Skip to main content

Posts

Showing posts from November 12, 2023

PACSO: ‘TUNATEKELEZA KWA VITENDO MAONO YA DK. MWINYI, DK. SAMIA’

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MRATIBU wa miradi kutoka Mwenvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, alisema wanatekeleza kwa vitendo, maono ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, la kuhakikisha elimu ya uraia na demomkrasia inawafikia wananchi. Mratibu huyo aliyasema hayo, wakati akizungumza na watendaji wa serikali na wanaasasi za kiraia, katika kongamano la pamoja, la kujenga ushirikiano, baina pande mbili hizo, kupitia mradi wa ‘uraia wetu’ lililofanyika Wawi Chake chake. Alisema, mradi huo ni tokeo moja wapo la maono ya viongozi hao, ambapo wameamua kuwakusanya watendaji wa serikali na wale wa asasi za kiraia, ili kuibua changamoto zinazokwamisha ushirikiano wao. Alieleza kuwa, washiriki wa kongamanio hilo, watapata nafasi ya kuelezea changamoto zao kikanuni, sera na kisheria ili kuona zinatatuliwaje kwa umoja wao. ‘’Sote ni mashahidi kuwa, wakati viongozi wetu wanaingia madarakan

KESI YA HEROIN PEMBA YAPIGWA KALENDA WAKILI, SHAHIDI WANAUMWA

  NA HAJI NASDSOR, PEMBA@@@@ KESI ya kupatikana dawa, zinazoaminika kuwa ni za kulevya, iliyopo Mahakama kuu Zanzibar kisiwani Pemba, imeshindwa kuendelea, baada ya shahidi na wakili wa utetezi, kutochomza mahakamani hapo, kwa udhuru wa kuumwa. Awali mtuhumiwa katika shauri hilo Ame Kheir Ali, aliwasili mahakamani hapo, akimsburi wakili wake Zahran Mohamed Yussuf, ili aendelee na hatua ya kumskiliza shahidi wa upande wa mashtaka, ingawa alielezwa na Jaji wa mahakama kuu kuwa, wakili wake anaumwa. Jaji Ibrahim, alimueleza mtuhumiwa huyo kuwa, kwa mujibu barua iliyopokelewa mahakamani hapo ni kuwa, wakili wake huyo hayupo kisiwani Pemba kwa sasa. ‘’Mtuhumiwa leo (jana) tunakuomba radhi, maana wakili wako Zaharan Mohamed Yussuf, hayupo hapa mahakamani na kisiwani Pemba, yuko Tanzania bara kimatibabu,’’alisema Jaji. Kisha, Jaji huyo aliupa nafasi upande wa mashtaka kusema, jambo juu ya hilo na Wakili wa serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Seif Mohamed Khamis, alikubaliana na ta

UKIMNYA UNAVYOWAATHIRI WATOTO KISAIKOLOJIA WALIOFANYIWA UDHALILISHJAJI

    NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@ MOJA ya jambo muhimu ambali wazazi na walezi waliowengi ambalo hawalifanyi hasa kwa miaka ya siku hizi, ni kukosa kuwa karibu na watoto wao. Ni tofauti kabisa na karne zilizopita, ambapo wazazi na walezi hao walitenga muda kukaa na watoto wao, kama sio wajukuu na kuwapa maelekezo ya hatma ya maisha yao. Wapo walikuwa wakithubutu kuwapa hadithi za mafundisho, namna bora ya kukabiliana na maisha na au wakati mwengine hata jinsi ya kupambana na adui.   Kwa karne ya sasa wazazi hujifanya hawana nafasi hiyo, wengi wakisingizia ugumu wa maisha, na hao wachache wanaokanaa nao, hukosa kuwapa dunia ilipofikia. Ndio maana mwanaharakati wa masuala ya kupinga ukatili na udhalilishaji Aisha Muhidin Juma wa Fuwoni, anasema kwa kule wazazi kukosa nafasi hiyo, husababisha watoto kuwa wapweke. Kisha kinachofauta anasema ni kugubikwa na madhara makubwa kwa watoto hao, tena hasa ikiwa wameshafanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji. Anaona wapo wazaz

