Skip to main content

Posts

Showing posts from March 6, 2022

JACKLIE "INTERNEWS KUENDELEA KUWANOA WAANDISHI TANZANIA"

                                                      NA HAJI NASSOR, PEMBA MKUU wa mradi jumuishi wa vyombo vya habari kanda ya Afrika kutoka shirika la kuwajengea uwezo waandishi wa habari Jacklie Jidubwi, amesema shirika hilo litaendelea kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili kuwa waledi kwa kuibua maumivu yanayowakumba watu wenye ulemavu chini. Mkuu huyo wa mradi aliyasema hayo machi 8, mwaka 2022 mjini Zanzibar wakati akiyaghairisha mafunzo ya siku2 kwa wanahabari wa Zanzibar juu ya uandishi bora wa habari za watu wenye ulemavu kupitia mradi wa jumuishi wa vyombo vya habari. Alisema Internews imevutiwa mno na kazi na mwamko walionao waandishi wa habari wa Tanzania wakiwemo wa Zanzibar kwa kuibua changamoto na madhila yanayowasakili watu wenye ulemavu. Alieleza kuwa kwa juhudi hizo za wazi wazi ndio maana shirika hilo limevutiwa na kazi hizo na kuahidi kuendelea kufanyakazi na vyombo vya habari. "Kwa hakika Internews tumevutiwa mno kuona mradi huu unatekelezwa katika nchi ka

Tukiwapa uongozi wanawake sio hidaya ni haki yao kikatiba

                                                NA HAJI NASSOR, PEMBA INAWEZEKANA wapo wanaodhani kuwa suala la kumpa uongozi mwanamke, kuanzia shehia hadi taifa, ni kama hidaya kutokwa kwa wenye mamlaka. Hidaya ni zawadi ambayo inawezekana mtu asipewe au pewe kwa mtoaji akiona ipo haja hiyo. Na wale wenye mamlaka na uwezo wa kushawishi mwanamke kupata nafasi ya uongozi, hudhani kuwa hili ni hidaya. Maana utasikia kauli kutoka kwa viongozi wanaume wakisema kuwa, kamati ya shehia fulani kama ina wajumbe 12, basi angalau wanawake wawe watatu. HALI HALISI Wanawake wanasema wamekuwa wakishuhudia kauli za kukatisha tama kuwa, hutumika maneno kama vile angalau wanawake wawili, lazima wanawake waepo. Asha Hassan Omar wa mtandao wa wanawake Mkoani anasema, imekuwa kama zawadi kutokana kwa wanaume wanapotaka kupewa nafasi. Anasema kwa karne hii tayari wameshapa uwelewa wa jinsi ya kuongoza, sasa hakuna majaribio tena kuwapa uongozi wanawake bali kama ni haki, itekelezwe. Anabainisha kuwa sheria

WAZIRI SAADA MKUYA ALIA NA MIUNDOMBINU ISIYORAFIKI KWA WATU WENYE ULEMAVU BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WAZIRI wa nchi Afisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar dk. Saada Mkuya Salim amesema bado watu wenye ulemavu wanaendelea kukabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo wanaofika baraza la wawakilishi kwa shughuli mbali mbali. Dk. Saada Mkuya aliyasema hayo Machi 7 mwaka 2022 ukumbi wa hoteli ya Maru maru mjini Zanzibar alipokuwa akifungua mafunzo ya siku2 ya uandishi wa habari za watu wenye ulemavu yalioandaliwa na Shirika la Internews kupitia mradi wa vyombo vya habari jumuishi nchini. Internews in Tanzania Alisema muhimili wa baraza la wawakilishi lilipaswa kuwa mfano mzuri wa kuweka miundombinu rafiki kwa kundi la watu wenye ulemavu ili iwe rahisi kwao wanapowagania haki zao. Alieleza kuwa hivi karibuni alimshuhudia mwanamke aliyealikwa barazani hapo akibebwa na wanaume ili kufika juu sehemu ya wageni. Internews Aidha Waziri huyo aliipongeza Internews Tanzania kwa kuwajengea uwezo waandishi wa habari katika kuibua changamoto za watu wenye ulemavu Zanzibar. Ha