Skip to main content

Posts

Showing posts from March 19, 2023

WAZIRI TABIA AGAWA JARIDA, ALIPA TANO SHIRIKA LA MAGAZETI YA SERIKALI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WIZARA ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, imelipongeza Shirika la Magazeti ya serikali, kwa ubunifu wao wa kuanzisha jarida maalum, la kutangaaza utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa wananchi. Hayo yameelezwa na Waziri wa hiyo Zanzibar, Tabia Maulid Mwita, wakati akizungumza na masheha wa wilaya nne za Pemba, kwenye hafla ya ugawaji wa jarida hilo, iliyofanyika ukumbi wa Mfuko wa Hifadhi Jamii Zanzibar ‘ZSSF’ Tibirinzi Chake chake. Alisema, uongozi wa Shirika hilo, umezitekeleza kwa vitendo ahadi za Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, pale alipowataka wakuu wa taasisi kuwa wabunifu, ili kuwafikia wananchi. Alieleza kuwa, ubunifu huo ambao umezalisha jarida la kueleza kwa upana yale yaliyotekelezwa na serikali, utasaidia sasa kwa wananchi kuyaona kwa vitendo. Waziri Tabia alieleza kuwa, ingawa vyombo vya habari vya serikali vipo ikiwemo ZBC, lakini kupitia jarida hilo, kumeongeza wigo kwa wananchi, kuyasoma yaliot

SAADA KIJANA ALIYEHAMASIKA KUUSAKA UONGOZI, ASEMA CHANGAMOTO, BEZO KWA WENZAKE ZINAMPA KASI ZAIDI

             NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ “AMA kweli subira ni kitu cha kheir, mwenye kusubiri hakosi” “ Kejeli, maneno mabaya, machafu, matusi ya nguoni yote sikujali… nahakikisha nafikia lengo langu”,. Hayo maneno ya kijana mashuhuri anaesaka uongozi kila pembe aliejulikana kwa jila la Saada Saleh mkaazi wa Chwale Wilaya ya Wete Pemba. Anasimulia kuwa, maneno hayo na kejeli za watu hayakuwa yakimridhisha, ingawa kwa vile alikuwa na msimamo wa kutafuta basi hawakuweza kupata nafasi ya kumvunja moyo.   “Lakini niliwashindwa na wamebaki vinywa wazi, yasiyoniridhi nilipitia kwa muda mrefu bila kugombana wala kulipiza kisasi nao hadi nilipofikia”, anasema. Majirani, marafiki wa karibu na hata kwa baadhi ya ndugu wa familia walikuwa wanasema mengi, lengo lao ni kuona hafikii kwenye malengo yake ya kuwa kiongozi.   Saada aliamini misemo mbali mbali ya kiswahili kwamba… subra ni ngao, na pia nia njema hairogwi na ndipo alipokaza buti kuona anapamba na adui zake kuhakikisha an

SHERIA YA ELIMU ZANZIBAR YATIMIZA MIAKA 41, WADAU WATAKA ICHUNGULIWE UPYA

    HABIBA ZARALI, PEMBA LICHA ya sheria ya elimu Zanzibar nambari 6 ya mwaka 1982 kufanyiwa marekebisho ya mwaka 1993, ili kuimarisha upatikanaji wa elimu bora, lakini bado inaliliwa. Sheria hiyo ambayo inaonekana kukosa mashiko ya kuwadhibiti wazazi na walezi kikamilifu wasioshughulikia watoto wasiokwenda skuli, au wanaokatisha masomo kwa kuwaozesha waume. Baadhi ya vifungu hivyo ni kile cha 20 (1) na 22 cha sheria ya elimu Zanzibar, kwa kumuozesha mtoto ambae bado mwanafunzi. Ambapo hapo mzazi atakuwa ni mkosa na akitiwa hatiani adhabu zake kwa kosa la kwanza anatakiwa kulipa faini isiyopunguwa shilingi 1,500 na isiyozidi 3,000. Kosa la pili katika sheria hiyo ni faini isiyopunguwa 3,000 na isiyozidi 5,500 ambapo kosa la tatu atalipa faini isiyopunguwa 5,500 na isiyozidi 10,000 au kifungo kisichozidi miezi sita au vyote viwili. Pamoja na sheria hii kuwa haimkatazi mwanafunzi kuoa au kuolewa kabla ya kukamilisha elimu ya lazima, lakini kifungu cha 20 (3) kinaeleza kuw

