Skip to main content

Posts

Showing posts from May 12, 2024

MAADHIMISHO SIKU YA UHURU WA HABARI DUNIANI, RC KUSINI PEMBA ASEMA NENO

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@@  WAANDISHI wa habari kisiwani Pemba wametakiwa kufuata maadili ya kazi zao, ili kuepuka kuingia kwenye makosa.    Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari, leo Mei 18, 2024 uliofanyika ukumbi wa Chuo cha Samail Gombani Chake chake Pemba, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, alisema mwandishi wa habari aliesomea fani ya habari hawezi kuvunja miiko na maadili.   Alisema kuwa, tasnia ya habari sasa imevamiwa na watu ambao hawakusomea fani hiyo, jambo ambalo linaweza kusababisha migogoro katika jamii na kushusha hadhi ya tasnia, hivyo ipo haja kwa waandishi wa habari kuzingatia maadili wakati wa kazi zao ili kuepuka changamoto zinazoweza kujitokeza.  "Siku hii ya uhuru wa habari ni muhimu kujitafakari kwamba tunafanya kazi kwa kiasi gani, tuna uhuru kiasi gani, vikwazo gani tunavyopitia na kupanga mikakati ya kuweza kutatua," alisema Mkuu huyo.  Mkuu huyo aliwataka waandishi hao kuibua c

ELIMU AFYA YA UZAZI KWA VIZIWI PEMBA BADO KAA LA MOTO

       NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KUANZIA mwaka 1983 hadi 1992, hatua zilichukuliwa, ikiwani pamoja na maamuzi ya mwisho ya Umoja wa Mataifa, kuitangaza Disemba 3 ya kila mwaka, kuwa siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu . Siku hiyo, pamoja na mambo mengine, kundi la watu wenye ulemavu hujadili, mafanikio na changamoto zao, zikiwemo za huduma za afya. Kisha serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliunda Mkakati wa Kitaifa wa Ujumuishi wa mwaka 2010 hadi 2015, na sera ya taifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004, ukitaja ulazima wa huduma za afya kwa watu wenye ulemavu. Ipo sera ya kitaifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2018 kwa upande wa Zanzibar, ambayo Ibara ya 20, inasisitiza uimarishwaji wa upatikanaji huduma bora na endelevu kwa kundi hilo. Serikali ilitunga sheria ya Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2010, ambapo ilikuja kuharakisha huduma bora na endelevu za afya kwao. Kwa Zanzibar, ilikuwa na sheria ya watu wenye ulemavu, nambari 9 ya mwaka 2006,

WAKULIMA WA MBOGA WAONESHWA NJIA KUKUZA KIPATO CHAO

  ASHA ABDALLA, PEMBA @@@@ WAKULIMA wa Mbogamboga na Matunda  wameshauriwa kusindika Matunda na kuusarifu Mchicha lishe ili kuimarisha Afya na  kujiongezea kipato katika soko na kuweza kuimarisha uchumi wa nchi . Ushauri huo ulitolewa na Warld vegetable centre kwa kushirikiana na ZEA chini ya mradi wa AID-I unaofadhiliwa na USAID, wakati walipokua wakipewa  Mafunzo ya nadharia na vitendo ,huko Pujini  katika kiwanda cha usindikaji  wilaya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba.  Mradi huo  ulisema unalengo la kuhakikisha wanatoa Elimu   kwa  wakulima  wadogowadogo kupitia katika mashambani mwao na darasani ili waweze kujua namana  gani wanaweza kuusarifu mchicha lishe na kusindika matunda ili kuboresha na kuongeza thamani ya mazao ya siweze  kupotea. Munira Rashid khamis ambae nimsimamizi wa masuala ya lishe na afya kutoka katika Mradi wa Warld vegetable centre aliesema kuwa ipo haja kubwa kwa wakulima wa mbogamboga na matunda  kupata uwelewa zaidi juu ya upotevu wa mazao na mbogamboga baada

MWAMBE, WATAKA UTAFITI WA KINA ONGEZEKO VITENDO VYA UDHALILISHAJI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Mwambe wilaya ya Mkoani Pemba, wameiomba serikali, kufanya utafiti wa kina kubaini sababu za kuongezeka matukio ya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto, ili kundi hilo nalo liishi kwa amani.   Walisema licha ya mikakati, mipango na maazimio ya muda mfupi na mrefu ya kutokomeza vitendo hivyo, bado vimekuwa vikishamiri siku hadi siku, jambo linalowapa wasiwasi wa kutokupungua.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, walisema hawaoni kuwa, iko siku wanawake na watoto watakuwa huru na vitendo vya ukatili na udhalilishaji, kutokana na kuongezeka siku hadi siku.   Walisema, kumekuwa na juhudi kubwa zinazofanywa na serikali kuu, kwa kushirkiana na washirika wake wa ndani na nje, jambo ambalo walitarajia kuona mabadiliko.   Maua Mwitani Ussi wa Jombwe, alisema kumekuwa na mikakati kuanzia ngazi ya familia, shehia, wilaya, mkoa, taifa na kimatifa ingawa kila siku vyombo vya habari, vinaripoti matu

MWENGE WA UHURU 2024, WATUA PEMBA UKITOKEA DAR- ES- SALAAM

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MWENGE wa uhuru wa kitaifa, umewasilileo Mei 13, 2024  katika mkoa wa kusini Pemba, kwa ajili ya kutembezwa katika wilaya za Mkoani na Chake chake, ukitokea mkoa wa Dar-es Salaam Tanzania bara.   Mwenge huo, umepokelewa katika uwanja wa ndege wa Pemba, na kupokelewa na wakuu wa mikoa ya kusini na kaskazini Pemba, wakuu wa wilaya nne za Pemba, maafisa wadhamini, viongozi wa Chama cha Mapinduzi, ‘CCM’ wa mikoa ya Pemba, wafanyakazi wa serikali na wananchi wengine.   Kabla ya Mkuu wa mkoa wa Dar-es Salaam Albert Chalamila kumkabidhi Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud mwenge huo, alisema aliupokea ukitokea mkoa wa Pwani ukiwa salama.   Mkuu huyo wa mkoa alisema, mwenge huo ukiwa ndani ya mkoa wake ulitembezwa urefu wa kilomita 427.7 kwa siku tano, na ulizindua miradi 39 yenye thamani ya shilingi bilioni 479.6.   Alieleza kuwa, pamoja na uzinduzi huo wa miradi, mwenge huo ulisababisha wananchi 994, kujitokeza kuchunguuza afya zao