HIZI HAPA SABABU ZA KUNAWIRI MATUKIO YA UDHALILISHAJI, MOJA KUKIMBIA WATUHUMIWA

     NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@ UDHALILISHAJI  ni kile kitendo ambacho hufanyiwa mtu yoyote bila ya ridhaa yake.   Na wakati mwingine kitendo hicho, kikashusha hadhi, thamani, utu, kuvurugika kwa ajili, kimwili, kijamii na hata kiuchumi kwa mtendewa.   Katika ulimwengu wetu wa sasa, kesi za udhalilishaji zimezidi kushamiri kila siku zikenda mbele, watuhumiwa wanaongezeka mitaani kwa kila leo.    Tatizo kubwa linalowakumba wanajamii ni kuoneana muhali kutokana na watendaji wa matukio hayo aidha ni watu wa karibu na familia, hivyo ikigundulika  kua ni baba au mjomba aliebaka basi kesi  inamalizwa kifamilia.   Haya si matukio mapya masikioni mwetu, ambayo yanafanyika na badala yake watuhumiwa wanakimbia na kupelekea waathirika kushindwa kupata haki yao.     WALIOPATA UKATILI WA UDHALILISHAJI WA KUBAKWA   Kwa mujibu wa mama mzazi wa Halima Juma (si jina lake halisi) mkaazi wa kijiji cha Kidemeni wilaya ya Chake Chake, alisikitishwa kutokana na tukio kama hilo, ambal

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

MASHEHA ZANZIBAR WATAKIWA KUKOLEZA USHIRIKIANO NA WARATIBU WAO

  Masheha Zanzibar wametakiwa kushirikiana vyema na waratibu wa kupinga vitendo vya udhalilishaji ambao wanafanyakazi katika Shehia mbali mbali za Unguja   na Pemba ili changamoto zinazowakabili katika utekelezaji wa Majukumu yao ziweze kutatuliwa kwa wepesi/urahisi. Akizungumza mmoja kati Maafisa   kutoka Divisheni ya Maendeleo ya Jamii ndugu Omar Haji Omar wakati walipofika kutambulisha kazi za Idara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto katika shehia, kwa Mashesha na Waratibu wa shehia kwa Wilaya ya kati Unguja, amesema mashirikiano yao yatawezesha kutatua changamoto kwa haraka.   Amefahamisha kwamba shughuli zote za   maendeleo au changamoto ya jamii katika shehia zao zinapaswa kuripotiwa katika Wizara husika lakini mashirikiano yao yatawezesha Wizara ya maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto kufanya kazi kwa ufanisi. Amesema utaratibu huu umekuja baada ya kuundwa kwa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto ikiwa miongoni mwa shughuli zake ni kutambua na ku

WAALIMU, WANAFUNZI WESHA WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI MAPAMBANO DHIDI YA UDHALILISHAJI

  NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@ WA A LIMU na wanafunzi wa skuli ya msingi ya Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, wamesahauriwa kuongeza juhudi za kupambana na vitendo vya udhalilishaji, ili wanawake na watoto wabaki salama kwa vitendo hivyo.   Hayo yameelezwa n a Mshauri nasaha kutoka kitengo cha mkono kwa mkono cha hospitali ya Chake chake Asha Massoud, wakati akitoa mafunzo kwa wanafunzi hao, juu ya dhana ya kupambana na udhalilishaji, mafunzo yaliyofanyika skulini hapo.   A lisema kuwa, kupitia mafunzo anaamini wanafunzi na waalimu hao, wameshapata njia sahihi ya kuongeza juhudi za mapambano dhidi ya udhalilishaji.   Alieleza kuwa, kila mmoja na kwa nafasi yake, anatakiwa kukemea na kutoa elimu ya kujikinga na masuala la udhalilishaji, ili jamii na hasa kundi la wanawake na Watoto libaki salama.   ‘’Kwanza niwatake waalimu na wanafunzi wa skuli hii ya Msingi Wesha, kuhakikisha wanaongeza makali ya kukemea na kutoa taarifa wanapoona viashiria vya udhalilishaji kwa mmo