MAKAMU WA RAIS 'WALEENI WATOTO KUZINGATIA MAADILI'

  Joyce Joliga Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwalea watoto kwa kuzingatia maadili ya kitanzania pamoja na kuongeza umakini katika maudhui yanayooneshwa katika televisheni.   Makamu wa Rais amesema hayo wakati akizungumza na waumini wa Kijiji cha kasumo mkoani Kigoma mara baada ya kushiriki Ibada ya kawaida ya katikati ya wiki katika Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Malkia wa Amani iliopo Kijiji hapo.   Amesema ni wazi kwa sasa kumekuwepo na changamoto ya mmomonyoko wa maadili ikiwemo ndoa za jinsia moja ambapo wazazi, walezi na jamii kwa ujumla inapaswa kukemea vikali ili kuondokana na taifa lisilofaa kwa vizazi vya sasa na baadaye.   Halikadhalika Makamu wa Rais amewaasa wananchi wa Kasumo na Mkoa wa Kigoma kwa ujumla kutoa ushirikiano wakati huu ambapo serikali inafanya ujenzi wa miundombinu ya barabara katika mkoa huo ambayo ni nyenzo muhimu kwa biashara na urahisi wa kufikia huduma za jamii k

WIZARA YA ARDHI, YATILIANA SAINI NA KAMPUNI YA SINOTEC UJENZI NYUMBA ZA MAENDELEO

NA SALMA LUSANGI, ZANZIBAR   Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi (WAMM) jana imesaini Hati ya Makubaliano na kampuni  ya Sinotec kwa ajili  ya Mradi wa Nyumba za Maendeleo Zanzibar.  Hafla ya utiaji saini  imefanyika jana katika ukumbi wa wizara hiyo ambapo kwa upande wa Wizara alisaini Katibu Mkuu Dkt Mngereza Mzee Miraji na kwa kampuni ya Sinotec alisaini Naibu Meneja Mkuu Jin Hua.  Akizungumza mara baada ya utiaji wa saini hiyo Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Mngereza amesema makubaliano hayo ni hatua ya mwanzo  katika utekelezaji wa mradi huo, ambapo lengo kuu ni kutekeleza Sera ya Makaazi bora kwa wananchi kupitia wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar. Naye Naibu Meneja Mkuu wa kampuni hiyo Jin Hua amesema amefarajika kupata fursa hiyo ya Kufanya kazi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya Ardhi ili kuifanya jamii kuwa na Makaazi bora ya kuishi. Kwa Upande wake Mkurugenzi Shirika la Nyumba Zanzibar (ZHC) Mwanaisha Ali Said amesema ujio wa kampuni hiyo n

WATU WENYE ULEMAVU VIKUNGUNI WALILIA UKOSEFU WA DAWA ZAO

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@@ WATU wenye ulemavu katika kijiji cha Vikinguni shehia ya    Ng'ambwa Wilaya ya Chake Chake Pemba wameiomba  Serikali kuwawekea dawa zao katika vituo vya afya, ili kuwasaidia katika kupunguza makali ya magonjwa yanayowasumbua.  Walisema kuwa, watu wenye ulemavu hasa wa akili pamoja na wenye kifafa wanahitaji watumie dawa kila siku ili kuimarisha afya zao, ingawa wakati mwengine hawatumii kutokana na kuzikosa dawa hizo ukilinganisha wengi wao hali zao ni duni kimaisha. Wakizungumza na Zanzibarleo kijijini kwao walisema, dawa hizo ni tatizo katika kituo cha afya cha Vikinguni hali ambayo inawafanya wakanunue, jambo ambalo wakati mwengine wanashindwa kutokana na kukosa fedha. "Kila siku watu hawa wanahitajia wameze dawa ili afya zao ziweze kuimarika lakini wakati mwengine tunashindwa kuwapa kwani mpaka tununue na hatuna uwezo", waliesema watu wenye ulemavu. Nassir Suleiman Hamad alisema kuwa, wamekuwa wakipata usumbufu wakati wanapoanguka watu wen

