafunzi Deo Mabula Alfred, alisema changamoto inayowakera ni kutokupewa vitambulisho, kile cha mitihan

WAZIRI LEILA AWAPA KONGOLE WANAFUNZI NG'OMBENI 'A' MKOANI KWA UFAULU

NA SALIM HAMAD, PEMBA @@@@   Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Leila Mohamed  Mussa amewapongeza wanafunzi wa Skuli ya Msingi  Ngo’mbeni  'A'  Wilaya ya Mkoani waliofulu vizuri  michepuo ya Darasa la saba waliofanya mitihani yao mwaka 2023. Waziri Leila aliyasema  hayo huko Mkoani Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba, wakati akizungumza na Walimu,Wazazi na Wanafunzi  katika sherehe ya kuwapongeza wanafunzi  wa Skuli  hiyo waliofaulu michipuo na kuwa  Skuli ya kwanza  katika Mkoa wa Kusini Pemba.  jumla ya wanafunzi 157  waliofanya Mitihani ya Darasa la saba katika Skuli ya Ng’ombeni (A) na katoa  michipuo 51 ambapo idadi hiyo imeifanya Skuli hiyo kuwa kwanza  kwa ufaulu kwa wanafunzi katika Mkoa wa Kusini Pemba. Alisema haikuwa kazi rahisi waliofanya wanafunzi hao kwani walipitia mazito wakati wa masomo yao,hivyo hawanabubudi kuzidisha jitihada zaidi katika kuona wanafika mbali na kutimiza ndoto zao. Alisema suala la kutafuta elimu ni jambo la msingi  ambalo Vijana wanapaswa