Skip to main content

Posts

Showing posts from April 9, 2023

WANASIASA PEMBA WAZIPA KONGOLE PEGAO, ZAFELA, TAMWA-ZANZIBAR

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANASIASA Kisiwani Pemba, wamesema kazi iliyofanywa na PEGAO, ZAFELA na TAMWA ya kuibua kero za wananchi na kuzifikisha eneo husika, na kisha kuchukuliwa hatua, hakuna mwanasiasa yeyote engeweza kuifanya kazi hiyo. Walisema, taasisi hizo zilifika katika wilaya zote nne za Pemba, na kukutana wananchi, wakiwemo wanawake na kuzisikiliza changamoto zao, na kisha kuzifika tasisi husika kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi. Wakizungumza kwenye mkutano maalum wa kuwasilisha utendaji kazi kwa wahamasishaji jamii hao, kupitia mradi wa kuiwezesha jamii kudai haki zao za uongozi, siasa na demokrasia, na kufanyika ofisi ya KUKHAWA, walisema kazi iliyofanywa ni kubwa. Mwenyekiti wa Chama cha wakulima cha AAFP, taifa Said Soud Said, alisema kazi hiyo anaona kusingekuwa na mwanasiasa yeyote, engeweza kuwafikia wananchi na kuchukua kero kwa lengo la kuzipatia sulhu. Alieleza kuwa, kazi hiyo inafaa kuthaminiwa na kuungwa mkono na serikali kuu, kwa kuziwezesha tasisi

SHEHA WAWI AKERWA KESI ZA UDHALILISHAJI KUFANYIWA SULHU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHEHA wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake Sharifa Wazir Abdalla, amewataka wananchi kuendelea kuziripoti kesi za udhalilishaji katika vyombo husika, na kutojihusisha na vikao vya kuzifanyia sulhu. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema kisheria kesi za udhalilishaji na za jinai kwa ujumla, hutakiwa kuripotiwa moja kwa moja, katika vyombo vya sheria. Alisema, ni kosa kwa jamii kuitisha vikao vya sulhu, kwani husababisha kuwapa nguvu wadhalilishaji, kwa vile wanakosa hukumu. Sheha huyo alieleza kuwa, kuwaripoti katika vyombo vya sheria, kutochechea makosa hayo kupungua katika jamii, ambayo huwaathiri wanawake na watoto. ‘’Kila mmoja awe mlinzi kwa mwenzake, na asikubali kushiriki katika vikao vya sulhu, iwe kwa ajili ya kuchukua fedha ama kumkimbiza mtuhumiwa,’’alieleza. Katika hatua nyingine, sheha huyo wa shehia ya Wawi Sharifa Waziri Abdalla, alisema wataendelea kutoa elimu kwa jamii, juu ya madhara ya matendo hayo. ‘’Sisi kupiti

UBAKAJI WA WATOTO, UNAVYOKIWEKA KISIWA CHA PEMBA SHAKANI

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ VIONGOZI, wanaharakati na wataalamu wa masuala ya saikolojia wameonya kuhusu athari za muda mrefu zitakazotokea kisiwani Pemba na Zanzibar kwa ujumla, endapo vitendo vya ubakaji vitaachwa bila kuchukuliwa hatua. Katika miaka ya karibuni, kumekuwa na matukio mengi ya mabinti ambao hawajafikia umri wa kuruhusiwa kushiriki ngono kubakwa, lakini wahusika kuachiwa baada ya kesi kuondolewa mahakamani. Katika mahojiano yaliyofanywa kati ya mwandishi wetu na makundi tofauti, ilielezwa kwamba hali hii ya sasa kama itaendelea, kuna hatari ya jamii ya Pemba kupata athari za muda mrefu. Moja iliyotajwa ni wingi wa watoto wasio na familia, waathiri wa ubakaji wenye msongo wa mawazo na kujengeka kwa utamaduni wa watu kutotii sheria. Mkaazi wa Shehia ya Minungwini, Maulid Saleh Hamad, anasema hofu yake kubwa, ni kwamba kuna athari nyingi zitajitokeza ikiwa ni pamoja na wabakaji kuzidi kusambaa kwenye mitaa yao na kupata nguvu zaidi ya kudhalilisha watoto. Bak

DC MTATIRO: 'WALEENI WATOTO KWA MAADILI YA TANZANIA'

  Joyce Joliga,Tunduru@@@@ Wazazi na walezi nchini wametakiwa kuwa mstari mbele katika malezi ya watoto wenye umri chini ya miaka 8 pamoja na vijana kulingana maadili ya Mtanzania. Wito huo umetolewa na mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Julius Mtatiro, wakati wa Ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika kitaifa katika Kanisa la Upendo wa Kristo Masihi Kiuma. Mtariro ameongeza kuwa Taifa linapaswa kusonga mbele likiwa salama kwa kuwalinda watoto na vijana wasiweze kuiga tabia za mataifa yaliyoporomoka kimaadili. "Wazazi wakiacha kutekeleza wajibu wao kwa watoto hatutaliokoa Taifa, na kama Yesu Kristo alibeba msalaba wake mpaka mwisho kumkomboa mwanadamu iweje wazazi washindwe kusimama kidete kwa ajili ya malezi bora ya watoto". amesema Mtatiro Pamoja na mambo mengine amewakumbusha Wananchi wa mkoa wa Ruvuma kujiwekea akiba ya chakula, badala kukiuza kabla ya msimu na kusababisha migogoro ya kifamilia. Nao baadhi ya waumini akiwemo Samwel Mzava ameshukuru viongozi kwa kuendelea ku