WATATU MIKONONI MWA POLISI TUHMA ZA UPIGAJI MAPANGA KENGEJA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ JESHI la Polisi Mkoa wa kusini Pemba, linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kumshambulia mfanyabiashara Maulid Haroub Mpemba na mke wake, katika eneo la Kengeja wilaya ya Mkoani Pemba. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi Mkoa huo Abdalla Hussein Mussa, alisema watuhumiwa hao, walikamatwa katika siku na maeneo tofauti humo. Aliwataja waliowakamata kuwa ni pamoja na Saleh Mohamed Abdalla ‘Mbambe miaka 33, Mohamed Rashid Mohamed miaka 42 wote wakaazi wa Mjiweni Kengeja na Salum Mohamed Seif ‘Rumbwi miaka 36 mkaazi wa Tumbi Wambaa. Alisema kuwa, baada ya kupokea taarifa za tukio hilo kutoka kwa wasamaria wema, majira ya saa 7:00 usiku Machi 17 mwaka huu, Jeshi la Polisi liliandaa mitego na kufanikiwa kuwakamata katika maeneo na siku tofauti. Alisema watuhumiwa hao, wanaodaiwa kumshambulia mfanyabiashara huyo kwa vitu vyenye ncha kali, katika sehemu mbali mbali za mwili wake, huku mke wake wakimshambulia kwa ku

RC MATTAR: UWAPE TUNGENI MASHAIRI KUPINGA UDHALILISHAJI, DAWA ZA KULEVYA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKUU wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massuod, amewataka washairi na watunzi wa Umoja wa Washairi wa Pemba ‘UWAPE’ kutunga mashairi, yenye kuihamasisha jamii, kupiga vita vitendo vya udhalilishaji, dawa za kulevya na majanga mengine . Alisema, jamii imezongwa na majanga na kukuawa kila siku, hivyo washairi wanayonafasi ya kukemea, kushauri, kuekeza njia ya kupunguza matendo hayo, na chanzo chake kupitia mashairi yao. Mkuu huyo Mkoa, ameyasema hayo Machi 19, 2023 ukumbi wa Umoja ni nguvu Mkoani, kwenye hutuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa wilaya ya Chake chake, Rashid Abdalla Ali. Mkuu huyo wa Mkoa alisema, njia ya mashairi ni nzuri na nyepesi katika kufikisha ujumbe husika kwa jamii, hivyo ni wakati wa washairi wa ‘UWAPE’ kuliono hilo haraka.. ‘’Kwa sasa, kila mmoja ni shahidi kuwa, jamii yetu inakumbana na majanga, mbali mbali hata migogoro ya ardhi, dawa za kulevya, udhalilishaji na mivutano ya kifamilia, hivyo washairi waang

WAZIRI RAHMA ATAKA ARDHI INAYOTUMIKA VIBAYA FUJONI KUREJSHWA SERIKALINI

  NA SALMA LUSANGI, ZANZIBAR Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Mhe.Rahma Kassim Ali ameuagiza uongozi wa Kamisheni ya Ardhi Zanzibar  kushirikiana na ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Magharibi "B" kuirudisha serikalini eka  iliopo Fujoni kufuatia kutumika kinyume na utaratibu. Eka hiyo inayomilikiwa  na bw Faki Rashed Faki  lakini anadaiwa kuikata viwanja na kuviuza kwa ajili ya ujenzi wa nyumba kinyume na matumizi ya shughuli za kilimo yaliyowekwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.  Mhe.Rahma ametoa agizo hilo alipofanya ziara kuitembelea eneo hilo mara baada ya kupata taarifa kutoka kwa mwananchi kuhusiana na uuzwaji wa eneo hilo la eka ya serikali.   "Hatua ya kurudisha serikalini eka hii itakua ni funzo kwa wale wote ambao walipewa eka kwa ajili kuziendeleza kwa shughuli za kilimo na badala yake kuzitumia eka hizo kwa kuzikata viwanja na kuuza"Alisisitiza  waziri Rahma.   Ameongeza kuwa Wizara ya Ardhi Zanzibar itahakikisha inazifatilia kwa makini eka zote za Se